MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Tanzania Yanadi Nishati Kimataifa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Tanzania Yanadi Nishati Kimataifa
Habari

Tanzania Yanadi Nishati Kimataifa

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
CAPE TOWN – AFRIKA KUSINI: TANZANIA inaendelea kutangaza fursa mbalimbali za uwezeshaji katika Sekta ya Nishati ili kuifungua nchi Kimataifa.
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio amesema hayo leo Novemba tano katika Kongamano la Wiki ya Nishati 2024 linalowakutanisha
wadau wa nishati ya mafuta, gesi asilia na nishati jadidifu kutoka barani Afrika na nchi nyingine duaniani.
Amesema utangazaji huo wa nchi ya Tanzania, unaenda sambamba na mpango wa kunadi vitalu vilivyo wazi nchini kwa ajili ya utafutaji wa mafuta na Gesi Asilia.
“Tanzania inatumia kongamano hili kueleza fursa nyingine za uwekezaji katika vitalu vya utafutaji wa mafuta na gesi asilia alivyopewa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) pamoja na fursa zilizopo katika mkondo wa kati na wa chini wa petroli ikiwemo miradi ya Mini LNG.,” amesema.
Pia amesema Mamlaka ya Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) itakuwa na banda la maonesho kwa kushirikiana na TGS, huko masuala mbalimbali ya mkondo wa juu wa petroli yataoneshwa pamoja na maandalizi ya duru ya tano ya kunadi vitalu vya utafutaji mafuta na gesi asilia vilivyo wazi nchini.
Vile vile amesema kongamano hilo litavutia washiriki wengi duniani kwa kuwa limekidhi mwelekeo wa dunia wa kuondokana na nishati chafuzi za mazingira.
Amesema washiriki kutoka Tanzania wataweza kukutana na kampuni mbalimbali za mafuta na gesi asilia duniani ikiwemo Schlumber Company Ltd.
Kwa mwaka 2024, kongamano hilo ni la 30  linafanyika kuanzia Novemba nne hadi nane likihusisha wadau wa nishati zote duniani.

You Might Also Like

TRA: Serikali imemgusa mkulima kupitia mabadiliko ya sheria

CATC yawaita wakulima kusomea urushaji wa ndege nyuki

Malecela: Nitakuza Vipaji, Nitafutia Vijana Ajira Dodoma Mjini

Rasmi Leo DSM Kuanza Biashara Saa 24

Waendelezaji Majengo 103 Kesi Ziko Mahakamani, -AQRB

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mbarawa Aagiza Matumizi Ya Kitufe Utambuzi Wa Dereva
Next Article Programu Ya Mazoezi Kwa Watumishi Wizara YA Mambo Ya Ndani Yazinduliwa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari November 22, 2025
Kwagila Awataka Wasimamizi Wa Elimu TAMISEMI Kuwajibika Kikamilifu
Habari November 21, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?