Na Mwandishi Wetu
WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu- Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu. Ridhiwani Kikwete amesema maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Uelewa Kuhusu Albino, hufanyika kila mwaka kukumbusha umuhimu wa kushirikisha wenye Ualbino,

Haki zao pamoja na umuhimu wa serikali kuendelea kuangalia maslahi na ulinzi wao.
Maadhimisho hayo yaliongozwa na
Kassim Majaliwa Majaliwa , Waziri Mkuu katika viwanja wa Mwanga Mkoani Kigoma Juni 13, 2025.
Ridhiwani amesema katika maadhimisho hayo ulizinduliwa mtandao maalum wa kusajili watu wenye Ulemavu unaowezesha kusajili kwa njia ya eletroniki hata kwenye maeneo yaliyo nje ya mtandao.

“Mfumo huu unawezesha taarifa za watu wenye ulemavu kuchukuliwa na kuchambuliwa ambapo zitaiwezesha serikali kupata taarifa za kina zitakazowezesha kupanga mipango ya maendeleo ikiwemo kuwashirikisha wenye Ulemavu,” amesema.

Amesema katika maadhimisho hayo, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa alitoa maagizo maalum kwa wakuu wa Mikoa na wadau waliokuwapo kuhusu matumizi sahihi ya mtandao huo.
