MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: SUA Yawafikia Wafugaji Wa Ng’ombe Wa Maziwa Kwa Tiba Mbadala Ya Homa Ya Kiwele
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > SUA Yawafikia Wafugaji Wa Ng’ombe Wa Maziwa Kwa Tiba Mbadala Ya Homa Ya Kiwele
Habari

SUA Yawafikia Wafugaji Wa Ng’ombe Wa Maziwa Kwa Tiba Mbadala Ya Homa Ya Kiwele

Author
By Author
Share
2 Min Read

 Na Lucy Ngowi

TANGA: WAFUGAJI wa ng’ombe wa maziwa jijini Tanga, wameshukuru kwa kupata elimu ya jinsi ya umuhimu wa usafi wakati wa kukamua ng’ombe ili kuepusha kupata homa ya kiwele iliyotolewa na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA).

Mfugaji kutoka Kata ya Mzizima, Winnie Lema amesema kupitia elimu hiyo waliyopewa kuhusu homa ya kiwele na SUA, kupitia mradi unaofadhiliwa na Kituo cha Kimataifa cha Maendeleo na Utafiti cha Canada (IDRC), imewangozea uelewa kwa kiwango kikubwa.

Amesema awali hawakuwa na elimu hiyo, hivyo imewawezesha kuyajua makosa waliyokuwa wakiyafanya bila kujua.

Mtafiti Kiongozi wa Mradi huo, Profesa Gaymary Bakari amesema mafunzo hayo yaliyohudhuriwa na wafugaji 47, yana lengo la kutoa mrejesho kwa wafugaji na kutambua changamoto wanazokumbana nazo.

“Mafunzo haya ni sehemu ya tathmini ya hali halisi ya homa ya kiwele katika mkoa wa Tanga, baada ya kufanya utafiti wa awali, sasa tumeleta mrejesho na kuwasikiliza wafugaji ili kuelewa changamoto na namna ya kuimarisha tiba tunayoendelea kuibuni,” amesema.

Naye Ofisa Mifugo kutoka Halmashauri ya Jiji la Tanga, Dkt. Rashid Chonga Nasoro, ameipongeza SUA kwa kupeleka elimu hiyo kwa wafugaji.

“Mafunzo haya yatasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza athari za homa ya kiwele. Tumejifunza njia sahihi za kukinga na kudhibiti ugonjwa huu,” amesema.

Mradi wa NANO COM unatekelezwa katika mikoa mitano nchini ambayo ni Tanga, Iringa, Mbeya, Njombe na Arusha. Tafiti katika maeneo haya zinalenga kubaini vyanzo vya homa ya kiwele na kubuni tiba mbadala kwa ajili ya wafugaji nchini Tanzania.

You Might Also Like

Kasulu Yatoa Mafunzo Utumiaji wa Mfumo Wa Kieletroniki Kwa Wakuu wa Divisheni, Vitengo

Waajiri Wasilisheni Michango Kwa Wakati

Mkongo Wa Mawasiliano Unalenga Kuleta Tija Kwa Wananchi

BOT Yafungia Applications 69 Za Mikopo Mtandaoni

Yonaz akabidhi boti ya doria kukabili vitendo vya kiuhalifu

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wanafunzi Msingi Wajitosa Kujifunza Kichina
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Wanafunzi Msingi Wajitosa Kujifunza Kichina
Habari May 12, 2025
Uchaguzi Mkuu 2025: Majimbo Mapya Nane Yaanzishwa, 12 Yabadilishwa Majina
Habari May 12, 2025
Serikali Inaboresha Miundombinu Ya Umeme Kibiti Kuondoa Changamoto Za Umeme – Kapinga
Habari May 12, 2025
Waziri Mkuu Kumwakilisha Dkt Samia Ivory Coast
Habari May 12, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?