MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Ridhiwani Azindua Mifumo Ya Kielektroniki Na Miongozo YA Kazi, Ajira, Ulemavu
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Ridhiwani Azindua Mifumo Ya Kielektroniki Na Miongozo YA Kazi, Ajira, Ulemavu
Habari

Ridhiwani Azindua Mifumo Ya Kielektroniki Na Miongozo YA Kazi, Ajira, Ulemavu

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Ridhiwani Kikwete, amezindua rasmi miongozo mitatu na mifumo miwili ya kielektroniki yenye lengo la kuboresha uratibu, usimamizi na utoaji wa huduma katika sekta za kazi, ajira, vijana na watu wenye ulemavu.
Habari Picha 9096
Uzinduzi huo umefanyika leo Agosti 22, mwaka 2025 jijini Dodoma,  ambapo Waziri Ridhiwani amesema hatua hiyo ni sehemu ya jitihada za Serikali katika kuimarisha huduma kwa kutumia teknolojia ya kisasa.
Habari Picha 9092
Amesema miongozo na mifumo hiyo inalenga kujenga msingi wa majadiliano jumuishi na yenye tija baina ya wadau wa kazi, pamoja na kuimarisha usimamizi wa mawakala wa ajira, kuhakikisha haki za watu wenye ulemavu zinalindwa, na kuwezesha ukusanyaji wa taarifa sahihi za soko la ajira kwa kutumia mifumo ya kidijitali.
Miongozo iliyozinduliwa ni pamoja na Mwongozo wa Majadiliano baina ya Serikali, Vyama vya Wafanyakazi na Vyama vya Waajiri wa mwaka 2025, Mwongozo wa Uratibu wa Vyama vya Watu Wenye Ulemavu wa mwaka 2025, pamoja na Mwongozo wa Wakala Binafsi wa Ajira wa mwaka 2025.
Habari Picha 9093
Pia mifumo ya kielektroniki iliyozinduliwa ni Mfumo wa Kitaifa wa Taarifa za Soko la Ajira wa mwaka 2025 na Mfumo wa Usimamizi wa Mashauri ya Usuluhishi na Uamuzi wa mwaka 2025.
Waziri Ridhiwani amesema mifumo hiyo itawezesha utatuzi wa mashauri ya kazi kwa haraka, kuongeza uwazi, na kusaidia wananchi hususan wanawake, vijana na watu wenye ulemavu  kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji na maendeleo ya taifa.
Habari Picha 9094
Ametumia nafasi hiyo kuwashukuru wadau mbalimbali kwa ushirikiano wao katika maandalizi ya miongozo na mifumo hiyo.
Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Mary Maganga amesema uandaaji wa miongozo hiyo ulikuwa wa kushirikisha wadau mbalimbali.
Ambao ni Shirika la Kazi Duniani (ILO), Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA), Shirikisho la Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Shirikisho la Vyama vya Watu Wenye Ulemavu (SHIVYAWATA), pamoja na Chama cha Mawakala Binafsi wa Ajira (TRAA).
Kwa upande wake, mwakilishi wa Katibu Mkuu Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Rashid Mtima amesema wafanyakazi wana imani kubwa na serikali kutokana na hatua ya kupandisha mishahara kwa asilimia 35 mwaka huu, hatua ambayo imeongeza ari kwa wafanyakazi kuelekea uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29 mwaka huu.
Habari Picha 9098
Naye Mwenyekiti wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE),  Patricia Shao amesema chama hicho kitaendelea kushirikiana na Serikali na wadau wengine wa sekta ya ajira kuhakikisha Tanzania inakuwa na nguvu kazi bora na yenye tija.
Amesema  kuwa miongozo hiyo inalenga kufanikisha lengo hilo.

You Might Also Like

TPHPA: Toeni taarifa mapema milipuko ya kwelea kwelea, nzige, viwavijeshi vamizi inapotokea

Dendego Achangisha Bilioni 1.7, Ujenzi Ofisi Ya CCM

Hivi Ndivyo Vipaumbele Vya Maliasili

Dkt. Komba: Mfumo wa kidijitali utaleta tija kwa mkulima

Wenye Ulemavu Wa Ngozi Wakumbukwa Kupitia FDH, Wapewa Msaada Wa Milioni 20

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Warsha Ya Luban Yaleta Mapinduzi Ya Elimu Ya Ufundi Nchini Tanzania
Next Article JOWUTA Yawasilisha Ripoti ya Ukaguzi kwa Msajili
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Majaliwa Apongeza Jeshi La Magereza Kurasimisha Ujuzi Kwa Wafungwa
Habari August 27, 2025
Mapokezi Ya Katibu Mkuu CCM  Dkt Migiro CCM, Aahidi Ushirikiano
Habari August 27, 2025
Majaliwa Aagiza Kuimarishwa kwa Mafunzo ya Ufundi Stadi Nchini
Habari August 27, 2025
VETA Yaanzisha Kozi Mpya ya Teknolojia ya Mifumo ya Viwandani
Habari August 26, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?