MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TARI Mlingano Yaleta Mapinduzi ya Mkonge, Viungo na Sayansi ya Udongo Tanzania
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TARI Mlingano Yaleta Mapinduzi ya Mkonge, Viungo na Sayansi ya Udongo Tanzania
Habari

TARI Mlingano Yaleta Mapinduzi ya Mkonge, Viungo na Sayansi ya Udongo Tanzania

Author
By Author
Share
4 Min Read
Na Lucy Ngowi
MOROGORO: TAASISI ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) kupitia kituo chake cha Mlingano, imeonesha mafanikio makubwa katika utafiti na uvumbuzi wa kisasa unaolenga kuboresha sekta ya kilimo nchini.
Mratibu wa Utafiti na Ubunifu kutoka TARI Mlingano, Dkt. Sibaway Mwango amesema hayo alipozungumza na Mwandishi wa Habari hizi katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea mkoani Morogoro.
Dkt.Mwango amesema kupitia maonesho ya kitaifa ya kilimo yanayoendelea, TARI Mlingano imejikita kuonesha mafanikio ya kipekee katika uzalishaji wa miche bora ya mkonge, utunzaji wa vinasaba vya viungo adimu pamoja na uboreshaji wa huduma za upimaji wa udongo kupitia maabara inayotegemewa na taifa.
Kwa upande wa mkonge, amesema TARI Mlingano imefanikiwa kuzalisha miche bora milioni 2.5 ya mkonge na kusambaza kwa wakulima katika maeneo mbalimbali ya nchi.
“Mbegu chotara ya mkonge aina ya H11648, ambayo kwa sasa ndiyo msingi wa uzalishaji wa mkonge nchini, imefanyiwa utafiti na wataalam wa taasisi hiyo,” amesema.
Amesema miche hiyo inapatikana katika banda la TARI Mlingano kwenye maonesho hayo na wakulima wamehamasishwa kufika kujionea mbegu hiyo iliyoimarishwa.
Kwa sasa, TARI Mlingano ina uwezo wa kuzalisha miche ya mkonge hadi milioni 3 kwa mwaka, ingawa mahitaji ya kitaifa yanazidi miche milioni 12. Ili kuziba pengo hilo, taasisi hiyo inaendelea na ujenzi wa maabara ya kisasa ya tissue culture ambayo inatarajiwa kukamilika ndani ya mwaka huu wa fedha.
“Maabara hiyo itakapokamilika, itazalisha zaidi ya miche milioni 10 kwa mwaka, hatua itakayosaidia kutatua kabisa changamoto ya upatikanaji wa miche bora ya mkonge nchini,” amesema.
Mbali na mkonge, TARI Mlingano pia ina jukumu la kuhifadhi na kuendeleza vinasaba vya viungo muhimu vya kiuchumi ikiwemo karafuu, cocoa, mdalasini, tangawizi, iriki na all spices.
Amesemq katika eneo la zaidi ya hekta 30, taasisi hiyo imehifadhi vinasaba hivi vyenye thamani kubwa kwa uchumi wa viwanda na masoko ya kimataifa.
“Kupitia vinasaba hivyo, wameweza kuzalisha miche bora na kusambaza kwa wakulima. Mwaka huu pekee, TARI Mlingano inazalisha miche 350,000 ya karafuu na kuisambaza katika halmashauri zote za Mkoa wa Morogoro,” amesema.
Pia amesema eneo la teknolojia na huduma za sayansi ya udongo, TARI Mlingano imejivunia kuwa na Maabara Kuu ya Udongo ya Tanzania, ambayo kwa sasa ipo kwenye hatua za mwisho za kufanyiwa ithibati ya kimataifa.
Amesema maabara hiyo imekuwa mhimili muhimu kwa wakulima, watafiti na sekta binafsi, lakini kwa muda mrefu wakulima wakubwa walilazimika kupeleka sampuli zao za udongo Afrika Kusini kutokana na ukosefu wa uhakika wa ubora wa huduma za kitaifa.
Kwa mujibu wa Dkt. Mwango, maabara hiyo inatarajiwa kuongeza uwezo wake wa kupima afya ya udongo kutoka sampuli 3,000 kwa mwaka hadi zaidi ya 30,000.
“Hii itatoa fursa kubwa kwa wakulima kupata takwimu sahihi kuhusu afya ya udongo wao, na hivyo kufanya maamuzi ya kilimo kisayansi na chenye tija zaidi,” amesema.v
TARI Mlingano kwa sasa imejikita kuhakikisha matokeo ya utafiti yanamfikia mkulima moja kwa moja, ikiwa ni pamoja na kuboresha upatikanaji wa miche bora, huduma za uchunguzi wa udongo na kuendeleza vinasaba vya mazao ya viungo. Hatua hizi zinaifanya taasisi hii kuwa kitovu cha mageuzi ya kilimo chenye tija nchini Tanzania.

You Might Also Like

Biteko Amwakilisha Rais Samia Harambee Ujenzi Kanisa Katoliki

TEA Yawaalika Wananchi Kujifunza SDF Unavyofanya Kazi

Posta Yaleta   Usafiri Wa Kitalii Ndani Ya Sabasaba

Ujenzi Jengo la Sayansi, Teknolojia, Ubunifu Kuanza Kesho Dodoma

Mdemu Azindua Utafiti Uliofanywa na FES Kwa Kushirikiana Na COTWU – T

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article SADC Yatathmini Maendeleo ya Mpango wa RISDP Katika Mkutano wa 45 Madagascar
Next Article UDSM Yabuni Teknolojia Mpya ya Kuhesabu Samaki Kwa Haraka 
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mbinu Mpya za Kilimo kwa Vijana Zapata Umaarufu Nanenane Banda La VETA
Habari August 6, 2025
VETA Yatahadharisha Changamoto ya Kuzidisha Uchanganyaji wa Chakula Cha Mifugo
Habari August 6, 2025
UDSM Yaanzisha Mkakati Kuokoa Nyuki Wadogo
Habari August 6, 2025
UDSM Imekuja Na App Inayounganisha Wakulima na Watoa Huduma za Kilimo kwa Haraka
Habari August 5, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?