MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Huduma za Maktaba Zabadilika: Malipo Kidijitali, Usomaji Mtandaoni
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Huduma za Maktaba Zabadilika: Malipo Kidijitali, Usomaji Mtandaoni
Habari

Huduma za Maktaba Zabadilika: Malipo Kidijitali, Usomaji Mtandaoni

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: MKUTUBI wa Maktaba Kuu ya Dar es Salaam, Saida Kalokola, amesema kuwa huduma za maktaba zimeboreshwa kwa kiwango kikubwa, na sasa watumiaji wanaweza kusoma vitabu popote walipo kupitia mfumo wa maktaba mtandaoni, mradi tu wawe wamelipia ada husika.

Akizungumza katika Maonesho ya 32 ya Kitaifa ya Vitabu Tanzania yanayoendelea jijini Dar es Salaam, Kalokola amesema kuwa awali watumiaji walilazimika kufika maktaba ili kupata taarifa za vitabu, ambapo walipewa kadi maalumu iliyoonyesha mahali kitabu kilipohifadhiwa.

Amesema kwa sasa mchakato umerahisishwa. Ada ya mwaka kwa matumizi ya maktaba mtandaoni ni Sh 10,000, huku ada ya siku ikiwa Sh 1,000. Baada ya kufanya malipo, mtumiaji hutaja kitabu anachokihitaji na anakipata moja kwa moja mtandaoni.

Amesema maktaba inatoa vitabu vya aina mbalimbali, ikiwemo vya masomo, hadithi, pamoja na vitabu vya ziada kwa watoto na watu wazima.

Aidha, amewahimiza wananchi kujiunga na huduma za maktaba, akibainisha kuwa kuna maktaba maalumu kwa watoto kuanzia umri wa miaka miwili na nusu, ambayo ada yake ni Sh 5,000 kwa mwaka, huku wanafunzi wa sekondari wakitozwa Sh 7,000 kwa mwaka.

Pia, ameeleza kuwa kuna huduma za maktaba kwa watu wasioona, zinazotolewa bure, zikiwemo nakala za vitabu vya nukta nundu pamoja na vitabu vya maandishi ya kawaida.

You Might Also Like

VETA Kujenga Mahusiano Na Wenye Ujuzi, Wabunifu

Mazao Ya Mikunde Yatajwa Kuwa Na Kiwango Kikubwa Cha Protini

PSSSF Itaendelea Kuwekeza Kwenye Maeneo Salama Yenye Tija

UDSM Yaanzisha Mkakati Kuokoa Nyuki Wadogo

Sirro: Kasulu Itambue Thamani ya Uwekezaji, Itenge Maeneo Rasmi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Next Article Viongozi Watakiwa Kuweka Haki Mbele Katika Kusimamia Masuala ya Wafanyakazi — COWTU (T)
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Viongozi Watakiwa Kuweka Haki Mbele Katika Kusimamia Masuala ya Wafanyakazi — COWTU (T)
Habari November 25, 2025
Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari November 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?