MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Polisi Kata Kupewa Pikipiki Nchi Nzima Kuimarisha Ulinzi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Polisi Kata Kupewa Pikipiki Nchi Nzima Kuimarisha Ulinzi
Habari

Polisi Kata Kupewa Pikipiki Nchi Nzima Kuimarisha Ulinzi

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Mwandishi Wetu
GEITA: SERIKALI inaendelea kuboresha utendaji kazi wa Polisi Kata na Shehia kwa kuwajengea vituo vya Polisi na kuwapatia vitendea kazi zikiwemo pikipiki nchi nzima ili watekeleze majukumu yao kwa urahishi.
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni amesema  hayo Mkoani Geita katika hafla ya kukabidhi pikipiki 50 zenye thamani ya Tsh Milioni 175 zilizotolewa na mgodi wa Geita Gold Mine (GGML).
Amesema Serikali inatambua kazi nzuri inayofanywa na Polisi  Kata na Shehia kwa kuwa wamesaidia kuimarisha usalama katika jamii.
Masauni amesema serikali kupitia bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi ya mwaka 2024/2025 imepanga na kutenga bajeti ya Bilioni 224 kwa ajili ya miradi ya maendeleo ili kukamilisha, kuendeleza na kuanza ujenzi wa ofisi, vituo na makazi ya askari.
Pia  kuongeza vitendea kazi vya kisasa katika kutoa huduma ikiwemo magari, pikipiki, boti na helkopta.
“Hadi sasa, Serikali imenunua Magari 384 kwa ajili ya utekelezaji wa kazi za Polisi kuanzia Makao Makuu ya Polisi hadi Wilaya, pikipiki 107 kwa ajili ya Polisi Kata na Shehia nchi nzima ikiwa ni lengo la Serikali kuhakikisha Jeshi la Polisi linapata vitendea kazi vya kutosha katika ngazi zote,” amesema.
Kwa upande mwingine Waziri Masauni amewapongeza mgodi wa Geita Gold Mine (GGML), na wadau wote ambao wamekuwa wakishirikiana na Wizara kupitia Jeshi la Polisi kwa kutoa michango mbalimbali ya kuliwezesha Jeshi hilo kutimiza majukumu yake ya kusimamia usalama wa raia na mali zao.
Naye Makamu wa Rais wa Geita Gold Mine, Terry Strong amesema anatarajia pikikipi hizo zitumike katika utoaji huduma za Polisi kwa wananchi katika maeneo ambayo yamekuwa hayafikiki kwa urahisi.
Kwa Upande wake Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martine Shigela ameshukuru mgodi huo kwa namna ambavyo wamekuwa wakitumia sehemu ya faida yao kuboresha taasisi za Serikali ikiwemo Jeshi la Polisi ambapo leo Kukabidhiwa pikipiki 50.
Pia  Mkuu wa Sera Mipango na Bajeti wa Jeshi la Polisi, Justus Kamugisha ambaye amemuwakilisha Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini, amesema pikipiki hizo zinakwenda kusaidia Polisi Kata 50 huku akibainisha kuwa Mkoa huo una idadi ya Kata 123.

You Might Also Like

Maofisa Tarafa na Watendaji wa Kata Waaswa kuwa wabunifu

Wadau wa Kisekta watakiwa kukabiliana na athari za mvua msimu 2024/25

Chuo Cha VETA Chazindua Mradi Wa Biogas

TFRA yazindua Chama cha wafanyabiashara wa Mbolea

Profesa Anangisye Atoa Neno Kwa Wahitimu

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Biteko – Asisitiza Umuhimu Wa Mifumo Thabiti Ya Nishati Jadidifu Kukidhi Mahitaji Ya Nishati
Next Article Tanzania Kujifunza Teknolojia Ya Magari Ya Umeme Singapore- Biteko
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?