MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: SUA Yawafikia Wafugaji Wa Ng’ombe Wa Maziwa Kwa Tiba Mbadala Ya Homa Ya Kiwele
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > SUA Yawafikia Wafugaji Wa Ng’ombe Wa Maziwa Kwa Tiba Mbadala Ya Homa Ya Kiwele
Habari

SUA Yawafikia Wafugaji Wa Ng’ombe Wa Maziwa Kwa Tiba Mbadala Ya Homa Ya Kiwele

Author
By Author
Share
2 Min Read

 Na Lucy Ngowi

TANGA: WAFUGAJI wa ng’ombe wa maziwa jijini Tanga, wameshukuru kwa kupata elimu ya jinsi ya umuhimu wa usafi wakati wa kukamua ng’ombe ili kuepusha kupata homa ya kiwele iliyotolewa na Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA).

Mfugaji kutoka Kata ya Mzizima, Winnie Lema amesema kupitia elimu hiyo waliyopewa kuhusu homa ya kiwele na SUA, kupitia mradi unaofadhiliwa na Kituo cha Kimataifa cha Maendeleo na Utafiti cha Canada (IDRC), imewangozea uelewa kwa kiwango kikubwa.

Amesema awali hawakuwa na elimu hiyo, hivyo imewawezesha kuyajua makosa waliyokuwa wakiyafanya bila kujua.

Mtafiti Kiongozi wa Mradi huo, Profesa Gaymary Bakari amesema mafunzo hayo yaliyohudhuriwa na wafugaji 47, yana lengo la kutoa mrejesho kwa wafugaji na kutambua changamoto wanazokumbana nazo.

“Mafunzo haya ni sehemu ya tathmini ya hali halisi ya homa ya kiwele katika mkoa wa Tanga, baada ya kufanya utafiti wa awali, sasa tumeleta mrejesho na kuwasikiliza wafugaji ili kuelewa changamoto na namna ya kuimarisha tiba tunayoendelea kuibuni,” amesema.

Naye Ofisa Mifugo kutoka Halmashauri ya Jiji la Tanga, Dkt. Rashid Chonga Nasoro, ameipongeza SUA kwa kupeleka elimu hiyo kwa wafugaji.

“Mafunzo haya yatasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza athari za homa ya kiwele. Tumejifunza njia sahihi za kukinga na kudhibiti ugonjwa huu,” amesema.

Mradi wa NANO COM unatekelezwa katika mikoa mitano nchini ambayo ni Tanga, Iringa, Mbeya, Njombe na Arusha. Tafiti katika maeneo haya zinalenga kubaini vyanzo vya homa ya kiwele na kubuni tiba mbadala kwa ajili ya wafugaji nchini Tanzania.

You Might Also Like

Faru Weusi, Simba, Tembo Waongezeka Ngorongoro

Zuhura Yunus Atoa Neno Kwa Madereva 

BUWSSA Yapewa Bilioni 28 Kutatua Tatizo La Maji

Mwenda: Tupo kwa ajili ya kuzitatua changamoto za wananchi

RAAWU na mafanikio iliyopata utawala wa Rais Samia

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wanafunzi Msingi Wajitosa Kujifunza Kichina
Next Article Kenya, Tanzania Zashirikiana na China Kukabiliana na Changamoto za Ushuru wa Marekani
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mchumi Ajitosa Kuwania Ubunge Manyoni
Habari July 1, 2025
Msomi Wa Afya, Fatuma Atia Nia Jimbo la Dodoma Mjini
Habari July 1, 2025
Dkt. Mashimba Achukua Fomu Ya Kuwania Nafasi Ya Ubunge
Habari July 1, 2025
TPHPA, MUCE Wasaini Hati Ya Makubaliano Maeneo Yanayogusa Sayansi
Habari July 1, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?