MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Silinde Akabidhi Nyaraka za Kufungua Masoko Mapya Nje ya Nchi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Silinde Akabidhi Nyaraka za Kufungua Masoko Mapya Nje ya Nchi
Habari

Silinde Akabidhi Nyaraka za Kufungua Masoko Mapya Nje ya Nchi

Author
By Author
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DODOMA: NAIBU Waziri wa Kilimo David Silinde amekabidhi nyaraka za kufungua masoko mapya kwa mazao ya kipaumbele tisa  ili kuondoa vikwazo vya usafi mimea vinavyokwamisha usafirishaji wa mazao nje ya nchi.
Silinde amekabidhi nyaraka hizo katika hafla ya Uzinduzi wa Masoko wa Kufungua Masoko Mapya ya Mazao ya Kipaumbele kwa Mwakilishi wa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Salvatory Mbilinyi jijini Dodoma.
Ameyataja mazao hayo kuwa ni parachichi, ndizi, tumbaku, viazi mviringo, vanilla, nanasi, karafuu, pilipili manga na kakao.
Amesema amewasilisha nyaraka hizo za ufunguzi wa mazao kwa nchi ambazo fursa zake za masoko kwenye mazao hayo ya kipaumbele bado hazijafikia kutokana na uwepo wa masharti tangulizi ambayo yanapaswa kutimizwa kabla ya kuanza kusafirisha mazao.
“Hatua hii itawezesha kuondoa vikwazo vya usafi mimea kwa sasa vinakwamisha usafirishaji  wa mazao hayo kwenye  nchi lengwa.
“Hiki kinachofanyika leo  ni maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan kuhakikisha kwamba tunakuwa  na masoko ya uhakika katika mazao yanayotokana  na kilimo,” amesema.
Ametaja nchi hizo kuwa ni China inahitaji vanilla na nanasi, Indonesia karafuu, Singapore karafuu, Israeli parachichi, Malaysia parachichi, Canada pilipili manga.
Nchi nyingine ni Uturuki nanasi, Brazil nanasi, Marekani kakao, Afrika Kusini ndizi, Zambia viazi mviringo, Pakistan tumbaku na Iraki tumbaku.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Afya ya Mimea na Viuatilifu Tanzania  (TPHPA), Profesa Joseph Ndunguru amesema taarifa ambazo nchi kwa kawaida huomba zinapopokea pendekezo la kufikia soko ni pamoja mimea iliyopendekezwa.
Pia Maeneo ya uzalishaji, wadudu wanaohusishwa na bidhaa iliyopendekezwa, usimamizi wa baada ya kuvuna na mpango wa sasa wa kuuza nje.
Amesema TPHPA inahakikisha kwamba hatua za ndani za usafi wa mazingira zinaoanishwa na viwango vya kimataifa kama vilivyowekwa na Mkataba wa Kimataifa wa Kulinda Mimea.
“TPHPA husaidia kuhakikisha kuwa bidhaa za kilimo za ndani zinaweza kushindana katika masoko ya kimataifa, na kuondoa vikwazo vya kiufundi katika biashara,” amesema.

You Might Also Like

SUA Chatumia Ngamia Mafunzo Ya Vitendo Kwa Wanafunzi

Dkt Biteko Ampongeza Mwanafunzi Aliyeelezea Miradi Ya Umeme

RC Chalamila, Wasaidizi Wake Kukutana na Kadogosa Kuzungumzia Ujenzi Wa Reli Dar

Wakulima wametakiwa kuzingatia matumizi sahihi ya mbolea

MOI Yaeleza Sababu Viungo Bandia Kuuzwa Kwa Bei Kubwa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wastaafu Epukeni Matapeli Kwenye Mafao-PSSSF
Next Article Masoko mapya nje ya nchi kuipatia nchi sh. trilioni 10
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
PURA Yajipanga Gesi Asilia Itumike Kwenye Magari
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?