MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Serikali imejipanga Mkakati wa Taifa wa Matumìzi ya nishati safi ya kupikia – Mramba
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Serikali imejipanga Mkakati wa Taifa wa Matumìzi ya nishati safi ya kupikia – Mramba
Habari

Serikali imejipanga Mkakati wa Taifa wa Matumìzi ya nishati safi ya kupikia – Mramba

Author
By Author
Share
2 Min Read
Ma Lucy Ngowi
DODOMA: KATIBU Mkuu wa Wizara ya Nishati, Felchesmi Mramba amesema serikali imejipanga kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia (2024 – 2034) ikiwemo kutoa elimu kwa wananchi ili kufikisha lengo la asilimia 80 ya Watanzania kutumia nishati hiyo katika kipindi cha miaka 10.
Mramba amesema hayo alipotembea banda la Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwenye maonesho ya Wakulima, Wafugaji na Wavuvi yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma.
Amesema Serikali imeandaa Mkakati wa Taifa wa matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia ambao unatoa mwelekeo wa nchi wa kuhamia katika matumizi ya nishati safi ya kupikia kutokana na faida zake mbalimbali.
Amezitaja faida hizo kuwa ni pamoja na  kuepusha wananchi na magonjwa yanayotokana na moshi unaotokana na  matumizi ya kuni na mkaa wa asili.
“Serikali ya Tanzania kupitia Sera mbalimbali za Kitaifa na Kimataifa inatambua umuhimu wa matumizi ya nishati safi ya kupikia kama nyenzo muhimu ya kukabiliana na athari za kimazingira, kiafya, kijamii na kiuchumi.
“Jitihada hizo za kuelekea kwenye matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia zinafanyika kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ikiwemo sekta binafsi.” amesema.
Kuhusu Maonesho ya Wakulima ya Nanenane, amesema kuwa yamekuwa ni sehemu ya wananchi kujionea utekelezaji wa miradi mbalimbali katika Sekta ya Nishati ikiwemo miradi ya Gesi Asilia na Mafuta.
Katika hatua nyingine, amesema Sekta ya Nishati inafungamanisha Sekta nyinginezo ikiwemo Madini, Maji, Kilimo na Mifugo ambapo katika Mifugo vinyesi vya wanyama hutumika kuzalisha nishati kwa ajili ya matumizi mbalimbali.
Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Dkt. James Mataragio ameipongeza Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa kuendelea kutoa elimu  kwa wananchi kuhusu mafanikio ya Sekta ya Nishati pamoja na Nishati Safi ya Kupikia.

You Might Also Like

Waziri Mkuu Majaliwa Amwakilisha Dkt.Mpango Mahafali Ya 43 OUT

Msigwa Azikumbusha Taassisi Za Serikali, TANROAD Ikielezea Mafanikio Yake

Stamico Yapewa Tuzo Na FDH Kujali Wenye Ulemavu

Tido Mhando: Marufuku Kuwasilisha Vyeti, Nyaraka Za Kughushi Maombi ya Ithibati, Press Card

Mfumo Wa Kuwabana Wachafuzi Wa Choo umetengenezwa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article AU yataka vyombo vya habari Afrika, kulinda Uhuru wa vyombo vya habari 
Next Article Wakulima wafunzwa kuhusu mlipuko wa panya TPHPA
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Waziri Mkuu Majaliwa Akabidhi Tuzo kwa BoT Geita
Habari September 22, 2025
BoT Yarahisisha Uuzaji wa Dhahabu kwa Wachimbaji, Yatoa Punguzo La Mrabaha
Habari September 22, 2025
Waziri Mkuu Apongeza Huduma Kidijitali za NSSF, Maonesho Ya Madini Geita
Habari September 22, 2025
Mkuu Wa Mkoa Shinyanga Asifu Kazi Ya Bodi Bima Ya Amana
Habari September 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?