MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Ofisa wa TARI Kuwapo Kila Kituo cha Umwagiliaji – Naibu Katibu Mkuu
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Ofisa wa TARI Kuwapo Kila Kituo cha Umwagiliaji – Naibu Katibu Mkuu
Habari

Ofisa wa TARI Kuwapo Kila Kituo cha Umwagiliaji – Naibu Katibu Mkuu

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA; NAIBU Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo anayesimamia Umwagiliaji na Zana za Kilimo, Athumani Kilundumya ametoa agizo kwa Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI), kuhakikisha kila kituo kinachowekezwa kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji kinakuwa na Ofisa kutoka TARI.
Amesema hayo katika Maonesho ya Nanenane ya Kitaifa na Kimataifa yanayoendelea Mkoani Dodoma.
Amesema lengo ni kuhakikisha tafiti zinazofanyika zinatumika moja kwa moja kwa wakulima waliopo maeneo husika.
Amesema uamuzi huo ni sehemu ya mkakati wa serikali wa kubadilisha kilimo kutoka cha kutegemea mvua kuwa kilimo cha kisasa cha umwagiliaji, kinachotegemea maarifa ya kitaalamu na teknolojia ya kisasa.
“Nataka TARI katika kila kituo tunachowekeza kwa ajili ya umwagiliaji, kuwe na Ofisa wao.
“Hii itahakikisha tafiti zao haziishii makabatini bali zinawafikia wakulima moja kwa moja,” amesema Kilundumya.
Ameongeza kuwa ni lazima tafiti za kilimo ziwafikie wakulima walio vijijini, si tu kwenye makongamano ya wataalamu.
“Tutumie sana tafiti hizi, tusiendelee na kilimo cha mazoea. Tukiwaelimisha wakulima wetu kutumia maarifa haya, tija itaongezeka hata kwa maeneo madogo,” amesema.
Naye Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Dkt. Edwin Mhende amesema matumizi ya mbegu bora zilizofanyiwa utafiti ndiyo njia ya kuleta uhakika wa chakula nchini.
“Kinachoweza kufanya uendelevu wa uhakika wa chakula ni matumizi ya mbegu bora zilizofanyiwa utafiti. Tunapongeza kazi nzuri ya TARI, wameleta maboresho makubwa kwenye sekta ya mbegu,” amesema.
Hata hivyo, Dkt. Mhende amesisitiza kuwa ni lazima mbegu hizo ziwe za gharama nafuu ili wakulima wengi waweze kumudu kuzinunua.
“Tusiishie kusema mbegu ni bora. Je, mkulima anapataje hiyo mbegu? Tuwekeze kuhakikisha gharama zinashuka, na mbegu hizo ziweze kuhimili mazingira kwa miaka mingi ijayo,” amesemq.
Awali Mkurugenzi Mkuu wa TARI, Dkt. Thomas Bwana, alisema kuwa taasisi hiyo imejikita kufanya utafiti wa kina kuanzia afya ya udongo, matumizi ya mbegu bora, hadi hatua za kuongeza thamani ya mazao.
“Lengo letu ni kuongeza tija ya kilimo. Katika msimu huu wa Nanenane, tunatoa elimu hiyo kwenye mabanda yote ya TARI kote nchini,” amesema.

You Might Also Like

Ujenzi wa Majengo Mapya 67 Ya Halmashauri Yamekamilika-Mchengerwa

Wagonjwa Wenye Maumivu Makali Kupatiwa Tiba Radiolojia MNH

Sagini Amwelezea Kaluta Amir Abeid Ni Alama Ya Kuigwa

Rais Samia Aungwe Mkono Ajenda Ya Nishati Safi Ya Kupikia-Makongoro Nyerere

Rais Samia akunwa na Tarura

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mbinu Mpya za Kilimo kwa Vijana Zapata Umaarufu Nanenane Banda La VETA
Next Article Bundi Wasaidia Kupambana na Panya: Teknolojia Asilia Inayobadili Maisha ya Wakulima
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

CAG Aipongeza TARURA Kwa Ujenzi Wa Miundombinu
Habari January 9, 2026
Tuna Deni La Kusimamia Miradi Na Kusikiliza Kero za wananchi Ili Kuleta Maendeleo Ya Kweli-Salome
Habari January 9, 2026
Rais Dkt Samia Azindua Majengo Ya Kisasa
Habari January 8, 2026
TEA, UNICEF Watekeleza Miradi ya Elimu Visawani Zanzibar
Habari January 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?