MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Katambi Aitaka TIRDO Kuongoza Mapinduzi ya Kufufua Viwanda Nchini
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Katambi Aitaka TIRDO Kuongoza Mapinduzi ya Kufufua Viwanda Nchini
Habari

Katambi Aitaka TIRDO Kuongoza Mapinduzi ya Kufufua Viwanda Nchini

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: NAIBU Waziri wa Viwanda na Biashara, Patrobas Katambi, amelitaka Shirika la Utafiti na Maendeleo ya Viwanda Tanzania (TIRDO) kufanya tathmini ya kina ili kubaini njia bora za kufufua viwanda vilivyokufa na kutoa ushauri wa kitaalamu utakaoviwezesha kurejea katika uzalishaji.
Katambi ametoa agizo hilo wakati wa ziara yake katika shirika hilo, akisisitiza umuhimu wa kuondoa changamoto zinazosababisha viwanda kusimama licha ya kuwepo miundombinu.
Amesema kero kubwa kwa wananchi ni kushuhudia viwanda vilivyopo lakini havifanyi kazi, hali inayokwamisha utoaji wa ajira na kupunguza mchango wake katika ukuaji wa uchumi wa taifa.
Habari Picha 10685
Kwa mujibu wa Katambi, utafiti ni nguzo muhimu ya maendeleo, kwani huwezesha upatikanaji wa taarifa sahihi zinazosaidia kupanga na kutekeleza mikakati ya maendeleo kwa ufanisi.
Katambi ameeleza kuwa matokeo chanya ya tafiti huchochea ukuaji wa viwanda, uwekezaji katika sekta ya uzalishaji na utengenezaji wa bidhaa zenye ubora na ushindani katika masoko ya ndani na nje ya nchi.
Aidha, tafiti husaidia kufahamu mienendo ya kiuchumi katika dunia ya sasa inayoendeshwa kwa kiasi kikubwa na maarifa pamoja na teknolojia.
Habari Picha 10686
Ameongeza kuwa Serikali inalitegemea TIRDO kutoa ushauri unaozingatia misingi ya sayansi na teknolojia ili kukuza viwanda imara vinavyoweza kushindana sokoni.
Ushauri huo unapaswa kuzingatia thamani ya fedha, uwekezaji wa viwanda, miundombinu na kusogeza huduma karibu na wananchi.
Pia amesisitiza kuimarisha teknolojia, ubunifu na uvumbuzi kama vipaumbele vya kukuza ajira na maendeleo ya taifa.
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TIRDO, Mkurugenzi wa Maendeleo ya Uhandisi (DED), Ramsons Mwilangali, amesema shirika linaendelea kusaidia sekta ya viwanda kwa kufanya tafiti za teknolojia stahiki, kusimamia na kusambaza matokeo ya tafiti kwa wadau wa ndani na nje ya nchi.

You Might Also Like

Ridhiwani Ashiriki Mazishi Ya Mwenyekiti SHIVYAWATA

Mradi wa Maadili Katika Utafiti Wa Binadamu Na Huduma Za Afya Wafanywa UDSM kwa Ushirikiano wa Kimataifa

Wataalamu wa Tanzania, Kenya Watoa Ufafanuzi Kuhusu Maana Na Matarajio Ya Jumuiya Ya China, Afrika yenye Mustakabali wa Pamoja

Rais Dkt Samia Awaaapisha Mawaziri, Awaaagiza Kutumia Rasilimali Za Nchi Kupata Fedha

Mwalim: Niko Tayari Kushirikiana na Majaliwa Nikipewa Ridhaa ya Urais

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Tafiti Nguzo Ya Maendeleo Ya Biashara, Uchumi – Katambi
Next Article Katambi Aagiza Ushindani Wa Haki Ili Kulinda Bei, Walaji
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

CAG Aipongeza TARURA Kwa Ujenzi Wa Miundombinu
Habari January 9, 2026
Tuna Deni La Kusimamia Miradi Na Kusikiliza Kero za wananchi Ili Kuleta Maendeleo Ya Kweli-Salome
Habari January 9, 2026
Rais Dkt Samia Azindua Majengo Ya Kisasa
Habari January 8, 2026
TEA, UNICEF Watekeleza Miradi ya Elimu Visawani Zanzibar
Habari January 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?