MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: TAMWA Yawawezesha Wanawake Kupitia Mradi wa Nyuki
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > TAMWA Yawawezesha Wanawake Kupitia Mradi wa Nyuki
Habari

TAMWA Yawawezesha Wanawake Kupitia Mradi wa Nyuki

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
CHAMA cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) kimetoa mafunzo ya ufugaji wa nyuki kwa wanawake wa kijiji cha Misufini, wilayani Kibaha mkoani Pwani, ili kuwawezesha kiuchumi na kuchochea uhifadhi wa mazingira kupitia uzalishaji na usindikaji wa mazao ya nyuki.
Akizungumza wakati wa mafunzo maalum kwa waandishi wa habari, Mkurugenzi wa TAMWA, Rose Reuben, amesema hatua hiyo ni sehemu ya mpango wa kuanzisha mradi wa mfano wa ufugaji wa nyuki katika shamba la shirika hilo lililopo Misufini.
“Shamba letu liko Misufini na tunataka majirani zetu hasa wanawake wanufaike na mradi huu. Lengo ni kuwawezesha kiuchumi kupitia shughuli endelevu,” amesema
Amesema nyuki ni chanzo muhimu cha kipato kwa kutumia rasilimali zilizopo kwenye mazingira ya asili, huku akieleza kuwa asilimia 80 ya shughuli za kilimo nchini hufanywa na wanawake.
“Kupitia ufugaji wa nyuki, wanawake watapata fursa ya kujipatia kipato endelevu kutoka kwa mazao kama asali, masega, chavua na gundi,” alieleza.
Kwa hatua ya awali, TAMWA inatarajia kuweka mizinga 200 ya nyuki kwenye shamba hilo kama sehemu ya utekelezaji wa mradi.
Naye Ofisa Biashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha, Christina Samweli, amesema nyuki wana mchango mkubwa katika maisha ya binadamu, si kwa asali pekee bali pia kwa mazao mengine yenye thamani kubwa kiafya na kibiashara.
“Mazao ya nyuki kama chavua na gundi ni tiba na chakula. Lakini bado jamii nyingi hazijafahamu fursa hizi,” amesema.
Amesema wanawake kuchangamkia mafunzo hayo kwa kuwa yanatoa maarifa muhimu ya kutumia ardhi kwa tija bila kuharibu mazingira.
Aidha, ufugaji wa nyuki umetajwa kuwa ni shughuli rafiki kwa mazingira kwani hauhitaji ukataji wa miti wala matumizi ya kemikali, bali huchochea uhifadhi wa misitu na mimea.
Kupitia mradi huo wanawake wa Misufini wanatarajiwa kuwa mfano wa kuigwa katika matumizi bora ya rasilimali asilia kwa ajili ya maendeleo ya jamii na uhifadhi wa mazingira kwa vizazi vijavyo.
–

You Might Also Like

Tume Ya Mipango Yaelekeza Waandishi Wa Habari Kutoa Elimu Ya Dira Ya Taifa Ya Maendeleo 2050

Dkt. Mushongi: Mahindi Ni Nguzo Kuu ya Uchumi na Usalama wa Chakula

Tume ya umwagiliaji yapambana kuinua kilimo

Kamati Ya Bunge Ya Ustawi Na Maendeleo ya Jamii, Yaipongeza Serikali Uwekezaji Kiwanda Cha Chai

Waziri Mkuu Apongeza Huduma Kidijitali za NSSF, Maonesho Ya Madini Geita

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Nishati Safi Kwa Kila Mtanzania Inawezekana – Saidy
Next Article TARI Kibaha Yaboresha Pia Mbegu za Mazao ya Mizizi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Waziri Mkuu Majaliwa Akabidhi Tuzo kwa BoT Geita
Habari September 22, 2025
BoT Yarahisisha Uuzaji wa Dhahabu kwa Wachimbaji, Yatoa Punguzo La Mrabaha
Habari September 22, 2025
Mkuu Wa Mkoa Shinyanga Asifu Kazi Ya Bodi Bima Ya Amana
Habari September 22, 2025
REA Yapamba Maonesho Ya Kitaifa Ya Teknolojia Ya Madini Geita
Habari September 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?