MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kafulila: Ushirikiano wa Sekta Binafsi na Umma Kuboresha Huduma
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Kafulila: Ushirikiano wa Sekta Binafsi na Umma Kuboresha Huduma
Habari

Kafulila: Ushirikiano wa Sekta Binafsi na Umma Kuboresha Huduma

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPPC), David Kafulila  amesema  mfumo wa ubia kati ya sekta binafsi na sekta ya umma (PPP) ni suluhisho la kisasa linalolenga kuongeza ufanisi, ubunifu na kupunguza gharama za utoaji huduma kwa wananchi kupitia miradi ya kimkakati ya maendeleo.
Hayo yamebainika wakati wa maonesho ya 49 ya Kibiashara yanayomalizika leo mkoani Dar es Salaam, katika banda la PPPC lililopo kwenye maonesho hayo.
Kafulila amesema mfumo huo wa PPP unaruhusu mwekezaji binafsi kushirikiana na taasisi za serikali iwe wizara, idara, serikali za mitaa au mashirika ya umma kwa mkataba wa muda mrefu.
Amesema kupitia mkataba huo, mwekezaji binafsi anajenga miundombinu mipya au kuboresha iliyopo kwa gharama zake, huku akiendesha huduma kwa niaba ya serikali kwa kipindi kilichokubaliwa kabla miundombinu hiyo haijarejeshwa serikalini.
“Lengo la PPP ni kutumia nguvu ya sekta binafsi iwe kifedha, kitaalamu, kiteknolojia au ubunifu kuboresha utoaji huduma kwa umma kwa njia nafuu na endelevu,” amesema.
Amesema mikataba ya PPP hupitia mzunguko wa maisha wa mradi ulioainishwa kisheria, kuanzia kuibua wazo, kufanya upembuzi yakinifu, kupata mbia, kujenga, kuendesha hadi kurejesha serikalini.
Aidha, ameeleza kuwa mkataba bora wa PPP hupimwa kwa vigezo vitatu muhimu vya Sekta binafsi kubeba mianya na hatari  kubwa za kifedha na kiutendaji,
Pia gharama nafuu kwa serikali na wananchi, na Manufaa kwa umma kama vile huduma bora, fursa za ajira, na ukuaji wa pato la taifa.
Vile vile amesema katika kuhakikisha uwazi na ushindani wa haki, Sheria ya PPP imeweka njia tatu za kumpata mwekezaji ambazo ni kwa kwa njia ya ushindani wa zabuni,
Pia bila ushindani endapo mradi umetoka kwa sekta binafsi na umekidhi vigezo maalum,
Na kwa utaratibu maalum unaopitia maoni ya Mwanasheria Mkuu na kuidhinishwa na Baraza la Mawaziri.
Kwa mujibu wa Kafulila, mfumo huo ni jukwaa madhubuti la kuvutia uwekezaji, kupunguza mzigo wa bajeti kwa serikali na kuharakisha utekelezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati kwa manufaa ya Watanzania wote.

You Might Also Like

Serikali Yazidi Kuhamasisha Nishati Safi, Yatoa Mitungi 225 Kwa Watumishi Gereza kuu Maweni

Wananchi Wahimizwe Ulipaji Kodi Kimtandao – Nyongo

Tumeridhika na kazi za TTCL – Mwanaisha

Wafanyabiashara 45 Wa Tanzania Wameanza Kutumia Soko La Eneo Huru La Afrika

NHIF: Ruksa wanachama kutumia NIDA

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Teknolojia Mpya Ya Uchomeleaji Yaleta Mapinduzi VETA Dodoma
Next Article NFRA Yawaalika Wadau Kununua Nafaka kwa Masoko ya Ndani na Nje
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Nyanya Cheri na Ngogwe Chungu Zarejea 
Habari July 13, 2025
NFRA Yawaalika Wadau Kununua Nafaka kwa Masoko ya Ndani na Nje
Habari July 13, 2025
Teknolojia Mpya Ya Uchomeleaji Yaleta Mapinduzi VETA Dodoma
Habari July 12, 2025
Tume Yapongeza OCPD kwa Mabadiliko ya Sheria
Habari July 12, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?