MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Agnesta Lambart: Nitakuwa Sauti ya Wananchi wa Segerea Bungeni
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Agnesta Lambart: Nitakuwa Sauti ya Wananchi wa Segerea Bungeni
Habari

Agnesta Lambart: Nitakuwa Sauti ya Wananchi wa Segerea Bungeni

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: MBUNGE wa Segerea, Agnesta Lambart (CHAUMA), amesema licha ya upinzani kuwa wachache katika Bunge la 13, anaamini kuwa uwakilishi bora hauhitaji wingi wa wabunge, bali hoja zenye tija kwa maendeleo ya wananchi.
Amesema hayo katika viwanja vya Bunge, leo Novemba 11, 2025 Jijini Dodoma.
“Wingi si kigezo cha ubora. Hata tukiwa wachache, tunaenda kuleta tofauti kubwa ndani ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” amesema Lambart.
Habari Picha 10251
Akimpongeza Spika wa Bunge, Mussa Azzan Zungu amesema ana imani naye kutokana na uzoefu wake kama kiongozi aliyewahi kuwa Naibu Spika, na anaamini Bunge litafanya kazi kwa ushirikiano na serikali katika kuwatumikia wananchi.
Lambart, ambaye amechaguliwa kwa kura zaidi ya 256,000, amesema ushindi wake umetokana na imani ya wananchi waliotambua utendaji wake wakati akiwa mbunge wa Viti Maalum kupitia CHADEMA, ambapo alijipatia heshima kwa hoja zenye mashiko zilizowasilishwa bungeni.
“Wananchi wa Segerea wananitegemea sana. Wanahitaji maendeleo na wanataka sauti yao isikike bungeni. Nitaendelea kusimamia yale yanayowagusa moja kwa moja,” amesema.
Mbunge huyo amesema licha ya Segerea kukua kwa kasi, bado kuna changamoto nyingi katika miundombinu, maji, afya, elimu na uchumi.
“Segerea imesahaulika kwa muda mrefu. Barabara hazipitiki, maji safi na salama hayapatikani, akina mama bado wanatembea umbali mrefu kuchota maji. Nitahakikisha dhana ya ‘Kumtua mama ndoo kichwani’ inatekelezeka kikamilifu katika jimbo langu,” amesema.
Aidha, amesema atahakikisha wananchi wa kipato cha chini, wakiwemo wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, wanapata mikopo isiyo na riba ya asilimia 10 kutoka halmashauri, kama njia ya kuwawezesha kiuchumi.
Akizungumzia elimu, Lambart amesema atapigania kuondoa mzigo wa michango mingi kwa wazazi, kwani sera ya serikali inasema elimu kuanzia darasa la kwanza hadi kidato cha sita ni bure.
“Nitahakikisha shule zangu zinapata ruzuku ya kutosha ili kuwapunguzia wazazi mzigo wa michango, hasa kwa kuwa wengi ni wa kipato cha chini,” amesema.
Mbunge huyo amesisitiza kuwa vipaumbele vyake vikuu ni kuboresha miundombinu, maji safi na salama, afya, elimu na uchumi, akiahidi kufanya kazi kwa bidii kuhakikisha wananchi wa Segerea wananufaika na matunda ya maendeleo.

You Might Also Like

Ridhiwan Kikwete awasilisha taarifa mwenendo wa ulipaji mafao

Zena Ahmed Said Aitaka NSSF Kuimarisha Uhamasishaji wa Uwekezaji kwa Umma

REA Yaupamba Mkutano Wa Kikanda Wa Nishati Bora 2024

Waomba Kuondolewa Vikwazo Vya Biashara Ya Mazao Ya Kilimo Ikolojia Mipakani

Majaliwa: Jiungeni NHIF Kupata Matibabu Ya Uhakika

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Chiku Athumani Aahidi Kusimamia Afya na Elimu kwa Umakini
Next Article Mbunge wa Monduli Aahidi Kusimamia Changamoto za Jimbo Lake
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Nchimbi Ahimiza Ushirikiano wa Wizara Katika Uhifadhi wa Mazingira
Habari March 10, 2026
Mtaka, Ndunguru Wakubaliana Ujenzi wa Maabara ya Kimkakati Njombe
Habari March 10, 2026
Wataalamu wa Fedha SADC Wakutana Pretoria Kujadili Bajeti
Habari March 9, 2026
TASFAM Yawawezesha Wanawake wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Kuadhimisha Siku ya Mwanamke
Habari March 9, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?