MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kasulu Yaandaa Bonanza La Michezo Kuhamasisha Uchaguzi Mkuu, Mapokezi Ya Mwenge
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Kasulu Yaandaa Bonanza La Michezo Kuhamasisha Uchaguzi Mkuu, Mapokezi Ya Mwenge
Habari

Kasulu Yaandaa Bonanza La Michezo Kuhamasisha Uchaguzi Mkuu, Mapokezi Ya Mwenge

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
KIGOMA:  MKUU wa Wilaya ya Kasulu, Isaac Mwakisu, amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki katika mapokezi ya Mwenge wa Uhuru pamoja na Uchaguzi Mkuu ujao, kwa kuwa matukio hayo ni ya kitaifa, yanaakisi mshikamano wa Watanzania.
Mwakisu amesema hayo leo Jumamosi Septemba Sita, mwaka 2025, wakati wa bonanza la michezo mbalimbali lililofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Kiganamo.
Habari Picha 9262
Amesema Mwenge wa Uhuru unatarajiwa kukimbizwa wilayani humo kwa siku mbili, Septemba 17 hadi 18, 2025.
Amesema mwenge huo utapokelewa  katika eneo la Mvugwe, Kasulu Vijijini, kabla ya kuingia Kasulu Mjini siku inayofuata.
“Maudhui makuu ya bonanza hili ni kuwakumbusha wananchi kuwa Mwenge utakimbizwa katika wilaya yetu.
Habari Picha 9263
“Ni muhimu tushiriki kwa wingi ili kuonesha mshikamano wetu na kuthamini amani na utulivu wa nchi yetu,” amesema Mwakisu.
Pia amesema Mwenge  ni alama adhimu ya taifa, na mapokezi yake ni kielelezo cha uzalendo na dhamira ya kudumisha amani, umoja na maendeleo ya taifa.
Habari Picha 9264
Amewakumbusha  wananchi kwa mujibu wa ratiba ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), Uchaguzi Mkuu utafanyika Oktoba 29, 2025.
Amesisitiza umuhimu wa wananchi kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi hilo muhimu kwa kusikiliza sera za wagombea na kuwachagua viongozi wanaowakilisha matarajio yao.
Habari Picha 9265
Katika mahojiano na Mwandishi wa Habari hii,  mmoja wa wananchi Nelstella Kihoza, amesema umati mkubwa ulioshiriki bonanza hilo ni ishara ya mwamko wa kisiasa na uzalendo miongoni mwa wananchi wa Kasulu.
Amesema ni imani pia wananchi watajitokeza kwa wingi kushiriki Uchaguzi Mkuu na Mbio za Mwenge wa Uhuru.
Habari Picha 9266
Naye Mwalimu Yusufu Hamisi amempongeza Mkuu wa Wilaya kwa ubunifu wa kuandaa bonanza hilo, akisema limewapa ari mpya ya kuendelea kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu matukio hayo muhimu ya kitaifa.

You Might Also Like

Tanzania, Uturuki Zaweka Dira Mpya ya Biashara ya Dola Bil. Moja

Wagonjwa wa Magonjwa Yasiyoambukiza waongezeka Temeke

Usajili Kwa Njia Ya Mtandao, Umeharakisha Ufunguaji Mashauri

Mjadala wa Kidiplomasia Ya Kisayansi Wafanyika Marekani

Mwenda: Tupo kwa ajili ya kuzitatua changamoto za wananchi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Biashara Kati Ya Tanzania Na Uturuki Yapanuka Kwa Kiasi  Kikubwa
Next Article Profesa Kitila Ataja Sababu Za Watanzania  Kumchagua Dkt Samia
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

CAG Aipongeza TARURA Kwa Ujenzi Wa Miundombinu
Habari January 9, 2026
Tuna Deni La Kusimamia Miradi Na Kusikiliza Kero za wananchi Ili Kuleta Maendeleo Ya Kweli-Salome
Habari January 9, 2026
Rais Dkt Samia Azindua Majengo Ya Kisasa
Habari January 8, 2026
TEA, UNICEF Watekeleza Miradi ya Elimu Visawani Zanzibar
Habari January 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?