MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Serikali Kuendelea Kutatua Changamoto Sekta Ya Uwekezaji Nchini
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Serikali Kuendelea Kutatua Changamoto Sekta Ya Uwekezaji Nchini
Habari

Serikali Kuendelea Kutatua Changamoto Sekta Ya Uwekezaji Nchini

Author
By Author
Share
2 Min Read

Na Lucy Lyatuu, Dodoma

WAZIRI wa Fedha,  Balozi Khamis Mussa Omar  amewaahidi wawekezaji kuwa Serikali itaendelea kutatua changamoto zinazoikabili sekta ya uwekezaji nchini kwa manufaa ya pande zote mbili kutokana na manufaa ya sekta hiyo kwa uchumi wa nchi na wawekezaji.

Balozi Omar amesema hayo mjini Dodoma, alipokutana na kufanya mazungumzo na Uongozi wa Kampuni mpya ya Uchimbaji Dhahabu Nyanzaga (Nyanzaga Mining Company Ltd), unaojengwa katika eneo la Nyanzaga Wilaya ya Sengerema Mkoani Mwanza ambao hadi kukamilika kwake unatarajiwa kugharimu zaidi ya dola za Marekani milioni 523.

Habari Picha 11181

Amesema  mradi huo ni mkubwa kujengwa Tanzania toka miaka zaidi ya 18 iliyopita ambapo mgodi wa Buzwagi ulijengwa.

“Ni mara yangu ya kwanza kukutana na uongozi wa mgodi wa dhahabu wa Nyanzagi na tumejadili kuhusu changamoto ya msamaha wa kodi na nimewaahidi kuwa hadi mwisho wa mwezi Februari, 2026, tutahakikisha changamoto hiyo inafanyiwa kazi kwankishirikiana na wadau wote wanaohusika” amesema  Balozi Omar.

Akizungumza kwa niaba ya ujumbe wa Mgodi huo, Meneja Mtendaji wa Ndani wa mradi wa Nyanzaga, Isaac Lupokela, ameishukuru Serikali Kupitia Waziri wa Fedha, kwa namna inavyoshughulikia masuala ya kufanikisha biashara na uwekezaji nchini.

Amesema kuwa Mgodi wa Dhahabu wa Nyanzaga, unatarajiwa kuanza uzalishaji ifikapo robo ya kwanza ya mwaka wa fedha 2026/2027.

Habari Picha 11180

Amesema kuwa Mmradi huo mpaka sasa wakati shughuli za ujenzi zinaendelea umetoa fursa za ajira za moja kwa moja na kupitia makandarasi takribani 2,000 ambao zaidi ya  asilimia 80 ni Wanzania.

Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu anayesimamia Sera za Uchumi, Elijah Mwandumbya, na kwa upande wa mwekezaji, walikuwepo Lee-Anne de Bruin – Ofisa Mkuu wa Fedha wa Kampuni Mama ya Australia (Perseus Mining Limited) na Mwneja Mkuu wa Ujenzi wa Mgodi wa Nyanzaga Matt Cavedon

You Might Also Like

NIT Yajivunia Uanzishwaji Chuo Cha Marubani

SANGU: e-Utatuzi Italeta Mapinduzi katika utoaji Haki

TEA Yatathmini Utekelezaji na Kupanga Mwelekeo Mpya Kupitia Baraza la Wafanyakazi

Aprili 2025 Matokeo Awamu Ya Kwanza, Maoni Dira Ya Taifa Na Maendeleo 2050 Kutolewa

Mbogamboga Na Vitunguu Vyaingiza Sh. Milioni 370 Kwa Miaka Minne

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Makamu wa Rais Azindua Mpango wa Kukuza Ujuzi, Ajira kwa Vijana
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Makamu wa Rais Azindua Mpango wa Kukuza Ujuzi, Ajira kwa Vijana
Habari February 9, 2026
Serikali yazindua Sera ya Taifa ya Kinga ya Jamii na ‘Hifadhi Scheme’ kwa Waliojiajiri
Habari February 9, 2026
CWT Yaiomba Serikali Kurekebisha Sheria za Vyama vya Wafanyakazi
Habari February 9, 2026
Serikali Yazindua Soko Kuu Jipya la Kariakoo Baada ya Moto wa 2021
Habari February 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?