MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Ntonda Ameipongeza TEA Kwa Utekelezaji Bora Wa Miradi Ya Elimu
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Ntonda Ameipongeza TEA Kwa Utekelezaji Bora Wa Miradi Ya Elimu
Habari

Ntonda Ameipongeza TEA Kwa Utekelezaji Bora Wa Miradi Ya Elimu

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
´Na Mwandishi Wetu
DAR ES SALAAM: NAIBU Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo,  Methusela Ntonda ameipongeza Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) kwa utekelezaji mzuri wa miradi ya maendeleo ya elimu kupitia Mfuko wa Elimu wa Taifa pamoja na Mfuko wa Kuendeleza Ujuzi (SDF).
Ntonda ametoa pongezi hizo alipotembelea banda la TEA katika ufunguzi wa Maonesho ya Kitaifa ya Kazi za Utamaduni na Sanaa yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja Mkoani Dar es Salaam.
Akiwa kwenye banda hilo, Ntonda alipata fursa ya kujionea shughuli mbalimbali zinazotekelezwa na TEA, zikiwemo taarifa za miradi ya elimu na Mfuko wa Kuendeleza Ujuzi, pamoja na bidhaa zilizotengenezwa na mmoja wa wanufaika aliyepata ufadhili wa kusomea Mafunzo ya Kuendeleza Ujuzi.
Vile vile Ntonda amevutiwa na juhudi za Mamlaka hiyo katika kuboresha miundombinu ya kujifunzia na kufundishia, sambamba na uwezeshaji uliotolewa kwa watanzania kupitia ufadhili wa mafunzo ya ujuzi.
Amesema uwekezaji uliofanywa kupitia mifuko yote miwili una mchango mkubwa katika kuleta maendeleo ya sekta ya elimu na kukuza maarifa kwa wananchi, hasa vijana.
Pia amesisitiza umuhimu wa kuendeleza jitihada hizo kwa kushirikisha wadau mbalimbali ili kuhakikisha elimu bora na fursa za ujuzi zinapatikana kwa watu wengi zaidi nchini.
Awali, akitoa utambulisho wa Mamlaka hiyo, Ofisa Uhusiano na Mawasiliano wa TEA, Eliafile Solla alisema TEA ilianzishwa kwa lengo la kusimamia Mfuko wa Elimu wa Taifa, ambapo majukumu yake makuu ni kutafuta rasilimali fedha kutoka kwa wadau wa ndani na nje ya nchi,
 Kuzitumia kusaidia juhudi za Serikali katika kuboresha miundombinu ya elimu nchini. Aliongeza kuwa TEA pia ina jukumu la kuratibu na kusimamia utekelezaji wa miradi ya uendelezaji ujuzi kupitia Mfuko wa SDF.

You Might Also Like

Program Ya Maeneo Yaliyochakaa Nchini Yaandaliwa

Rais Samia akagua gwaride maalum

Dar Sasa Kufanya Biashara Saa 24, Kuanza Februari 22 Mwaka Huu

CMA yawataka wafanyakazi walioachishwa kazi kuwasilisha mgogoro ndani ya muda

Profesa Kitila Ataja Sababu Za Watanzania  Kumchagua Dkt Samia

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article JOWUTA : Waandishi Vitendeeni Haki Vyama Vyote
Next Article Spika Tulia Kufungua Kongamano La Uhuru Wa Wanataaluma Afrika UDSM
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari November 22, 2025
Kwagila Awataka Wasimamizi Wa Elimu TAMISEMI Kuwajibika Kikamilifu
Habari November 21, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?