MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: EAC Iweke Ushindani Kuongeza Thamani Ya Malighafi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > EAC Iweke Ushindani Kuongeza Thamani Ya Malighafi
Habari

EAC Iweke Ushindani Kuongeza Thamani Ya Malighafi

Author
By Author
Share
5 Min Read
Na Lucy Lyatuu
SERIKALI imeitaka Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kuweka nafasi yake ya ushindani katika kuongeza thamani ya malighafi kwa kuzingatia maendeleo ya dunia.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mahmoud Thabit Kombo, ametoa wito huo Dares  Salaam wakati wa Mkutano wa Wakurugenzi Wakuu wa Baraza La Biashara La Afrika Mashariki ( EABC).
Amesisitiza dhamira ya Tanzania ya mtangamano wa kikanda na kuitaka sekta binafsi kuwa makini katika kuishirikisha Wizara ili kufungua fursa za biashara na uwekezaji ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na kwamba EAC ndiyo jumuiya pekee ya kikanda ya kiuchumi yenye Katibu Mkuu anayehusika na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Habari Picha 9440

Amesema Tanzania imeonyesha uimara na ukuaji shirikishi wa uchumi ambapo katika mwaka, 2025 uchumi unatarajiwa kukua kwa asilimia 5.9, kwa mujibu wa Benki ya Maendeleo ya Afrika.

“Ukuaji huu unaonyesha athari za mageuzi ya kuboresha mazingira ya biashara, ukuaji wa viwanda, na ushirikiano wa kina wa kikanda unaoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” amesema.

Katika maelezo yake, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC),  Veronica Nduva, amesema: “EAC sasa ni jumuiya ya kiuchumi iliyounganishwa zaidi barani Afrika katika biashara, ikibakiza asilimia 28 ya mauzo ya nje ndani ya bara na kupata  asilimia 19 ya uagizaji kutoka nchi nyingine za Afrika.

Habari Picha 9441

Amesema uzalishaji wa viwanda vya Tanzania, kwa mfano, vilipanda kutoka asilimia tisa  ya Pato la Taifa kwa mwaka 2010 hadi asilimia 23.2 mwaka 2022 chini ya Mkakati Jumuishi wa Maendeleo ya Viwanda wa mwaka 2025.

Hata hivyo ametoa wito wa kuchukuliwa kwa hatua za makusudi ili kukuza ukuaji wa viwanda hasa katika mnyororo wa thamani wa pamba hadi nguo akibainisha kuwa bidhaa za viwandani huchangia chini ya asilimia 30 ya mauzo ya nje, kwani kikapu cha mauzo ya nje kinatawaliwa na bidhaa ghafi za kilimo, na hivyo kupunguza uundaji wa ajira.

Amesema kwa sasa asilimia 64 ya uagizaji wa EAC unabakia kuwa bidhaa za viwandani, nyingi kutoka Asia na kusisitiza dhamira ya EAC kufanya kazi kama kambi moja katika kuendeleza ajenda hiyo.

Katika Katibu Mkuu wa EAC, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, balozi Stephen  Mbundi amezitaka sekta binafsi kuweka ukanda huo kimkakati ndani ya Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA) na Eneo Huria la Biashara la Utatu (TFTA).

Habari Picha 9442

Mwenyekiti wa EABC, Angelina Ngalula, amempongeza Katibu Mkuu wa EAC kwa kuchukua muda wake kushirikisha sekta binafsi ya Tanzania na kupendekeza kwamba, ili kuimarisha uhusiano wa kibiashara na uwekezaji, ni muhimu kuhakikisha matumizi sawa ya Ushuru wa Pamoja wa Nje wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, kuwianisha kodi za ndani, kuondoa vizuizi vya mara kwa mara visivyo vya Ushuru, Kupunguza Vikwazo vya Ushuru, Kupunguza Ushuru na Kukomboa kikamilifu huduma za Biashara.

 

Mwenyekiti wa Shirikisho la Wenye Viwanda Tanzania (CTI),  Hussein Sufiani amewataka wazalishaji na wafanyabiashara kushiriki kikamilifu katika majadiliano na kuwasilisha masuala yao, ambayo yataunganishwa zaidi na Kikundi Kazi cha Kiufundi cha EAC-EABC ili kutoa taarifa na kupinga mapendekezo ndani ya mchakato wa kufanya maamuzi ya sera ya EAC.

 

Katika salamu za ukaribisho, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa EABC,  Adrian Raphael Njau, amesema , mwaka 2023, jumla ya biashara ya EAC ilifikia dola bilioni 109, lakini biashara ya ndani ya EAC ilifikia dola bilioni 13.8 tu, ikiwa ni asilimia 13 tu ya biashara yote.

Amesema Tanzania inaongoza kwa biashara ya ndani ya EAC kwa dola bilioni 4.9, ikifuatiwa na Kenya dola bilioni 2.85 na Uganda dola bilioni 2.14 na kufafanua kuwa ili eneo hilo lifikie lengo la asilimia 40 la biashara ya ndani ya EAC ifikapo 2030, lazima kukabiliana na Vikwazo Visivyo vya Ushuru.

 

You Might Also Like

Polisi Yaimarisha Usalama Timu za Simba na Yanga Kesho

TUCASA Yatoa Mapendekezo ya Sheria, Sera Kwa Serikali Kutatua Ucheleweshaji Wa Malipo

TARI yapongezwa kwa kuwa na teknolojia bora za kilimo

Wananchi Wahimizwa Kulinda Maeneo Yaliyohifadhiwa  Kisheria- Kamishna  Wakulyamba

Vijana Ni Chachu Ya Maendeleo Endelevu Wakiwezeshwa-Kikwete

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Wastaafu Watakiwa Kutafuta Ushauri  Wa Kitaalam Kwa Matumizi Ya Mafao
Next Article Geita Ina Dhahabu Lakini Haina Maendeleo” – Salum Mwalim
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Waziri Mkuu Majaliwa Akabidhi Tuzo kwa BoT Geita
Habari September 22, 2025
BoT Yarahisisha Uuzaji wa Dhahabu kwa Wachimbaji, Yatoa Punguzo La Mrabaha
Habari September 22, 2025
Waziri Mkuu Apongeza Huduma Kidijitali za NSSF, Maonesho Ya Madini Geita
Habari September 22, 2025
Mkuu Wa Mkoa Shinyanga Asifu Kazi Ya Bodi Bima Ya Amana
Habari September 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?