MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Nishati Safi Kwa Kila Mtanzania Inawezekana – Saidy
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Nishati Safi Kwa Kila Mtanzania Inawezekana – Saidy
Habari

Nishati Safi Kwa Kila Mtanzania Inawezekana – Saidy

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: MKURUGENZI Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Hassan Saidy amesema kufikia mwaka 2034, zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania wanaweza kuwa wanatumia nishati safi ya kupikia, kutokana na mipango madhubuti ya Serikali na uwekezaji mkubwa unaoendelea kufanyika.
Akizungumza katika maonesho ya Kimataifa ya Kilimo ya Nane Nane 2025 yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni, Jijini Dodoma, Saidy amesema Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, imeanza kutekeleza kwa vitendo Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi kwa kipindi cha zaidi ya miaka minne sasa.
Amesena juhudi hizo zimehusisha uwekezaji mkubwa wa rasilimali fedha, muda na teknolojia, hatua ambayo imeongeza mwamko wa wananchi kutumia teknolojia za kisasa za nishati safi.
Amewashauri Watanzania kuchagua aina ya nishati safi inayolingana na uwezo wao wa kifedha, kwani fursa za kuchagua zipo.
“Nishati safi ni pamoja na umeme, gesi ya majumbani, gesi asilia, mkaa mbadala, kuni mbadala na gesi vunde. Aina hizi zinapatikana lakini matumizi yake yanategemea hali ya uchumi wa mtu binafsi. Ndiyo maana tunasisitiza watu kuchagua kwa uangalifu kulingana na uwezo wao,” amesema.
Ametaja baadhi ya miradi mikubwa iliyotekelezwa na Wakala huo ikiwemo, Kuwezesha Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kutumia nishati safi ya kupikia katika kambi 22 nchini, kwa gharama ya Sh. Bilioni tano.
Uwezeshaji wa maeneo 211 ya Jeshi la Magereza kutumia nishati safi, kwa gharama ya Sh. Bilioni 35.2.
Kusaini mkataba na Kampuni ya Taifa ya Madini (STAMICO) kwa ajili ya uzalishaji wa mkaa mbadala.
“Hii inaonesha dhamira ya Serikali kuhakikisha taasisi zake nazo zinakuwa mfano katika matumizi ya nishati safi,” amesema.
Amehamasisha wananchi kutembelea banda la REA lililopo katika eneo la Wizara ya Nishati, Hema Na. 2 (Government Pavilion No. 2), upande wa Kusini Mashariki wa viwanja vya maonesho ya Nzuguni, ili kupata elimu kuhusu nishati safi na teknolojia zake.
Ameeleza pia kuhusu fursa zinazotolewa na Serikali kupitia REA, ikiwa ni pamoja na utoaji wa mikopo nafuu kwa ajili ya ujenzi na uendelezaji wa vituo vidogo vya bidhaa za mafuta (Petroli na Dizeli) vijijini, pamoja na maendeleo makubwa ya usambazaji umeme katika vijiji na vitongoji nchini kote.

You Might Also Like

Makalla aitaka Halmashauri Longido kutenga fedha, ujenzi wa uzio Samia Girls

Rais Samia kufungua mkutano wa Mawaziri wa Uvuvi

RC Chalamila Ataka Reli Za Ndani Ya Mkoa Kusafirisha Abiria, Kupunguza Msongamano

Tanzania, Uingereza Kushirikiana Kuendeleza madini.

CCM Kuwezesha Wananchi Kufuatilia Mkutano Mkuu Maeneo Ya Wazi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Bodi ya Maziwa Yatoa Mafunzo ya Ubora, Usalama wa Maziwa Katika Maonyesho ya Nane Nane
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Bodi ya Maziwa Yatoa Mafunzo ya Ubora, Usalama wa Maziwa Katika Maonyesho ya Nane Nane
Habari August 7, 2025
Balozi wa Tanzania Nchini Italy Afurahishwa  Ubunifu wa TPHPA Maonesho ya Nanenane
Habari August 7, 2025
Wadau Wakaribishwa Kuwekeza Katika Uchakataji, Biashara ya Mkonge Nchini
Habari August 7, 2025
Mramba Afungua Mafunzo Ya Teknolojia Ya Nishati Jua Kwa Watalaam
Habari August 7, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?