MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Kadogosa: Serikali Yatenda Haki Kwa Wakulima, Wafugaji, Wananchi Wa Vijijini
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Kadogosa: Serikali Yatenda Haki Kwa Wakulima, Wafugaji, Wananchi Wa Vijijini
Habari

Kadogosa: Serikali Yatenda Haki Kwa Wakulima, Wafugaji, Wananchi Wa Vijijini

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: MBUNGE wa Bariadi Vijijini, Masanja Kadogosa, ameipongeza Serikali ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali inayowanufaisha wakulima, wafugaji na wananchi wa vijijini.
Akizungumza bungeni jijini Dodoma, Kadogosa amesema sekta ya kilimo imepiga hatua kubwa kupitia ruzuku za mbolea na pembejeo, pamoja na programu mbalimbali za kuwawezesha wakulima kuongeza uzalishaji.
“Ruzuku hizi zimeleta unafuu mkubwa kwa wakulima wetu. Kwa upande wa wafugaji, serikali imeendelea kutoa chanjo za mifugo na kujenga majosho katika maeneo mbalimbali. Katika ilani mpya ya CCM, tumewekewa mpango wa kuongeza maeneo ya malisho kutoka ekari milioni tatu hadi milioni sita ,” amesema Kadogosa.
Mbunge huyo ameongeza kuwa, licha ya mafanikio hayo, bado suala la maji vijijini limepewa kipaumbele maalum.
“Kwa sasa, upatikanaji wa maji vijijini ni asilimia 80.9, lakini bado mahitaji yetu ni makubwa. Tuna mradi mkubwa wa Shilingi Bilioni 440 unaotekelezwa sasa, ambao utapita Busega, Bariadi Mjini, Bariadi Vijijini, Kitilima na Meatu. Mradi huo ukikamilika, tutaondokana kabisa na changamoto ya maji,” amesema.
Kadogosa pia alitumia nafasi hiyo kumpongeza Spika mpya wa Bunge, Mussa Zungu, akisema ana imani ataendesha Bunge lenye ushirikiano na Serikali kwa kuzingatia misingi ya kikatiba.
“Tunatarajia kuwa na bunge lenye mijadala yenye tija kwa wananchi. Spika Zungu ana uzoefu mkubwa, na naamini ataongoza Bunge letu kwa hekima, kuhakikisha bajeti na sheria zinazopitishwa zinaakisi mahitaji halisi ya Watanzania,” amesema.
Kadogosa amesema kuwa mafanikio haya yanaonyesha utekelezaji thabiti wa ilani ya CCM na dhamira ya Serikali ya kuhakikisha wananchi wa vijijini wanapata huduma bora na maendeleo endelevu.

You Might Also Like

Kilimo Yaomba Trilioni 1.24 Mwaka Wa Fedha 2025/26

THBUB Mdau Mkubwa Utekelezaji Wa Majukumu 

Wakazi Wa Ntyuka Wataka Kiongozi Mchapakazi

Dendego Achangisha Bilioni 1.7, Ujenzi Ofisi Ya CCM

Sekta Ya Madini Yapaisha Pato La Taifa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Spika Mussa Zungu Atoa Hotuba Baada Ya Kuchaguliwa
Next Article Mbunge Ndoinyo Kubadilisha Taswira ya Ngorongoro Na Kuimarisha Utalii, Ufugaji
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari November 22, 2025
Kwagila Awataka Wasimamizi Wa Elimu TAMISEMI Kuwajibika Kikamilifu
Habari November 21, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?