MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Taasisi Za Serikali Zapewa Wiki Tano Kujiunga Na Mfumo
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Taasisi Za Serikali Zapewa Wiki Tano Kujiunga Na Mfumo
Habari

Taasisi Za Serikali Zapewa Wiki Tano Kujiunga Na Mfumo

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Danson Kaijage
TAASISI zote za Serikali zimetakiwa kuingia katika mfumo wa kielektroniki utakaowezesha mifumo ya Serikali kuwasiliana (GovESB), na ambazo hazijaingia katika mfumo huo zimepewa muda wa siku 30 ziwe zimejiunga.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ametoa maagizo hayo kwenye kilele cha Maadhimisho ya wiki ya Utumishi wa Umma, alipomwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan kwenye maadhimisho hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Chinangali Park Jijini Dodoma.
Amesisitiza taasisi zote za umma ambazo hazijajiunga na mfumo huo mwisho ni Julai 30 mwaka huu.
Amesema  mfumo huo una faida kubwa katika utumishi wa umma kwa kuwa utasaidia kurahisisha utendaji, kutoa taarifa kwa wakati, kuondoa makosa ya kibinadamu katika kuwahudumia wananchi pamoja na kuwabana wala rushwa.
“Nimefurahi kujulishwa kwamba jumla ya mifumo 223 kutoka kwenye taasisi 185 imeunganishwa na kusomana,” amesema.
Ametoa wito kwa taasisi zote za umma zenye mifumo na zinazoendelea kubuni mifumo zihakikishe mifumo hiyo inasomana na inaweza kubadilishana taarifa kupitia mfumo huo wa GovESB ikiwa ni njia mojawapo ya kuendelea kuboresha huduma za Serikali.
Pia ameitaka Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) kuhakikisha mifumo iliyounganishwa inaendelea kubadilishana taarifa.
“Lakini pia kila anayeingia jiridhishe kuwa anaweza kuwasiliana na wengine wote waliomo ndani, mmenieleza na mmesema kwamba ndivyo ilivyo, nasisitiza kwamba hakikisheni hiyo mifumo inasomana na inabadilishana taarifa,” amesema.
Pia ametoa wito kwa watumishi wa umma kuzingatia miiko na maadili ya utumishi katika utekelezaji wa majukumu yao kwa kuzingitia Sera na Sheria kwa manufaa na maendeleo ya Taifa letu.
“Nitumie nafasi hii kuwapongeza sana watumishi wote wa umma nchini, niwahikishie kuwa serikali ya awamu ya sita iko pamoja nanyi. Fanyeni hivyo kwa ajili ya manufaa na maendeleo ya Taifa letu,” amesema.
Kwa upande wake Waziri wa Nchi-Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene amesema Tanzania imetambulika kimataifa ambapo mwaka 2022 Benki ya Dunia ilifanya utafiti kuhusu ukomavu wa matumizi ya teknolojia duniani katika utoaji wa huduma za Serikali na ushirikishwaji wa wananchi.
Amefafanua kuwa ripoti ya utafiti huo iliyotolewa Machi, 2023 ilibanisha kuwa Tanzania imefanikiwa kupanda daraja kutoka kundi B hadi kundi A na kushika nafasi ya 26 duniani, nafasi ya puli Afrika na nafasi ya kwanza katika nchi za Afrika Mashariki.
Katika tukio hilo,Majaliwa alizindua mifumo miwili ambayo ni GovESB Pamoja na Mfumo wa e-Wekeza unaomwezesha Mtumishi wa Umma kuwekeza katika Mfuko wa Faida (Faida Fund).
Siku ya Utumishi wa Umma husherehekewa Juni 23 kila mwaka na nchi wanachama wa Umoja wa Afrika kwa lengo la kutambua mchango wa Watumishi wa Umma katika maendeleo ya nchi zao na Bara la Afrika kwa ujumla
Mwisho..

You Might Also Like

Masauni Kuzifanyia Kazi Changamoto Alizozibaini Katika Ziara Yake

TPHPA ina mchango mkubwa utoshelevu wa chakula – Profesa Ndunguru

Mkuu wa Mkoa akabidhi matrekta kwa wakulima kutoka Pass Leasing

CMA yawataka wafanyakazi walioachishwa kazi kuwasilisha mgogoro ndani ya muda

Makalla aitaka Halmashauri Longido kutenga fedha, ujenzi wa uzio Samia Girls

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Lukuvi Asema 2024 Bangi Ilivunja Rekodi, Tani Zaidi Ya 2000 Zilikamatwa
Next Article Kamishna TFS Aongoza Kikao Cha Viongozi Wa Kamisheni ya Misitu Afrika
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mchumi Ajitosa Kuwania Ubunge Manyoni
Habari July 1, 2025
Msomi Wa Afya, Fatuma Atia Nia Jimbo la Dodoma Mjini
Habari July 1, 2025
Dkt. Mashimba Achukua Fomu Ya Kuwania Nafasi Ya Ubunge
Habari July 1, 2025
TPHPA, MUCE Wasaini Hati Ya Makubaliano Maeneo Yanayogusa Sayansi
Habari July 1, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?