MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: COSTECH, CRDB Foundation Yazindua Mikopo Nafuu Kwa Wabunifu
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > COSTECH, CRDB Foundation Yazindua Mikopo Nafuu Kwa Wabunifu
Habari

COSTECH, CRDB Foundation Yazindua Mikopo Nafuu Kwa Wabunifu

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: TUME ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), pamoja na CRDB Foundation, imezindua mpango wa mikopo nafuu kwa wabunifu, ukihusisha Sh. Bilioni 4.6, ambapo serikali kupitia tume hiyo imetoa dhamana ya Sh. Bilioni 2.3.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda katika uzinduzi wa hafla hiyo amesema  hatua hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan, kuhakikisha wabunifu hususan vijana, wanawezeshwa kwa vitendo ili kushiriki katika uchumi wa kisasa.
 “Maelekezo ya Mheshimiwa Rais ni wazi kabisa: vijana wetu wabunifu wasaidie kujenga uchumi. COSTECH na CRDB Foundation wametekeleza agizo hilo kwa vitendo,” amesema.
Profesa Mkenda ameipongeza CRDB Foundation kwa kuonyesha mfano wa taasisi inayotambua fursa zilizopo kwa wabunifu wa Kitanzania, na kuitaka sekta binafsi na wadau wengine kuiga mfano huo kwa kuwekeza moja kwa moja katika miradi ya vijana.
“Kama kweli tunataka mapinduzi ya kiuchumi, basi tuwekeze kwenye akili na maarifa ya Watanzania,” amesema.
Naye Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, Dkt. Amos Nungu, amesema mchakato wa utoaji mikopo utaendeshwa kwa uwazi, kidigitali, na kwa kuzingatia usawa.
Amesema zaidi ya wabunifu 400 kutoka mikoa mbalimbali tayari wamepatiwa mafunzo na ushauri,  wako katika hatua ya kuingia kwenye mfumo wa kupata mikopo.
“Hatutaki tena wazo zuri libaki mezani. Tunataka lionekane sokoni, lichangie pato la taifa, na lifungue ajira,”almesema.
Mpango huo pia unajumuisha vipengele vya mafunzo kabla na baada ya mkopo, ili kuhakikisha kuwa wabunifu wanatumia fedha walizopata kwa njia endelevu na zenye matokeo.
Mada kama akili bunifu, usimamizi wa biashara, na matumizi ya teknolojia ni sehemu ya kozi zitakazotolewa.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Foundation, Tully Esther Mwambapa, ameleza kuwa taasisi yao imejipanga kuhakikisha wabunifu wanaoungwa mkono wanapewa siyo tu fedha, bali pia mafunzo, ushauri, na mwongozo wa kitaalamu.
“Tunaamini kuwa ubunifu unaweza kuwa injini ya maendeleo ikiwa tu utapewa mazingira wezeshi ya kifedha na kiufundi,”amesema.

You Might Also Like

VETA Mikumi Yatengeneza Mashine Ya Kuchakata Majani Ya Mifugo

OUT Yawapiga Msasa Watumishi Wa Mamlaka Za Serikali Za Mitaa

Kilimo Yaomba Trilioni 1.24 Mwaka Wa Fedha 2025/26

Masauni: Mapendekezo Ya Kulifanya NEMC Kuwa Mamlaka Yamepokelewa

Wizara Ya Madini Kununua Chopa, Kufanya Utafiti

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Kabudi Aelezea Mafanikio Ya Wizara Yake
Next Article 𝐓𝐅𝐒 Y𝐚𝐧𝐝𝐚𝐚 M𝐤𝐚𝐤𝐚𝐭𝐢 W𝐚 M𝐢𝐚𝐤𝐚 1𝟎 Ku𝐞𝐧𝐝𝐞𝐥𝐞𝐳𝐚 N𝐚 K𝐮𝐡𝐢𝐟𝐚𝐝𝐡𝐢 M𝐢𝐬𝐢𝐭𝐮 Ya Mi𝐤𝐨𝐤𝐨 𝐓𝐚𝐧𝐳𝐚𝐧𝐢𝐚 𝐁𝐚𝐫𝐚
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

NSSF Yaendelea Kutoa Elimu Ya Hifadhi Ya Jamii ‘ Karibu Tukuhudumie’
Habari June 21, 2025
Wananchi Watakiwa Kutowachagua Watoa Rushwa
Habari June 19, 2025
Kihenzile: Mifumo Ijengwe Kuhakikisha Huduma Zinapatikana Kwa Haraka, Salama, Zenye tija
Habari June 19, 2025
MOI Yawasogelea Dodoma, Mikoa Jirani
Habari June 19, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?