MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mazao Ya Mikunde Yatajwa Kuwa Na Kiwango Kikubwa Cha Protini
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mazao Ya Mikunde Yatajwa Kuwa Na Kiwango Kikubwa Cha Protini
Habari

Mazao Ya Mikunde Yatajwa Kuwa Na Kiwango Kikubwa Cha Protini

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
MOROGORO: MTAFITI wa mazao jamii ya mikunde kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo  Tanzania (TARI), Mussa Tamba ameshauri wakulima na wananchi kutumia mazao ya mikunde katika lishe kwa kuwa yana kiwango kikubwa cha protini.
Tamba  ambaye ametoka Kituo cha TARI Ilonga kilichopo Kilosa Morogoro amesema hayo alipozungumza na Mwandishi wa Habari hii, katika Maonesho ya kilimo ya nanenane mwaka huu 2025, Kanda ya Mashariki yanayoendelea mkoani Morogoro.
Ametaja mazao hayo kuwa  ni mbaazi, kunde, dengu, njugu mawe, choroko, na soya.
Ameeleza kuwa zao la soya lina asilimia 37 hadi 40 ya protini na mafuta karibu asilimia 22. Pia lina madini ya chuma na zinko kwa wingi, ambayo ni muhimu kwa afya ya binadamu.
Amesema Katika maonesho ya kilimo yanayoendelea, TARI Ilonga imewasilisha teknolojia ya mbegu bora na elimu juu ya kanuni bora za kilimo cha mikunde ili kuongeza tija kwa mkulima.
“Kwa upande wa mbaazi, kuna aina saba zilizogawanywa katika makundi matatu kulingana na muda wa kukomaa.
“Muda mfupi wa miezi minne, mbegu aina ya Komboa  haitegemei msimu na inaweza kupandwa wakati wowote ikiwa kuna chanzo cha maji.
“Muda wa kati ya miezi sita, Tumia mbegu aina ya Ilonga 14 M1 na Ilonga 14 M2 , hupandwa msimu wa masika nchini nzima lakini si zaidi ya mita 1900 kutoka usawa wa bahari.
“Muda mrefu wa miezi tisa mbegu aina ya Karatu, Kiboko na Mali. hazifai kupandwa mikoa ya Pwani kutokana na  hali ya hewa,” amesema.
Amesema mazao mengine kama chorizo, kunde na soya pia yana aina mbalimbali zinazopendekezwa kulingana na maeneo na misimu ya mvua.
Akielezea Choroko ametaja aina nne kuwa ni Nuru, Imara, TARIGRAM 1, TARIGRAM 2,  hukomaa kwa siku 65 hadi 70 na hustawi vizuri hadi mita 1500 kutoka usawa wa bahari.
Pia Kunde ambazo zimegawanyika katika makundi mawili, zisizotambaa ni Vuli 1, Vuli 2 ambazo hukomaa kwa siku 65-70.
Zinatambaa ni Fahari, Raha 1, Raha 2, Tumaini, Vuli AR 1 na Vuli AR 2 ambazo hukomaa kwa miezi mitatu na hupendekezwa kupandwa masika. Vuli AR 1 na 2 zina uwezo wa kukinzana na magugu na wadudu wa gugu chawi.
Amesema soya zipo aina nne
Ambazo ni Uyole Soya 1 hadi 4 , Uyole Soya 2 inapendekezwa zaidi ukanda wa mashariki, hususan msimu wa masika. Zao hili linahitaji unyevu wa kutosha.
Amehimiza wakulima kufuata kanuni bora za kilimo kama kupanda kwa nafasi sahihi, matumizi ya dawa za kuzuia na kutibu magonjwa ya mimea, na kuchagua aina bora za mbegu kulingana na eneo.

You Might Also Like

Bodi ya mkonge kutoa ajira kwa watu 10,000 ifukapo 2030

UDSM Yaja Na Bajaji Inayotumia Maji Na Mafuta

Serikali Kuendelea Kutenga Fedha Kwa ajili ya Ukamilishaji wa Maboma ya Vituo vya Afya

Rais Samia aungwa mkono na Tughe, watalii 800 watua Ngorongoro

Afya Bora Yachochea Ustawi wa Wananchi Kigoma

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mchome: Ubunifu wa VETA Ni Mkubwa, Sasa Ni Wakati Wa Uzalishaji Kwa Wingi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mchome: Ubunifu wa VETA Ni Mkubwa, Sasa Ni Wakati Wa Uzalishaji Kwa Wingi
Habari August 8, 2025
TARI Kibaha Yaboresha Pia Mbegu za Mazao ya Mizizi
Habari August 7, 2025
TAMWA Yawawezesha Wanawake Kupitia Mradi wa Nyuki
Habari August 7, 2025
Nishati Safi Kwa Kila Mtanzania Inawezekana – Saidy
Habari August 7, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?