MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Endeleeni Kuunganisha Mifumo Ya TEHAMA Ya Kisekta – Kakoso
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Endeleeni Kuunganisha Mifumo Ya TEHAMA Ya Kisekta – Kakoso
Habari

Endeleeni Kuunganisha Mifumo Ya TEHAMA Ya Kisekta – Kakoso

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Mwandishi Wetu
DAR ES SALAAM: KAMATI ya Bunge ya Miundombinu imeipongeza Serikali kwa kuanzisha Maabara ya Uidhinishaji wa Vifaa vya Mawasiliano ya Kielektroniki ikiwa ni maabara ya kwanza katika Ukanda wa Afrika Mashariki.
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Selemani  Kakoso ametoa pongezi hizo wakati Kamati hiyo ilipotembelea Mradi wa Maabara ya Uidhinishaji wa Vifaa vya Mawasiliano ya Kielektroniki unaotekelezwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).
Kakoso ameitaka Serikali kuendelea kuunganisha mifumo ya TEHAMA ya kisekta ili vifaa vya mawasiliano vinavyoingia nchini viwe na viwango vinavyotakiwa kitaifa, kikanda na kimataifa akitolea mfano wa mifumo ya TCRA na TBS kusomana.
Pia TCRA imeshauriwa kutoa elimu kwa umma kuhusu uwepo na umuhimu wa maabara hiyo ili kumwezesha mwananchi kufahamu ubora wa kifaa cha mawasiliano kabla ya kukinunua.
Pamoja na hilo Kamati imesisitiza kwa mamlaka hiyo  kuendelea kufanya ukaguzi wa kushtukiza mara kwa mara kwa kushirikiana na taasisi mbalimbali za serikali.
Akitoa taarifa ya maabara hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA, Dkt. Jabir Bakari amesema ujenzi wake ulianza Aprili 2023 na kukamilika Machi, 2024 ikiwa ni mwaka mmoja tu kama ulivyopangwa na inafanya kazi katika maeneo mawili ambayo ni eneo la kupima mawimbi ya redio na eneo ya kupima viwango vya mionzi.
Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari,  Maryprisca Mahundi  ameishukuru Kamati na kuihakikishia kuwa Wizara imepokea ushauri wote uliotolewa na Kamati kwa ajili ya kuboresha.
Uwepo wa Maabara hiyo nchini kunaifanya Tanzania kuwa nchi ya 12 Barani Afrika,  Nchi nyingine ni Tunisia, Afrika Kusini, Ghana, Nigeria, Cameroon, Benini, Togo, Senegal, Mali na Mauritania.

You Might Also Like

Vyombo vya Habari ni Kama Maji’ -Biteko 

Kasi Ya Kusambaza Umeme Kwenye Vitongoji Yaanza-Kapinga

Miradi iliyokamilika ianze kutoa huduma- Nyamoga

Uteuzi: Abubakar Mombo Ateuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Usalama wa Taifa, Siwa amestaafu

Wakulima wafunzwa kuhusu mlipuko wa panya TPHPA

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mkurugenzi VETA Kasore Akiteta Jambo Na Mhitimu Fani Ya Ushonaji
Next Article NSSF Kutoa Mafao Siku Moja Baada ya Kustaafu
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Ofisa wa TARI Kuwapo Kila Kituo cha Umwagiliaji – Naibu Katibu Mkuu
Habari August 6, 2025
Mbinu Mpya za Kilimo kwa Vijana Zapata Umaarufu Nanenane Banda La VETA
Habari August 6, 2025
VETA Yatahadharisha Changamoto ya Kuzidisha Uchanganyaji wa Chakula Cha Mifugo
Habari August 6, 2025
UDSM Yaanzisha Mkakati Kuokoa Nyuki Wadogo
Habari August 6, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?