MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Changamoto ya uelewa mwiba kwa wasafirishaji Comoro
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Changamoto ya uelewa mwiba kwa wasafirishaji Comoro
Habari

Changamoto ya uelewa mwiba kwa wasafirishaji Comoro

Shani
By Shani
Share
2 Min Read

Na Lucy Ngowi

BALOZI wa Tanzania nchini Comoro, Saidi Yakubu amesema wafanyabiashara wanaosafirisha bidhaa kwa usafiri majini kati ya Comoro na Tanzania wanapatwa na changamoto kubwa kwa sababu ya uelewa mdogo wa kanuni kwa watoa huduma wanaofanya shughuli hizo.

Balozi Yakubu, aliyasema hayo wakati alipokuwa akijadiliana na watumishi wa TASAC pamoja na wana diaspora waliopo katika Kliniki ya Diaspora katika viwanja vya Bunge la Comoro, mjini Moroni.

“Tulikaa na wadau wa TASAC ili kupata mrejesho, kwa kiasi kikubwa changamoto inayowakabili wafanyabiashara wa diaspora ni suala la uelewa wa huduma za meli, nani anapaswa kufanya nini, kwa mujibu wa sheria zinazoendesha usafiri majini,” amesema.

Amesema changamoto nyingine ambayo imebainika ni ukosefu wa uwepo wa vyombo imara na salama vya usafari majini vinavyotumika katika nchi ya Tanzania na Comoro,.

Katika hilo amesema juhudi mahsusi zinafanywa na upande wa Tanzania ili kuwa na vyombo kwa upande wa Tanzania ili kutatua changamoto hiyo.

“Suala lingine ambalo ni la kulifanyia kazi ni kuwa na vyombo imara vya usafiri utakaotumika katika nchi hizi mbili na kwa bahati nzuri tumeshapewa ahadi na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwamba MV. Mapinduzi itakapopona itatumika kwa ajili ya usafiri kati ya Comoro na Tanzania,” amesema.

Hata hivyo, Yakubu amesema uwepo wa TASAC katika Kliniki hiyo umesaidia kutoa elimu kwa wadau wa usafirishaji na wafanyabiashara kwa ujumla kwa kuwa asilimia kubwa ya bidhaa za chakula zinazoingia Comoro zinatokea Tanzania kwa hiyo ni soko zuri na sekta ya usafirishaji ndio kiungo katika kuhakikisha bidhaa hizo zinafika Comoro.

Naye Ofisa Udhibiti Usafirishaji wa TASAC, John Butoto ametoa elimu kwa diaspora na kuwaasa kuhakikisha wanatumia watoa huduma wanaotambulika kisheria jambo ambalo litasaidia kufuatilia pindi wanapopata changamoto za kupotea kwa mzigo.

“Wafanyabiashara wengi mnashindwa kufikisha malalamiko yenu kwa mamlaka husika kwa sababu hamtumii watoa huduma sahihi,

“Orodha ya watoa huduma ambao wanatambulika kisheria ipo na tutaiwasilisha ubalozini kwetu ili muweze kuwatumia watoa huduma hao waliosajiliwa na kupewa leseni za kufanya huduma hizo na TASAC,” amesema

You Might Also Like

Sagini Amwelezea Kaluta Amir Abeid Ni Alama Ya Kuigwa

Vitongoji 1997  Vimepatiwa Huduma Ya Umeme, Kilimanjaro  

Rais Samia Aweka Jiwe La Msingi Kongani Ya Kwala

Changamoto uchakataji Mkonge kupatiwa ufumbuzi

Simbachawene Asema Serikali Yajivunia Mafanikio TASAF

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Kampeni ya Mama Samia imewafikia zaidi ya watu 4000 mikoa saba
Next Article Rais Samia akisikiliza jambo
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

TPDC Kufikisha Gesi Nchi Nzima  Ndani Ya Miaka Miwili Na Nusu  Kuanzia Sasa
Habari March 11, 2026
Nchimbi Ahimiza Ushirikiano wa Wizara Katika Uhifadhi wa Mazingira
Habari March 10, 2026
Mtaka, Ndunguru Wakubaliana Ujenzi wa Maabara ya Kimkakati Njombe
Habari March 10, 2026
Wataalamu wa Fedha SADC Wakutana Pretoria Kujadili Bajeti
Habari March 9, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?