MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Sekta Ya Madini Yazidi Kuchangia Ukuaji Wa Uchumi – Majaliwa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Sekta Ya Madini Yazidi Kuchangia Ukuaji Wa Uchumi – Majaliwa
Habari

Sekta Ya Madini Yazidi Kuchangia Ukuaji Wa Uchumi – Majaliwa

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
GEITA: WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amesema sekta ya madini inaendelea kuwa mhimili muhimu wa ukuaji wa uchumi nchini, baada ya kufanikisha ukuaji wa asilimia 10.9 mwaka 2022 na kuchangia asilimia 10.1 kwenye Pato la Taifa mwaka 2024, kutoka asilimia 9.0 mwaka uliopita.
Majaliwa allmesema hayo kwenye uzinduzi wa Maonesho ya Nane ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan, mkoani Geita.
Amesema mafanikio hayo yametokana na juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita, hasa katika kuimarisha mifumo ya ukusanyaji mapato, udhibiti wa biashara ya madini na matumizi ya teknolojia kama mfumo wa online mining cadastre, pamoja na kuanzishwa kwa masoko ya madini na ufuatiliaji wa mikataba ya uwekezaji.
Habari Picha 9531
“Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuboresha mazingira ya uwekezaji katika sekta hii ili kuhakikisha madini yanachangia maendeleo ya kiuchumi kwa Watanzania wote,” amesema Majaliwa.
Ametoa wito kwa wadau wa sekta ya madini kuwekeza zaidi kwenye teknolojia ili kuongeza tija katika shughuli za utafiti, uchimbaji, usafishaji na biashara ya madini.
“Teknolojia ni msingi wa maendeleo ya sekta hii. Bila teknolojia, hatuwezi kuongeza tija, kulinda mazingira, wala kuhakikisha usalama wa wachimbaji,” amesema.
Akizungumzia mafanikio ya wachimbaji, Majaliwa amesema kuwa kati ya mwaka 2021 hadi 2025, wachimbaji wadogo mkoani Geita wamezalisha zaidi ya kilo 22,000 za dhahabu zenye thamani ya Sh. trilioni 3.44, huku Serikali ikivuna Sh. bilioni 235.5 kupitia mrabaha.
Kwa upande wa makampuni makubwa, Geita Gold Mine na Buckreef wamezalisha jumla ya kilo 76,530 za dhahabu zenye thamani ya Sh. trilioni 11.38 na kuipatia Serikali zaidi ya Sh. bilioni 793 kama mrabaha.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini, Yahya Samamba, ameongeza kuwa Tanzania sasa ina viwanda vya kuzalisha vifaa vya uchimbaji, na kwamba katika mwaka wa fedha 2024/2025 uzalishaji wa dhahabu umefikia tani 62 kiwango kinachoiweka Tanzania miongoni mwa wazalishaji watano bora wa dhahabu barani Afrika.
Naye Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shigela, amesema Serikali imefanya kazi kubwa ya kusambaza umeme vijijini, hususan katika maeneo ya wachimbaji wadogo, ili kuwawezesha kufanya shughuli zao kwa ufanisi zaidi.
“Tumehakikisha maeneo mengi ya wachimbaji wadogo yamefikishiwa umeme, kufuatia maelekezo ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan,” amesema Shigela.

You Might Also Like

TARI Yaleta Mapinduzi Kilimo cha Minazi

Sierra Leone Yaipongeza TARURAUjenzi Wa Madaraja, Barabara Za Mawe

Ridhiwani Kikwete Akagua Maandalizi ya Kilele Mbio za Mwenge Jijini Mwanza

Msisubiri Kupewa Amri, Ufanyaji Usafi Kwenye Maeneo Yenu – Lugendo

Profesa Nombo Azindua Miongozo Ya Usimamizi Ya Utafiti, Ubunifu COSTECH

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Waziri Mkuu Majaliwa Akabidhi Tuzo kwa BoT Geita
Next Article Mgodi Wa Dhahabu Wa Nyanzaga Kunufaisha Wananchi, Ujenzi Wazidi Kupaa
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

CAG Aipongeza TARURA Kwa Ujenzi Wa Miundombinu
Habari January 9, 2026
Tuna Deni La Kusimamia Miradi Na Kusikiliza Kero za wananchi Ili Kuleta Maendeleo Ya Kweli-Salome
Habari January 9, 2026
Rais Dkt Samia Azindua Majengo Ya Kisasa
Habari January 8, 2026
TEA, UNICEF Watekeleza Miradi ya Elimu Visawani Zanzibar
Habari January 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?