MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Fursa za Uwekezaji Kanda ya Ziwa: Buzwagi na Maeneo Mengine ya Kimkakati
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Fursa za Uwekezaji Kanda ya Ziwa: Buzwagi na Maeneo Mengine ya Kimkakati
Habari

Fursa za Uwekezaji Kanda ya Ziwa: Buzwagi na Maeneo Mengine ya Kimkakati

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
GEITA: MAMLAKA ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA), imezieleza fursa mpya za uwekezaji kwenye sekta ya madini na nyinginezo katika maeneo maalum ya kanda hiyo.
Ofisa Uwekezaji Mkuu Kanda ya Ziwa, kutoka TISEZA, Erastus Malai ameelezea fursa hizo katika maonesho ya nane ya sekta ya madini yanayoendelea mkoani Geita, na kuongeza kuwa serikali imejipanga kutoa vivutio vya kipekee kwa wawekezaji.
Habari Picha 9585
Akizungumza na waandishi wa habari, Malai amebainisha kuwa eneo la Buzwagi, lilio Geita, limepangwa kutumika kwa shughuli za uchenjuaji madini.
“Eneo hili lenye ukubwa wa ekari 1333 limeandaliwa kwa miundombinu ya kisasa, ikiwa ni pamoja na majengo, barabara, ofisi, na uwanja wa ndege.
“Mwekezaji anayekuja katika eneo hili hatahitaji kugharamia miundombinu, bali atalenga moja kwa moja kuanzisha kiwanda cha kuchanjua madini,” amesema Malai.
Habari Picha 9586
Pia amesema Serikali pia imeandaa maeneo mengine ikiwemo Nala (Dodoma), ekari 607, Kwara (Kibaha, Pwani) ekari 100, na Bagamoyo ekari 151.
Amesema maeneo mengine yaliyoandaliwa kwa ajili ya uwekezaji ni katika sekta za kilimo, uvuvi, utalii, ujenzi wa majengo ya biashara, ufugaji, na utengenezaji wa viwanda.
“Tumeweka mikakati ya kuhamasisha uwekezaji katika viwanda vya kutengeneza dawa, vifaa tiba, uundaji wa magari na boti, bidhaa za ngozi, nguo, na vifaa vya majumbani.
“Buzwagi, ambalo ni moja ya maeneo maarufu kwa shughuli za uchimbaji madini, linatoa fursa ya pekee kwa wawekezaji kutokana na maandalizi ya miundombinu iliyokamilika.
Habari Picha 9587
“Hii ni sehemu ambapo wawekeza katika sekta ya madini wanaweza kuanzisha viwanda vya kuchambua na kuchuja madini bila kujali gharama za ujenzi wa miundombinu, kwani tayari zipo,” amesema.
Ameongeza kuwa Serikali pia itatoa vivutio vya kodi kwa wawekezaji watakaoamua kuwekeza katika eneo hilo,  pamoja na visivyo vya kodi ili kufanikisha maendeleo endelevu.
Malai ameelezea fursa nyingine katika Kanda ya Ziwa  kwamba fursa inatolewa kwa wafanyabiashara na wawekezaji.
“Sekta ya kilimo, kwa mfano, ina nafasi nyingi za uwekezaji hasa katika mazao ya biashara kama pamba, chai, na kahawa. Uvuvi na utalii pia vinatoa fursa kubwa kutokana na utajiri wa maziwa makubwa na maeneo ya kihistoria.
“Wawekezaji na wafanyabiashara wanahamasishwa kuja kuwekeza kwenye maeneo yetu ya kanda ya ziwa kwa sababu kuna miundombinu inayohitajika kwa shughuli zao,” amesema Malai.
Amesema “Kwa niaba ya serikali, tunatoa wito kwa wawekezaji wote, ndani na nje ya nchi, kuja kuwekeza kwenye maeneo haya muhimu.
“Tutatoa msaada na vivutio vya kodi ili kuhakikisha kwamba uwekezaji unakuwa endelevu na faida kwa pande zote.” Amesema.
Kwa kumalizia, Malai amewahimiza wawekezaji kuja kushiriki katika fursa hiyo mpya, akisisitiza kwamba wakati ni sasa, kwani serikali imejipanga kuhakikisha kuwa mazingira ya uwekezaji ni ya kirafiki na yenye tija kwa pande zote.

You Might Also Like

Wazalishaji, Waagizaji Mbolea Watakiwa Kuzingatia Afya ya Udongo kwa Tija ya Kilimo

Walimu Kupatiwa Mafunzo ya Tehama

CHAUMMA: Tupo Tayari Kupunguza Gharama za Maisha – Salum Mwalim

Chalamila afanya ukaguzi mwenendo wa utoaji huduma Kivuko cha Feri

Kingoba : Sheria Inawataja Waliotoa Mchango Sekta Ya Habari Ambao Sio Waandishi Wa Habari

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Takribani watu 200 Wamepata Ushauri Wa Kibingwa Wa Ubongo, Mifupa 
Next Article Kingalame Asisitiza Umuhimu wa Wachimbaji Kuuza Dhahabu Serikalini
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

ARTICLE 19,  JOWUTA KUSHIRIKIANA KUIMARISHA HAKI ZA WANAHABARI
Habari October 18, 2025
Profesa Ndunguru Aongoza Kikao Cha Mawaziri Wa DLCO- EA Akimwakilisha Bashe
Habari October 17, 2025
Mgombea NCCR-Mageuzi Awaasa Watanzania Wasikubali Propaganda
Habari October 17, 2025
Profesa Nombo: Ushirikiano wa VETA, Sekta Binafsi Waimarisha Mafunzo ya Ufundi Stadi
Habari October 17, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?