Na Lucy Lyatuu,Dodoma
BODI Ya Maji,Bonde La Ziwa Victoria imebainisha kuwa kuingia Kwa mifugo mingi katika vyanzo vya Maji huchangia kwa winging kuchafuka Kwa Maji ya ziwa hilo ambalo Lina ukubwa wakilomita za mraba 154,000.
Mkurugenzi wa Bodi hiyo, Dkt Renatus Shinhu amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa Idara ya Habari Maelezo na kufafanua fursa mbalimbali zipatikanazo chini ya Bonde hilo.

Amesema mbali ya changamoto hiyo lakini pia kilimo pembezoni nacho kumekucha chanzo kikubwa cha kuchafuka Kwa Maji ya Ziwa hilo Kwa kukaa michanga na matope hivyoo akiwaomba Wananchi kutofanya hivyo.
Amesema kutokana na changamoto hiyo kuna haja ya kuendelea kuelimisha jamii Ili kufahamubathari za kuchafuka Maji hayo,lakini wao wenyewe kushiriki katika kulinda Maji hayo ambayo Yana umuhimu mkubwa kwao na jamii Kwa ujumla.
Amesema maji ya Ziwa hilo yanategemewa Kwa kiwango kikubwa na Wananchi Kwa ajili ya matumizi ya kunywa na pengine hata kumwagilia hivyo jitihada za kuyalinda na kutunza vyanzo vya Maji zinahitajika Kwa winging.
“Zaidi ya asilimian51 ya Maji ya Ziwa hutumikankwa ajili ya kunywa,pia ziwa linatumika Kwa ajili ya uzalishaji kiuchumi,umwagiliaji na hata utalii hivyo ni jukumu la Bodi na Wananchi Kwa ujumla kulitunza Ili maendeleo yaendelee kuwepo,” amesema Dkt Shinhuna kuongea kuwa Ziwa hilo linashirikisha pia nchi tati za Afrika Mashariki na pia linaingiliana na Bonde La Mto Nile.
Ameongeza kuwa Kwa sasa Bodi hiyo Ina vituo 90 Kwa ajili ya kusimamia mwelekeo wa Maji Ili kujua yapo kiasi Gani na ubora lakini pia husimamia ugawaji wa Maji Kwa Wananchi Kwa kutoa vibali.
Amesema pia Bodi imetoa vibali zaidi ya 1000 vya matumizi ya Maji Kwa jamii na kwamba wanagawa Maji kuzingatia matumizi ya binadamu lakini pia wakijalo mazingira.

