MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Majaliwa Afurahishwa Na Ustadi Wa Vijana Wenye Ulemavu Veta
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Majaliwa Afurahishwa Na Ustadi Wa Vijana Wenye Ulemavu Veta
Habari

Majaliwa Afurahishwa Na Ustadi Wa Vijana Wenye Ulemavu Veta

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi 

MBEYA: WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa ameonesha kufurahishwa na juhudi za Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) katika kuwawezesha vijana wenye mahitaji maalum kwa kuwapatia elimu ya ufundi stadi itakayowawezesha kujitegemea na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya taifa.

Majaliwa ameonyesha furaha hiyo alipotembelea banda la VETA katika Maadhimisho ya Kitaifa ya Vijana Yanayoendelea mkoani Mbeya, ambapo alishuhudia vijana wenye ulemavu wakionyesha umahiri wao katika ushonaji wa nguo na teknolojia ya kompyuta.

Akizungumza mbele ya Waziri Mkuu, Balozi wa VETA katika Kitengo cha Watu Wenye Mahitaji Maalum, Francis Anthony, ambaye ni fundi na sasa mwalimu wa kompyuta, amesema alihitimu mafunzo ya kitaalamu kupitia VETA na kwa sasa anawafundisha wengine.

“Nilianza kama mwanafunzi, sasa ninafundisha. Huu ni uthibitisho kuwa VETA imewajengea uwezo vijana wenye mahitaji maalum,” amesema Anthony.

Naye Riziki Ndumba, mwanafunzi kutoka VETA Songea anayesomea ushonaji, amesema alianza bila ujuzi wowote lakini kupitia msaada wa walimu na viongozi wa chuo, amehitimu kozi ya miaka miwili kwa mafanikio.

“Nataka kuwa mfano kwamba hata sisi wenye ulemavu tunaweza kufanya kazi na kujitegemea,” amesema.

Kwa upande wake, Ofisa Uhusiano kwa Umma kutoka VETA Makao Makuu, Elmer Sarao, amesema taasisi hiyo inaendelea kuwekeza katika kuwafikia vijana wote, wakiwemo wenye ulemavu.

Amesema mmoja wa walimu waliopo sasa ni mhitimu mwenye ulemavu aliyesoma VETA kuanzia mwaka wa kwanza hadi wa tatu, na sasa anafundisha katika chuo cha mafunzo Morogoro.

“Huyu ni mfano hai kuwa ulemavu si kikwazo cha ufanisi. Tunajivunia kuwalea na kuwaendeleza vijana hawa,” amesema Sarao.

Kwa mujibu wa VETA, uwepo wa vijana wenye mahitaji maalum katika vyuo vyao ni sehemu ya mkakati wa serikali kuhakikisha hakuna anayeachwa nyuma katika kujenga taifa lenye nguvu kazi jumuishi, mahiri na yenye tija.

 

 

 

 

 

 

 

 

You Might Also Like

Mpanduji Wa COTWU – T Aelezea Changamoto Zinazowakabili Waendesha Bodaboda, Bajaji

Malecela: Nitakuza Vipaji, Nitafutia Vijana Ajira Dodoma Mjini

COSTECH yazindua program kuwajengea uwezo wanawake kidijitali

TARI: Mabadiliko Ya Tabia Nchi Yamepunguza Ufanisi Wa Mbegu

Salum Mwalim: Nitarejesha Hadhi ya Kanda ya Ziwa na Kuinua Zao la Pamba

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wanawake 1,063 Wahitimu Mafunzo Ya Ujuzi VETA Mbeya Kupitia Mpango Wa Rais Samia
Next Article Mamlaka Ya Elimu Tanzania Yaimarisha Ushirikiano Na Wadau Wa Maendeleo Ya Elimu
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mita  Janja Zazinduliwa,  Tanesco  Yatakiwa Kuzisambaza Nchi Nzima
Habari December 5, 2025
DIT Andaeni Taarifa  Itakayowezesha Wanafunzi Kupelekwa Nje Kujifunza-Mkenda
Habari December 5, 2025
Msama Aipongeza Hotuba Ya Samia, Atoa Neno Kwa Vijana, Wazee, Wanaharakati
Habari December 4, 2025
Profesa Silayo Aaga, Jawara Kuchukua Uongozi Mpya wa AFWC25
Habari December 3, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?