MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Maboresho Mfumo wa Sheria Zinazosimamia Uwekezaji Kuchochea Uwekezaji Nchini
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Maboresho Mfumo wa Sheria Zinazosimamia Uwekezaji Kuchochea Uwekezaji Nchini
Habari

Maboresho Mfumo wa Sheria Zinazosimamia Uwekezaji Kuchochea Uwekezaji Nchini

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Mwandishi Wetu
MFUMO wa  ya sheria za uwekezaji nchini ukiboreshwa  utasaidia  kuweka mazingira mazuri, yenye uhakika yatakayovutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.
Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania, Jaji wa Mahakama ya Rufani Beatrice Korosso amesema hayo
katika kikao cha Kamisheni ya Tume hiyo kilichokaa kujadili rasimu ya taarifa ya sheria zinazosimamia uwekezaji nchini ikiwemo sheria ya Uwekezaj, mkoani Morogoro.
Amesema maboresho hayo yakifanyika yatasaidia kuondoa vikwazo kama urasimu, kodi zisizovutia au taratibu ngumu za kupata vibali vya biashara.
Pia yatasaidia kuongeza ushindani wa nchi katika soko la kimataifa la uwekezaji.
Jaji Korosso amesema maboresho hayo ni muhimu kwa kuwa yataiwezesha nchi kuendana na viwango vya kimataifa vya biashara, uwekezaji na kufanya sheria zake ziwe sambamba na mikataba ya kikanda na kimataifa ili kupata masoko mapya yatakayovutia  uwekezaji wa kigeni.
Vilevile maboresho hayo yatachochea uanzishaji wa viwanda, ukuzaji wa ajira, na kuongeza mapato ya Serikali kupitia kodi na tozo  zitokanazo na uwekezaji hivyo nchi itakuwa imejenga mazingira yenye tija ya kiuchumi ambayo yatachangia ukuaji wa uchumi na kuleta maendeleo endelevu.
“Marekebisho ya sheria yanaweza kusaidia kuhakikisha kuwa wawekezaji wa ndani, hususan wajasiriamali wadogo na wa kati, wanapata fursa sawa za kushiriki katika uchumi.
“Kwa kuweka motisha kwa uwekezaji wa ndani, nchi inaweza kukuza uchumi wa wananchi wake na kupunguza utegemezi wa uwekezaji wa kigeni pekee,” amesema.
Katika hilo amesema tume imepiga hatua kubwa katika kukamilisha taarifa yenye mapendekezo ya maboresho mfumo wa  ya sheria za uwekezaji nchini kutokana na umuhimu wake katika  maendeleo ya kiuchumi, kisiasa, na kijamii.
Naye Katibu Mtendaji wa Tume hiyo, George Mandepo awali alieleza kwamba mapendekezo yaliyotolewa yatasaidia katika kuendana na mabadiliko ya kiuchumi, teknolojia, na utandawazi kama vile teknolojia ya habari (TEHAMA), nishati mbadala, na biashara za mtandaoni zinazohitaji sheria ambazo zinaweza kuruhusu na kuwezesha uwekezaji katika maeneo mapya yanayokua kwa kasi.
Akizungumzia kuhusu uhifadhi wa mazingira na rasilimali asili, Mandepo  ameeleza kwamba maboresho ya sheria za uwekezaji ni muhimu katika kuhakikisha kuwa shughuli za uwekezaji zinaendana na ulinzi wa mazingira na kuweka misingi ya kuhakikisha kwamba miradi ya maendeleo ya kiuchumi haiathiri mazingira au kuharibu rasilimali za asili, kama vile ardhi, maji, na misitu.
Amesema maboresho ya mfumo wa sheria za uwekezaji ni muhimu kwa maendeleo ya kiuchumi, usalama wa kisheria katika wawekezaji na uimarishaji wa mifumo ya kiutawala na kijamii.
Pia amesema maboresho ya mfumo huo  yanatachochea ukuaji wa uchumi, ajira na kuhakikisha uwekezaji endelevu kwa manufaa ya nchi na wananchi wake.

You Might Also Like

Matukio Mbalimbali Katika Picha Baada Ya Waziri Mkuu Kuwasilisha Makadirio Ya Mapato Ya Bajeti

TPHPA yakusanya zaidi ya sampuli 10,000 za mbegu asili

Rais Samia Aridhia Malipo Ya Fidia Barabara Ya Afrika Mashariki

Wiki ya kudhibiti bidhaa bandia kuhitimishwa DSM

VETA Mikumi Yatengeneza Mashine Ya Kuchakata Majani Ya Mifugo

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Tume Ya Kurekebisha Sheria Tanzania Kuipitia Sheria Ya Takwimu
Next Article TARURA Yaunganisha Vijiji Vya Ifinisi, Kambanga na Bugwe Wilayani Tanganyika
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?