MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Stamico Yahimiza Ubunifu, Uaminifu Na Kujituma
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Stamico Yahimiza Ubunifu, Uaminifu Na Kujituma
Habari

Stamico Yahimiza Ubunifu, Uaminifu Na Kujituma

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Mkurugenzi Mtendaji atoa ahadi kwa wafanyakazi, wachimbaji wadogo
Na Lucy Ngowi
GEITA: MKURUGENZI Mtendaji wa Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Venancy Mwase, amewataka wafanyakazi wa shirika hilo kuendelea kuwa wabunifu, waaminifu na kujituma zaidi katika majukumu yao, huku akiahidi kuwashika mkono kwa karibu kutokana na juhudi na mafanikio wanayoendelea kuonyesha.
Amezungumza hayo  Septemba 28, 2025, wakati wa kufunga Maonesho ya Nane ya Sekta ya Madini yaliyofanyika Geita.
Habari Picha 9702
Amewapongeza wafanyakazi wa STAMICO kwa kazi nzuri wanayoifanya akisema,”Kushukuru ni jambo jema, lakini niwaambie  mnafanya kazi nzuri sana,”.
Ameahidi kuwasaidia wachimbaji wadogo hususani wanawake kwa kugawa pampu za maji kwa kusema,
“Nimeahidi mwenyewe. Kamilisheni utafiti wa mahitaji, tutaanza kutoa kwa awamu hadi akina mama wote waondokane na changamoto hiyo.”
Habari Picha 9705
Amesisitiza kuwa dhamira ya Serikali ni kuwawezesha wachimbaji wadogo wazawa hasa wanawake na vijana kupitia vifaa, elimu na miundombinu muhimu.
Pia amesema agizo la Rais Samia Suluhu Hassan la kutenga mashine inayotumika kwa ajili ya utafiti au uchimbaji wa madini (rig), moja mahsusi kwa wanawake tayari limeanza kutekelezwa, vifaa vikiwa karibu kukamilika.
Habari Picha 9706
“Tunafuata utaratibu ule ule: Crasha iko, shed iko, na sasa tunatafuta vijana wa kusaidia vikundi hatua kwa hatua,” amesema.
Mwase amesena STAMICO inaendelea kujipanga kuhakikisha inaongeza msaada mkubwa kwa wafanyakazi na wadau wa sekta ya madini.
“Kila kidogo Serikali inachotoa kupitia STAMICO, mafanikio yake yanaonekana. Kwa nini msipewe kikubwa? Hatujawahi kuangushwa.” amesema.
Habari Picha 9704
Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Chama cha Wanawake Wachimbaji Madini Tanzania (TAWOMA), Salma Ernest ametoa shukranikwa Mkurugenzi wa STAMICO kwa kusaidia utekelezaji wa Mradi wa Malika wa Madini mkoani Geita.
Mradi uliowezesha wanawake kufanyika kwa tafiti za kijiolojia, kuundwa kwa vikundi vipya vya wanawake wachimbaji, Kutoa elimu kwa zaidi ya wanawake 640, Kugawa jokarasha tano kati ya 20 zilizopo nchini, na kusaidia ushiriki wa wanawake kwenye maonyesho ya mwaka huu 2025.
“Tumetembelea mabanda yote, tumetambulika sisi ni nani na tunafanya nini. Tumekutana na mabenki na makampuni makubwa  haya yote yametokea kwa sababu umetufungulia njia,” amesema.

You Might Also Like

Zitumieni fursa za misitu na nyuki-Tafori

UDSM Chasaini Mikataba Na Kampuni Za Kichina, Kujengea Uzoefu Wanafunzi Wake

UDOM Yatafiti Dawa za Malaria, Vidonda vya Tumbo, Kisukari Kutoka Mimea ya Asili

Serikali Kuendelea Kutenga Fedha Kwa ajili ya Ukamilishaji wa Maboma ya Vituo vya Afya

Tunaunga mkono jitihada za Rais Samia katika Utalii

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TBA Yakaribisha Wawekezaji Kushiriki Miradi Mikubwa ya Ujenzi
Next Article TASAC Yapiga Marufuku Kampuni Binafsi Kusafirisha Shehena Hatarishi Za Migodini
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?