MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Simbachawene: Simu za mkononi zinaondoa umakini kwa watumishi wa umma
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Simbachawene: Simu za mkononi zinaondoa umakini kwa watumishi wa umma
Habari

Simbachawene: Simu za mkononi zinaondoa umakini kwa watumishi wa umma

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Simbachawene: Simu za mkononi zinaondoa umakini kwa watumishi wa umma
Na Mwandishi Wetu
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene amesema watumishi wengi wa umma wamepoteza umakini kutokana na kushika simu za mkononi ambazo zinawafanya wasahau majukumu yao kwa muda husika.
Simbachawene amesema hayo wakati akifunga semina ya Waajiri na Viongozi wa Matawi ya Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania ( TUGHE).
“Tunaenda nchi za wenzetu tunaona hawaingii na simu za mkononi ofisini, simu zinawekwa akitoka ndio anachukua na kufanya mawasiliano.
“Sisi watanzania matumizi ya simu yanatumika sivyo ofisini. Makundi yenyewe ni mengi. Kuna kundi la vikoba, la familia, ulilomaliza nao chuo, makundi chungu nzima. Kwa hali hii utahudumia watu saa ngapi?,” amehoji.
Anasema wapo watumishi wanaojitetea ni wafanyakazi wa kazi za ofisini, lakini na muuguzi naye ana makundi amemwekea mgonjwa drip, muuguzi huyo anaendelea kuchati.
Amesema likiwekwa katazo la matumizi ya simu za mkonono ofisini, mgogoro utakuwa ni mkubwa.
“Kama kuna kitu kinachoharibu afya zeru, ukishagusa simu ukitaka kulala usingizi unakata. Tumeathirika na simu, umakini wa kazi unapotea ukishika simu,”amesema.
Amesema watumishi wa umma wasipojikita kufanya kazi kwa bidii, kwa umakini nchi haitasonga mbele.
Kwa upande mwingine amesema watumishi wakitambua wao ni kioo cha jamii ni lazima wavae mavazi yanayokubalika kwa mujibu wa sheria.
Amesema isipowekwa sheria kali za watumishi wa umma,itakuwa kama maeneo mengine duniani.
“Watumishi wa umma baadhi yetu wanavaa vibaya hawajali kanuni za uvaaji. Tukumbuke sisi ni kioo cha jamii lazima uvae vazi linalokubalika kwa mujibu wa sheria.
“Nitamwelekeza Katibu Mkuu kutoa waraka maalum juu ya mavazi ya utumishi wa umma. Kwani huwezi mtumishi wa umma ukaacha bega wazi,” amesema.
Naye Katibu Mkuu Tughe, Hery Mkunda amesema lengo la semina ni kutoa uelewa wa pamoja kati ya waajiri na wafanyakazi sehemu za kazi.
Amesema hilo llitaboresha na kuondoa changamoto.

You Might Also Like

Uzinduzi wa Ubia Wiki Ya Ubunifu Tanzania 2025 Wafanyika

Mkuu Wa Mkoa Shinyanga Asifu Kazi Ya Bodi Bima Ya Amana

Samia: Sera Iliyozinduliwa, Somo La Ujasiriamali Ni Lazima

Wataalam wa “Visit Finland” Wabadilishana Uzoefu Kutangaza Utalii Duniani 

Mwalim: Ardhi Yetu ni Ufunguo wa Uhuru wa Kiuchumi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Ujenzi Miundombinu ya Kuongeza Udahili kipaumbele Cha Serikali
Next Article Tanzania yajipanga kutumia nishati ya nyuklia kuzalisha umeme
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

CAG Aipongeza TARURA Kwa Ujenzi Wa Miundombinu
Habari January 9, 2026
Tuna Deni La Kusimamia Miradi Na Kusikiliza Kero za wananchi Ili Kuleta Maendeleo Ya Kweli-Salome
Habari January 9, 2026
Rais Dkt Samia Azindua Majengo Ya Kisasa
Habari January 8, 2026
TEA, UNICEF Watekeleza Miradi ya Elimu Visawani Zanzibar
Habari January 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?