MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: OCPD Nguzo Kuu ya Utungaji Sheria – Dkt. Ndumbaro
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > OCPD Nguzo Kuu ya Utungaji Sheria – Dkt. Ndumbaro
Habari

OCPD Nguzo Kuu ya Utungaji Sheria – Dkt. Ndumbaro

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: WAZIRI wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro amesema kuwa Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria (OCPD) ni mhimili muhimu, wa lazima katika mchakato mzima wa utungaji, urekebishaji na ufasili wa sheria nchini,
Hivyo  bila ofisi hiyo hakuna sheria inayoweza kuwasilishwa bungeni kwa ajili ya kutungwa.
Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro amesema hayo alipotembelea banda la OCPD katika Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara yajulikanayo kama  Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Dkt. Ndumbaro amesema OCPD ndiyo inayoratibu mchakato wa kuandaa miswada, kuifanyia marekebisho na kuifasili kwa lugha nyepesi na ya kueleweka kwa wananchi.
“Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria ni kiungo muhimu katika mchakato wa utunzi wa sheria kuu na ndogo. Bila ofisi hii hakuna sheria itakayokwenda bungeni, hakuna urekebishaji wa sheria wala ufasili wake. Ni ofisi ya msingi katika mfumo wa sheria wa nchi,” amesema.
Amesema kuwa ofisi hiyo pia ina jukumu la kufasili sheria kutoka lugha ya Kiingereza kwenda Kiswahili, jambo linalowezesha wananchi wengi zaidi kuelewa sheria zinazowaongoza. Kufikia Juni 30 mwaka huu 2025, tayari sheria 300 kati ya 446 zimefasiliwa na kazi hiyo inaendelea.
“Kwa sasa wanafanya kazi nzuri ya kuhakikisha sheria zote zinapatikana kwa lugha ya Kiswahili. Hii itarahisisha upatikanaji wa haki na uelewa wa sheria kwa wananchi,” amesema.
Dkt. Ndumbaro ameeleza kuwa Serikali imetenga fedha za kutosha katika mwaka huu wa fedha ili kuhakikisha kazi ya ufasili wa sheria zote inakamilika kabla ya mwisho wa mwaka huu wa kalenda, ikiwa ni hatua muhimu ya kuweka sheria katika lugha ya Taifa kwa matumizi ya wote.
Kwa upande wake, Mwandishi wa Sheria kutoka OCPD, Philemon Mrosso, amesema ofisi hiyo inashiriki maonesho ya SABASABA kwa lengo la kutoa elimu kwa wananchi kuhusu mchakato wa utungwaji wa sheria pamoja na kuelezea majukumu yake.
“Tunawahamasisha wananchi kushiriki katika uundwaji wa sheria kupitia wawakilishi wao bungeni na pia kutoa maoni kuhusu sheria zinazowagusa moja kwa moja. Tumepokea maoni mengi na tutaendelea kuyachakata kwa ajili ya maboresho,” amesema Mrosso.
Amesema ofisi hiyo ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha ufasili wa sheria zilizobaki pamoja na kanuni zake ili zipatikane kabla ya mwezi Oktoba mwaka huu 2025 kwa matumizi rasmi.

You Might Also Like

Wakulima Wa Zabibu Wakiri Bidhaa Zilizoongezwa Thamani Zina Soko

Wanawake Pelekeni Batiki Kwenye Soko Huru La Afrika

Serikali Inaendelea Kutekeleza Mradi wa Kupeleka Umeme Grid Ya Mtwara Na Lindi- Kapinga

JMAT Yatoa Neno Yanayoendelea Kwa Vijana Wa Kenya

TEA, TotalEnergies Marketing Ltd Wakabidhi Madawati 130 Wilayani Kibiti

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Pato la Mwananchi Lapanda Tabora
Next Article Johari Ataka Ufasili wa Sheria za Uchaguzi Ukamilike
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?