MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Biteko Agongea Msumari Elimu Ya Ufundi Stadi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Biteko Agongea Msumari Elimu Ya Ufundi Stadi
Habari

Biteko Agongea Msumari Elimu Ya Ufundi Stadi

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi

DAR ES SALAAM: NAIBU Waziri Mkuu ambaye pia ni Waziri Wa Nishati, Dotto Biteko amesema kama kuna mahali panapaswa kuwekezwa mkazo zaidi  ni kwenye ufundi stadi.

Biteko amesema hayo wakati akifunga Maadhimisho ya Miaka 30 ya Uanzishwaji wa Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), yaliyofanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere Dar es Salaam (JNICC).

Akifafanua hilo amesema, tafiti zinaonyesha  ikiwekezwa dola moja kwenye ufundi stadi,  kitakachopatikana ni sawa na kupata dola nne.

“Bahati njema tunapomfundisha mtoto tunamfundisha kwenye nyanja tatu za ujifunzaji. Tunamfundisha kwenye nyanja ya utambuzi, nyanja ya uelekeo pamoja na ustadi,” amesema.

Amesema katika miaka ya karibuni imekuwa ni kawaida kuona mtoto amemaliza kidato cha sita kwa mfano au ana digrii ya kitu Fulani lakini hawezi hata kujipikia chakula mwenyewe au kujifulia.

“Hakuna taifa lolote linaendelea bila kuwekeza watu kwenye stadi Fulani. VETA wakati inaendelea yapo matishio yanayotishia stadi mbalimbali. Tunafundisha watoto wetu na mabadiliko ya tabia ya teknolojia duniani yamekuwa tishio kubwa sana,” amesema.

Pia amesema kwa miongo miwili sasa sekta ya uzalishaji ilishuka kwa asilimia 20 na sekta ya huduma ikapanda kwa asilimia 27, ni kwa sababu ya uwepo wa mitambo ambayo inafanywa na watu wengi zaidi.

Amesisitiza kuwa wakati wanafundisha vijana wanawafundisha kuwa tayari kukabiliana na changamoto zinazokuja.

Vile vile amesema kuwa maadhimisho hayo ya VETA yamefanikiwa kwani uongozi na watumishi wake wameifanya iweze kufurukuta kila mmoja aizungumze kwa mtazamo anaouona.

You Might Also Like

Maziwa Kukuza Uchumi Wa Wafugaji

Sababu Nne Zilizofanikisha Mafanikio Katika Uandikishaji

GIZ, IUCEA waratibu uchambuzi wa data kidijitali kwa wahitimu

Nishati Safi Ya Samia Yawafikia Wanawake chalinze

RAAWU na mafanikio iliyopata utawala wa Rais Samia

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article NIT Yajivunia Uanzishwaji Chuo Cha Marubani
Next Article COSOTA Yapokea Migogoro 136 Ndani Ya Miaka Minne
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Waziri Mkuu Majaliwa Akabidhi Tuzo kwa BoT Geita
Habari September 22, 2025
BoT Yarahisisha Uuzaji wa Dhahabu kwa Wachimbaji, Yatoa Punguzo La Mrabaha
Habari September 22, 2025
Waziri Mkuu Apongeza Huduma Kidijitali za NSSF, Maonesho Ya Madini Geita
Habari September 22, 2025
Mkuu Wa Mkoa Shinyanga Asifu Kazi Ya Bodi Bima Ya Amana
Habari September 22, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?