MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: eGA Yatengeneza  Mifumo  Kurahisisha  Kazi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > eGA Yatengeneza  Mifumo  Kurahisisha  Kazi
Habari

eGA Yatengeneza  Mifumo  Kurahisisha  Kazi

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Lyatuu
MAMLAKA  ya Serikali Mtandao (eGA) imesema imetengeneza mifumo mbalimbali ya  Teknolojia Ya Habari Na Mawasiliano (TEHAMA) inayosaidia kurahisisha kazi za kila siku serikalini.
Aidha imewawezesha wananchi kupata huduma kwa njia ya kidigitali na kwa urahisi zaidi
Meneja Mawasiliano wa eGA, Subira Kaswaga, amesema hayo  katika maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa maarufu kama Sabasaba yanayoendelea katika viwanja vya Mwalimu Nyerere,  Dar es Salaam.
Amesema  mamlaka hiyo imepewa jukumu la kisheria kusimamia matumizi ya TEHAMA ndani ya Serikali ili kurahisisha utendaji kazi pamoja na huduma kwa wananchi.
“eGA meendelea kuonesha namna ambavyo Serikali inavyotekeleza mageuzi ya kidigitali kwa lengo la kuboresha utoaji huduma kwa wananchi kupitia matumizi ya TEHAMA,” amesema
Amesema miongoni mwa mifumo hiyo ni mfumo wa e-Mrejesho, ambao ni jukwaa la kidigitali linalowawezesha wananchi kuwasiliana moja kwa moja na Serikali kwa njia ya kupeleka maoni, pongezi au malalamiko, huku Serikali nayo ikijibu na kutoa mrejesho wa hatua zilizochukuliwa.
Amesema mfumo huo unapatikana kwa njia tatu, ikiwemo kupitia simu ya mkononi, na unampa uhuru mwananchi kuficha taarifa zake za msingi iwapo hataki kujulikana, huku pia akipatiwa namba ya ufuatiliaji wa taarifa aliyoitoa.
“Kwa mfumo huu, taasisi za umma zinaweza kuona ni malalamiko ya aina gani zinayapokea mara kwa mara, hivyo kumsaidia kiongozi wa taasisi kutambua idara au kitengo kinachosababisha changamoto kwa wananchi, na kuchukua hatua stahiki,” amesema.
Mbali na hilo, mfumo huu pia unasaidia kupima uwajibikaji wa watendaji wa umma kwa kuruhusu ufuatiliaji wa hatua zinazochukuliwa baada ya malalamiko kuwasilishwa. Viongozi wakuu wa Serikali kama Katibu Mkuu Utumishi na Katibu Mkuu Kiongozi wanaweza kuona kwa uwazi taarifa za malalamiko katika taasisi zote za umma.
Kutokana na mafanikio hayo, Subira amesema kuwa mfumo wa e-Mrejesho umeendelea kuipa sifa Tanzania kimataifa, ambapo Julai 7, 2025, eGA ilishinda tuzo ya kimataifa iliyotolewa na Shirika la ITU katika kipengele cha Serikali Mtandao.
“Ni fahari kubwa kwamba mfumo huu umetengenezwa na Watanzania, na leo unatutambulisha kimataifa. Tunawahamasisha wananchi wauitumie mfumo huu ili Serikali iwafikie kwa urahisi na kwa ufanisi,” amesema.
Amesisitiza kuwa ni wajibu wa watumishi wa umma kuhakikisha kuwa maoni na malalamiko yanayowasilishwa kupitia mfumo huo yanashughulikiwa ipasavyo ili kukuza uwajibikaji na kuongeza imani ya wananchi kwa Serikali.

You Might Also Like

Ridhiwani Apongeza Kurudi Kwa Gazeti La Mfanyakazi TANZANIA

Makalla aitaka Halmashauri Longido kutenga fedha, ujenzi wa uzio Samia Girls

TEA Yawaalika Wananchi Kujifunza SDF Unavyofanya Kazi

Rais Mwinyi Kuzindua Maabara Nguvu Za Atomi

TIB Yaanda Mkakati Kabambe Wanawake Kuchangamkia Fursa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article
Next Article TSB Yasisitiza Umuhimu Kuwekeza Kwenye Uchakataji Wa Mkonge
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Tanzania, Comoro Zaongeza Ushirikiano wa Lugha
Habari July 10, 2025
TSB Yasisitiza Umuhimu Kuwekeza Kwenye Uchakataji Wa Mkonge
Habari July 10, 2025
July 10, 2025
Habari July 10, 2025
Wanafunzi, Watafiti, Wanataaluma Kujadili Dini, Utamaduni na Maisha ya Kisasa
Habari July 10, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?