MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Serikali Yazindua Soko Kuu Jipya la Kariakoo Baada ya Moto wa 2021
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Serikali Yazindua Soko Kuu Jipya la Kariakoo Baada ya Moto wa 2021
Habari

Serikali Yazindua Soko Kuu Jipya la Kariakoo Baada ya Moto wa 2021

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: RAIS wa Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Februari 8, 2026 amefungua rasmi Soko Kuu Jipya la Kariakoo jijini Dar es Salaam, akisisitiza kuwa mradi huo ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuimarisha mazingira ya biashara, kuongeza tija ya uchumi na kulinda mitaji ya wafanyabiashara.
Rais Dkt. Samia amesema ujenzi wa soko hilo ni matokeo ya dhamira ya Serikali ya kurejesha Soko la Kariakoo baada ya soko la awali kuteketea kwa moto Julai 2021, kwa kufanya ukarabati na kujenga soko jipya linalokidhi viwango vya usalama, ubora na mahitaji ya biashara ya kisasa.
Amehimiza uendeshaji wa soko hilo kuzingatia misingi ya ufanisi, nidhamu na ushindani wa haki, akibainisha kuwa Kariakoo ni mhimili wa biashara ya kitaifa na kikanda, na kitovu muhimu cha uchumi kinachowaunganisha wazalishaji, wasambazaji, wauzaji na wanunuzi kutoka ndani na nje ya nchi.
Vilevile, Rais Dkt. Samia ameipongeza Ofisi ya Waziri Mkuu – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), makandarasi na wasimamizi wa mradi kwa kujenga miundombinu yenye ubora wa hali ya juu, ikiwemo mifumo ya usalama na huduma za kijamii.
Ameuelekeza uongozi wa soko kuendelea kuimarisha mazingira rafiki kwa wanawake wafanyabiashara, ikiwemo huduma za mama na mtoto.
Katika kuhakikisha uendeshaji wenye tija, Rais Dkt. Samia amesisitiza umuhimu wa mifumo thabiti ya zimamoto, uokoaji na dharura, pamoja na upangaji rasmi wa ratiba za kushusha na kupakia mizigo ili kupunguza msongamano na kurahisisha biashara.
Akihitimisha, Rais Dkt. Samia amesema Soko Kuu Jipya la Kariakoo ni uwekezaji wa kimkakati wa Taifa unaopaswa kulindwa na kusimamiwa kwa ufanisi, ili liendelee kuwa injini ya uchumi na mfano wa masoko ya kisasa barani Afrika.

You Might Also Like

TMDA Kudhibiti Bidhaa Za Tumbaku Ili Wananchi Wasiendelee Kupata Madhara

Kamati Ya Bunge Yaridhishwa Na Utaratibu Wa Manunuzi Ya Bando

Ridhiwan Azindua Jengo La Biashara La TUCTA-Arusha

Ndejembi Akabidhiwa Ofisi Na Dkt. Biteko Aliyekuwa Naibu Waziri Mkuu Na Waziri Wa Nishati

Mjadala wa Kidiplomasia Ya Kisayansi Wafanyika Marekani

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TALGWU Yaipongeza Timu Ya Makatibu Wa Mikoa Na Mawakili Wa Kanda Kwa Kutoa Huduma Bora Kwa Wanachama
Next Article CWT Yaiomba Serikali Kurekebisha Sheria za Vyama vya Wafanyakazi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mavunde: Makaa ya Mawe Ni Injini ya Maendeleo ya Viwanda
Habari March 30, 2026
Programu Mpya ya TPHPA Yalenga Usalama wa Mazao Sokoni
Habari March 30, 2026
CHAKUHAWATA Yaimarisha Ulinzi wa Haki za Walimu, Yafikia Wanachama 49,750
Habari March 29, 2026
Upungufu wa Wataalamu wa Ustawi wa Jamii Wachangia Changamoto Kwenye Huduma za Jamii
Habari March 28, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?