MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Shule 216 Za Serikali Zatumia Nishati Safi Ya Kupikia – Kapinga
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Shule 216 Za Serikali Zatumia Nishati Safi Ya Kupikia – Kapinga
Habari

Shule 216 Za Serikali Zatumia Nishati Safi Ya Kupikia – Kapinga

Author
By Author
Share
2 Min Read

Na Danson Kaijage

DODOMA: NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga amesema hadi kufikia Machi 2025 takribani Shule za Serikali 216 zimehamia katika matumizi ya nishati safi ya kupikia ambapo kati ya hizo, Sekondari 146 zinatumia gesi ya LPG.

Kapinga ameyasema hayo Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Liwale, Zuberi Mohamedi Kuachauka aliyeuliza ni lini majiko yanayotumia gesi yataanza kutumika kote nchini.

“Serikali kupitia REA inaendelea kutoa ruzuku ya ujenzi wa miundombinu ya nishati safi ya kupikia kwa shule nyingine na Aprili 20, 2025,

REA kupitia Wizara ya Nishati imepokea kibali kutoka TAMISEMI cha kufunga miundombinu ya huduma ya nishati safi ya kupikia katika shule 115 zikiwemo shule za Mikoa za sayansi za wasichana 16, shule za kitaifa za wavulana 7, shule za bweni za kawaida 66 na shule kongwe za sekondari 26”. Amesema Kapinga

Amesisitiza kuwa Serikali kupitia REA na wadau mbalimbali itaendelea kufunga miundombinu ya nishati ya kupikia katika shule za sekondari kulingana na upatikanaji wa fedha.

Kapinga ameongeza kuwa Wizara ya Nishati kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza miradi ya kufunga mifumo ya nishati safi ya kupikia Jeshi la polisi na Magereza katika Mikoa 24, jeshi la Zima Moto pamoja na huduma za Wakimbizi.

Aidha, amesisitiza kuwa upo mkakati wa kufunga mifumo ya nishati safi ya kupikia katika Taasisi zilizo chini ya Wizara ya afya ikiwemo hospitali za Mikoa, za Wilaya na za kitaifa takribani 21.

Wakati huo huo akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Tunza Malapo aliyetaka kufahamu ni nini mkakati wa Serikali kuhakikisha shule, Zahanati na Vituo vya afya vipya vinajengwa vikiwa na mifumo ya nishati safi ya kupikia.

Akijibu swali hilo Kapinga amesema kupitia mkakati wa nishati safi ya kupikia ambao utekelezaji wake umeanza kutekelezwa, Serikali inaelekea kwenye mtazamo huo wa Shule, Zahanati na Vituo vya afya kujengwa sambamba na miundombinu ya nishati safi ya kupikia.

You Might Also Like

Katiba Na Sheria Kutoa Kipaumbele Kusikiliza Malalamiko Ya Wananchi

Ridhiwani Awashika Mkono Wenye Mahitaji Maalum

Dkt. Komba: Mfumo wa kidijitali utaleta tija kwa mkulima

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’

Elimu Itolewe Kuhusu Ufahamu Wa Kuwepo Kwa Fedha Maalum – Ridhiwani

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Ridhiwan Atembelewa Na Watendaji NMB
Next Article Mtindi wa Korosho, Stafeli Wafanyiwa Utafiti UDSM
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Waziri Mkuu Majaliwa Akabidhi Tuzo kwa BoT Geita
Habari September 22, 2025
BoT Yarahisisha Uuzaji wa Dhahabu kwa Wachimbaji, Yatoa Punguzo La Mrabaha
Habari September 22, 2025
Waziri Mkuu Apongeza Huduma Kidijitali za NSSF, Maonesho Ya Madini Geita
Habari September 22, 2025
Mkuu Wa Mkoa Shinyanga Asifu Kazi Ya Bodi Bima Ya Amana
Habari September 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?