MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Spika Mussa Zungu Atoa Hotuba Baada Ya Kuchaguliwa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Spika Mussa Zungu Atoa Hotuba Baada Ya Kuchaguliwa
Habari

Spika Mussa Zungu Atoa Hotuba Baada Ya Kuchaguliwa

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: SPIKA wa Bunge Mussa Azzan Zungu, ametoa hotuba yake ya kwanza mara baada ya kuchaguliwa kuwa Spika katika mkutano wa kwanza wa Bunge la 13 jijini Dodoma.
Katika hotuba yake, Spika Zungu ameshukuru Chama Cha Mapinduzi (CCM) pamoja na Mwenyekiti wa Chama hicho, Rais Samia Suluhu Hassan, kwa imani waliyomuonesha kwa kumteua kugombea nafasi ya uspika kwa tiketi ya CCM.
“Ninasimama kwa mara ya kwanza nikiwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Namshukuru sana Mwenyekiti wa Chama changu, Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan, kwa kuniamini na kuchagua jina langu kugombea uspika wa CCM,” amesema.
Amesema kuwa licha ya wengi kuwania nafasi hiyo ndani ya chama, CCM iliamua kumpa dhamana hiyo kubwa, jambo analoliona kama heshima na wajibu wa kulitumikia Taifa kwa bidii.
Aidha, Spika Zungu amewashukuru wabunge wote waliompigia kura, akisema ushindi huo ni wa wabunge wote bila kujali itikadi zao.
“Nathamini sana kura na imani mlizonipa. Ushindi huu ni wetu sote. Naahidi kuwatumikia wabunge wote kwa usawa bila ubaguzi wowote. Ofisi ya Spika itakuwa wazi kwa kila mbunge,” amesema.
Pia amemshukuru Spika aliyemaliza muda wake, Dkt. Tulia Ackson, ambaye kwa sasa ni Rais wa Umoja wa Wabunge Duniani (IPU), kwa uongozi wake bora na mchango mkubwa alioutoa katika kuliongoza Bunge.
Spika Zungu ameahidi kushirikiana kwa karibu na Naibu Spika pamoja na Mwenyekiti wa Bunge katika kuhakikisha Bunge linafanya kazi zake kwa ufanisi, kuheshimu taratibu na kutoa maazimio yenye manufaa kwa wananchi.
“Tutahakikisha Bunge letu linaendelea kuwa chombo cha ushauri, usimamizi na uwakilishi wa kweli wa wananchi,” amesema.

You Might Also Like

JOWUTA Yataka Sheria Za Kazi Kuwalinda Wafanyakazi Katika Vyombo Vya Habari

Maliasili Yapongezwa Kwa Kutekeleza Maono Ya Rais Samia  

Teknolojia Mpya Ya Uchomeleaji Yaleta Mapinduzi VETA Dodoma

Wizara Ya Madini Kununua Chopa, Kufanya Utafiti

Waziri Mkuu Mstaafu Pinda Atoa Neno Kwa Vijana, Maadhimisho Miaka 30 VETA

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mbunge wa Monduli Aahidi Kusimamia Changamoto za Jimbo Lake
Next Article Kadogosa: Serikali Yatenda Haki Kwa Wakulima, Wafugaji, Wananchi Wa Vijijini
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari November 22, 2025
Kwagila Awataka Wasimamizi Wa Elimu TAMISEMI Kuwajibika Kikamilifu
Habari November 21, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?