MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kapinga Afichua Fursa Kubwa za Ajira na Biashara kwa Vijana Nchini Tanzania
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Kapinga Afichua Fursa Kubwa za Ajira na Biashara kwa Vijana Nchini Tanzania
Habari

Kapinga Afichua Fursa Kubwa za Ajira na Biashara kwa Vijana Nchini Tanzania

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read

Na Lucy Ngowi

WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga, amesema uwekezaji katika sekta ya viwanda na biashara unazalisha fursa kubwa za ajira, hasa kwa vijana.

Aidha amesema Serikali inathamini ujasiriamali wa wazawa na inahakikisha wanapata nafasi za kuendeleza biashara zao, jambo linalochangia kukuza vipaji vya vijana na kuimarisha uchumi wa ndani.

Waziri Kapinga alieleza hayo Dar es Salaam, alipozungumza na waandishi wa habari katika Mkutano ulioandaliwa na Idara ya Habari – Maelezo.

Habari Picha 10589

Kapinga alieleza fursa zilizopo katika kilimo biashara, viwanda vya kuongeza thamani ya rasilimali, biashara ya kikanda kupitia Eneo Huru la Biashara la Bara la Afrika (AfCFTA), viwanda vinavyoanzishwa katika kongani, teknolojia na utafiti, biashara mtandaoni, na usambazaji katika minyororo ya thamani.

“Sekta ya viwanda haiwezi kujengwa bila vijana. Serikali imejenga miundombinu, kufungua masoko, kurahisisha mikopo na usajili wa biashara. Sasa ni jukumu la vijana kuchukua hatua,” alisema.

Akizungumzia Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050, Waziri Kapinga alibainisha viwanda imara, biashara yenye ushindani na sekta binafsi yenye nguvu kama nguzo za uchumi shirikishi.

Habari Picha 10590

Aidha, maboresho ya sera na sheria yameboresha mazingira ya biashara, kuongeza mauzo ya nje ya bidhaa na huduma, na kukuza uzalishaji wa ndani wa bidhaa kama saruji, mabati, flat glass na tiles, huku nchi ikipata ziada ya bidhaa kwa ajili ya kuuza nje.

Vilevile alizungumzia usajili na utoaji wa leseni kwa njia ya mtandao umeboresha urahisi wa biashara, na kuunganisha mifumo ya taasisi 29 za Serikali na binafsi.

Alisema Maboresho hayo yameongeza idadi ya kampuni na biashara zilizosajiliwa, leseni za biashara na viwanda, na kuongeza kasi ya urasimishaji wa biashara.

Waziri Kapinga pia alieleza miradi mikubwa inayozalisha ajira kwa vijana, ikiwemo Mradi wa Mchuchuma na Liganga, Magadi Soda Engaruka, Mradi wa Chuma Maganga Matitu na Mradi wa Makaa ya Mawe Katewaka,

Pamoja na uwekezaji wa kongani za viwanda kama Kwala na Modern Industrial Park. Miradi hiyo nazalisha ajira za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja kwa vijana wenye ujuzi wa ufundi, uhandisi, biashara na usambazaji.

Aidha, teknolojia na ubunifu vinatumika kuendeleza viwanda vidogo, kutoa mashine na teknolojia za kuchakata mazao, uzalishaji wa mkaa mbadala, biogas na bidhaa za mifugo.

Waziri huyo alisema, Serikali pia inatoa mikopo nafuu kupitia mfuko wa NEDF, TADB na Mfuko wa Dhamana, ili kuwasaidia vijana kuanzisha viwanda vidogo, biashara za uzalishaji na ubunifu wa teknolojia.

Waziri alisisitiza: “Biashara mtandao na masoko ya kidijitali ni fursa kubwa kwa vijana. Serikali itaendelea kuweka miundombinu, mafunzo na rasilimali ili waweze kufanikisha ndoto zao, kuhakikisha malipo salama, masoko makubwa na msaada wa kitaaluma.”

You Might Also Like

MOI Yaeleza Sababu Viungo Bandia Kuuzwa Kwa Bei Kubwa

Katambi Awataka CBE Kutoa Elimu Yenye Ushindani Kimataifa

Zitumieni fursa za misitu na nyuki-Tafori

Huduma ya Mahakama ya Mwanzo yasogezwa Wilaya ya Ubungo

Mchengerwa Apongeza Shule Ya Sekondari Kibaha Kwa Ufaulu Wa Hali Ya Juu

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mchengerwa Aongoza Ujumbe Wa Tanzania Kwenye Uzinduzi Wa Mkutano Wa Dunia Wa Tiba Asili
Next Article Serikali Yasisitiza Utoaji Huduma Bora Utekelezaji Bima Ya Afya
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

CAG Aipongeza TARURA Kwa Ujenzi Wa Miundombinu
Habari January 9, 2026
Tuna Deni La Kusimamia Miradi Na Kusikiliza Kero za wananchi Ili Kuleta Maendeleo Ya Kweli-Salome
Habari January 9, 2026
Rais Dkt Samia Azindua Majengo Ya Kisasa
Habari January 8, 2026
TEA, UNICEF Watekeleza Miradi ya Elimu Visawani Zanzibar
Habari January 8, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?