MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: MAIPAC Yasisitiza Maadili Na Usalama Kwa Waandishi Wa Habari
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > MAIPAC Yasisitiza Maadili Na Usalama Kwa Waandishi Wa Habari
Habari

MAIPAC Yasisitiza Maadili Na Usalama Kwa Waandishi Wa Habari

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
ARUSHA: WAANDISHI wa habari wameaswa kuandika habari zinazohamasisha amani na kuzingatia usalama wao wanapoandika masuala ya migogoro.
Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Taasisi ya Waandishi wa Habari ya Kusaidia Jamii za PembezonI (MAIPAC), Mussa Juma, wakati wa mafunzo kwa wanahabari kuhusu uandishi unaochochea amani na namna ya kujilinda wanapotekeleza majukumu yao
Juma ameonya kuwa uandishi wa upande mmoja usiozingatia maadili na maslahi mapana ya umma unaweza kuchochea migogoro katika jamii.
Habari Picha 11206
Amesisitiza umuhimu wa kufanya uchambuzi wa kina wa habari kabla na baada ya kuchapishwa au kurushwa hewani.
“Tujiulize habari ina madhara au faida gani kwa jamii. Tusiwe na upendeleo, na tuzingatie tahadhari za kiusalama, ikiwemo usalama wa kidijitali na binafsi,” amesema.
Habari Picha 11208
Kwa upande wake, Wakili wa kujitegemea John Sendodo amewataka wanahabari kuzingatia sheria za vyombo vya habari hata kama zina upungufu.
Ametaja baadhi ya sheria hizo kuwa ni Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016, Sheria ya Makosa ya Mtandaoni ya mwaka 2015 na Kanuni za Maudhui ya Mtandaoni.
Sendodo, ambaye pia anashirikiana na shirika la kimataifa la Protection Africa, amefafanua vifungu mbalimbali vya sheria hizo pamoja na mikataba ya kimataifa inayohusu taaluma ya habari, akisisitiza wanahabari kutekeleza wajibu wao bila kuvunja sheria.
Habari Picha 11209
Mmiliki wa Chuo cha Uandishi wa Habari cha Fanikiwa kilichopo Arusha, Joseph Mayagilla, amesisitiza umuhimu wa kuzingatia maadili ya taaluma hiyo.
Amesema uandishi usiozingatia misingi ya kitaaluma umeleta madhara katika jamii.
Mayagilla amependekeza kurejeshwa kwa madawati maalumu katika vyombo vya habari, ikiwemo ya uchunguzi, amani na maendeleo pamoja na uchumi, ili yaongozwe na waandishi wabobezi na kuboresha ubora wa habari.
Naye mtaalamu wa saikolojia, Ester Cornelio, amewataka wanahabari wanaokabiliwa na msongo wa mawazo kutafuta ushauri wa kitaalamu badala ya kujifungia au kutumia pombe na sigara kupunguza maumivu ya kihisia.
Amesema wanaume wengi wamekuwa wahanga wa sonona kwa kushindwa kueleza hisia zao, tofauti na wanawake ambao mara nyingi huzungumza na kupata nafuu.
Habari Picha 11211
Wakichangia mada, Meneja wa Dawati la Kidigitali wa Star TV, Tausi Mbowe, na Anthony Mayunga wa Serengeti Media wamesisitiza umuhimu wa maadili ya uandishi, uelewa wa sheria na namna ya kukabiliana na msongo wa mawazo.
Mbowe amependekeza kuwepo kwa mafunzo endelevu kwa wanahabari, hususan kuhusu sheria na usalama wa kidijitali.
Wanahabari wengine walioshiriki, akiwemo Elizabeth Nyivambe (Mbeya), Muta Robet (Geita) na Zakaria Mtigandi (Manyara), wamesisitiza umuhimu wa kuendeleza mafunzo, hasa katika matumizi sahihi ya mitandao na masuala ya usalama.
Mafunzo hayo yamehusisha waandishi wa habari kutoka mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Geita, Mara, Manyara, Mbeya na Arusha, na yalidhaminiwa na shirika la wanahabari la Press Unlimited.

You Might Also Like

Tanesco yashauriiwa kuendeleza kasi

Tanzania, Afrika Kusini Zakubaliana Kuharakisha Makubaliano ya Ushirikiano

Dkt. Adesina Wa AfD Avutiwa Na Mwenendo Uchumi Wa Tanzania

TUCTA: Vijana Ni Nguvu Kazi Ya Taifa, Watumie Fursa Kujijenga

Rais Samia afungua kikao kazi cha watendaji serikalini

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Serikali Kuendelea Kutatua Changamoto Sekta Ya Uwekezaji Nchini
Next Article Watu Wenye Ulemavu Nchini Wafikia Mil 5.3
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mavunde: Makaa ya Mawe Ni Injini ya Maendeleo ya Viwanda
Habari March 30, 2026
Programu Mpya ya TPHPA Yalenga Usalama wa Mazao Sokoni
Habari March 30, 2026
CHAKUHAWATA Yaimarisha Ulinzi wa Haki za Walimu, Yafikia Wanachama 49,750
Habari March 29, 2026
Upungufu wa Wataalamu wa Ustawi wa Jamii Wachangia Changamoto Kwenye Huduma za Jamii
Habari March 28, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?