Na Mwandishi Wetu, Lahti, Finland
WIZARA Ya Maliasili na Utalii imeahidi kushirikiana na Kituo kikubwa cha kuzalisha mbegu za miti katika mji wa Oitti, Lahti, Finland.
Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt.Hassan Abbas amesema hayo nchini Finland alipoongozana na Kamishna wa Uhifadhi wa Wakala wa Misitu Tanzania ( TFS), Profesa Dos Santos Silayo akiwa katika kituo hicho.
“Tanzania tuna vituo vyetu vya mbegu za miti lakini hapa tumejionea teknolojia za kiwango cha juu na kwa kuwa hapa nipo na Kamishna wa Uhifadhi wa Wakala wetu wa Misitu (TFS), Prof. Dos Santos Silayo, tumekubaliana tutashirikiana na kituo hiki kuboresha utafiti wetu na uzalishaji wa mbegu na miche ya miti nchini,,” amesema.

Kituo hicho ni miongoni mwa vituo vya mbegu vinavyoongoza Ufini na duniani kuzalisha mbegu bora za miti ya mbao na kufanya pia tafiti za mbegu za aina mbalimbali ya miti.

Pia Dkt. Abbasi na ujumbe wake walitembelea moja ya kampuni kubwa ya kutengeneza vifaa vya viwanda vya mbao cha Raute, Lahti, kinachouza vifaa vyake nchi mbalimbali duniani na kujionea teknolojia za kisasa katika sekta ya misitu.