MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Mchome: Ubunifu wa VETA Ni Mkubwa, Sasa Ni Wakati Wa Uzalishaji Kwa Wingi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Mchome: Ubunifu wa VETA Ni Mkubwa, Sasa Ni Wakati Wa Uzalishaji Kwa Wingi
Habari

Mchome: Ubunifu wa VETA Ni Mkubwa, Sasa Ni Wakati Wa Uzalishaji Kwa Wingi

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: MWENYEKITI wa Bodi ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), Profesa Sifuni Mchome, ameipongeza VETA kwa hatua kubwa ya ubunifu katika sekta mbalimbali, huku akitoa rai ya kuingia kwenye uzalishaji mkubwa wa bidhaa hizo ili kukidhi mahitaji ya soko.
Profesa Mchome ametoa kauli hiyo alipotembelea banda la VETA katika Maonesho ya Kitaifa ya Kilimo (Nanenane) yanayofanyika mkoani Dodoma, ambapo alishuhudia kazi mbalimbali za ubunifu zinazofanywa na wataalamu na wanafunzi kutoka vituo mbalimbali vya VETA nchini.
Katika ziara hiyo, ameona teknolojia mbalimbali zenye ubunifu wa hali ya juu, ikiwemo mashine za umwagiliaji kwa kutumia nishati ya jua, vifaa vya kuchakata chakula cha mifugo kama kuku, na mavazi ya kisasa yaliyotengenezwa na vijana wa VETA.
Amesisitiza kuwa vifaa hivyo vina uwezo wa kuchochea maendeleo ya sekta ya kilimo na viwanda iwapo vitaingizwa kwenye uzalishaji kwa wingi.
“Nimefurahishwa sana na kazi inayofanywa na VETA. Hii ni hatua kubwa katika ubunifu wa nishati jadidifu, teknolojia ya kilimo na uzalishaji wa mavazi. Sasa ni wakati muafaka kwa VETA kwenda mbele zaidi na kuanza uzalishaji mkubwa wa vifaa hivi. Soko lipo na lina uhitaji mkubwa,” amesema.
Aidha, ameshauri taasisi hiyo kuandaa mkakati mahsusi wa kuongeza uzalishaji wa bidhaa zinazobuniwa ili zisibaki kuwa maonyesho tu, bali ziwe sehemu ya suluhisho la changamoto za maendeleo vijijini na mijini.
“VETA inaweza kuwa sehemu muhimu ya utekelezaji wa Dira ya Maendeleo ya Taifa. Tukizalisha vifaa hivi kwa kiwango kikubwa, tutakuwa tunasaidia wakulima, wafugaji, na sekta nyingine nyingi,” amesema.
Maonesho ya Nanenane ni jukwaa muhimu kwa taasisi kama VETA kuonesha mchango wao katika maendeleo ya sekta ya kilimo, ambapo ubunifu na mafunzo ya vitendo yanayoendeshwa na mamlaka hiyo yameendelea kutambuliwa kama kichocheo cha maendeleo ya uchumi wa viwanda.

You Might Also Like

Vyama Vya Wafanyakazi Vihimize Waajiri Kutoa Taarifa WCF, Zinazohusu Wafanyakazi Wanaopata Ajali, Ugonjwa Kazini

USAID yatoa Dola mil nane Kwa kampuni za Tanzania

Tanzania Yaongoza Kwa Ushiriki, Makongamano Ya Ushirika Ndani, Nje Ya Nchi

Mapinduzi ya Elimu Geita: Wasichana Wamerudi Shule kwa Kasi

Mfumo Wa KieletronikiWa Albino Kurahisisha Kuwatambua – Ridhiwani

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TARI Kibaha Yaboresha Pia Mbegu za Mazao ya Mizizi
Next Article Mazao Ya Mikunde Yatajwa Kuwa Na Kiwango Kikubwa Cha Protini
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Vitabu Vya Sauti Kuvutia Vijana, Serikali Yapongeza Ubunifu Wa Mkuki Na Nyota
Habari November 22, 2025
Ubora Wa E & D Vision Publishing Wamkuna Waziri Kabudi Maonyesho Ya Vitabu Dar
Habari November 22, 2025
Kabudi: Vitabu Ni Tiba, Atoa Wito Kuimarisha Maktaba, Uchapaji 
Habari November 22, 2025
Kwagila Awataka Wasimamizi Wa Elimu TAMISEMI Kuwajibika Kikamilifu
Habari November 21, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?