MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wadau Wakaribishwa Kuwekeza Katika Uchakataji, Biashara ya Mkonge Nchini
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wadau Wakaribishwa Kuwekeza Katika Uchakataji, Biashara ya Mkonge Nchini
Habari

Wadau Wakaribishwa Kuwekeza Katika Uchakataji, Biashara ya Mkonge Nchini

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA: BODI ya Mkonge Tanzania imewataka wadau  mbalimbali kujiunga na mnyororo wa thamani wa mkonge, hususan katika eneo la uchakataji na uongezaji thamani wa zao hilo muhimu kwa uchumi wa taifa.
Mkuu wa Sehemu ya Maendeleo ya Mkonge kutoka Bodi hiyo, Saimon Kibasa ametoa wito huo katika Maonesho ya Nanenane yanayoendelea mkoani Dodoma.
Amesema  lengo ni kuwaelimisha wananchi na wawekezaji kuhusu fursa lukuki zilizopo katika sekta ya mkonge, ikiwa ni pamoja na upatikanaji wa mbegu bora, utaalamu wa kilimo bora cha mkonge, na uwekezaji katika viwanda vya kuchakata zao hilo.
“Serikali ilianza rasmi kampeni ya kuhamasisha kilimo cha mkonge mwaka 2020, na tangu wakati huo, kumekuwa na mwitikio mkubwa kutoka kwa wakulima kote nchini.
“Kwa sasa, zao la mkonge limefikia hatua ya mwisho ya uzalishaji mashambani, na kinachohitajika sasa ni kuongeza uwezo wa kuchakata mkonge ili kuongeza thamani na tija kwa wakulima na taifa kwa ujumla,” amesema.
Amesema Bodi hiyo inakaribisha wawekezaji kuanzisha au kuimarisha viwanda vya kuchakata mkonge, pamoja na kutoa huduma za kuchakata kwa wakulima wadogo, ili kuwawezesha kunufaika na zao hilo.
“Pia kuna fursa kubwa ya kuuza nyuzi za mkonge (singa) zinazozalishwa baada ya uchakataji, ambazo zina mahitaji makubwa katika masoko ya ndani na ya kimataifa, hasa kwenye viwanda vya kutengeneza kamba, mikeka, bidhaa za viwandani na hata nguo,” amesema.
Sekta ya mkonge inatajwa kuwa na mchango mkubwa katika kuongeza kipato cha wakulima, kuboresha ajira vijijini, na kukuza pato la taifa, hivyo inahitaji ushiriki mpana kutoka kwa wadau wa sekta binafsi, taasisi za kifedha, na wajasiriamali.

You Might Also Like

Shemdoe apongeza

Majaliwa Asisitiza Serikali Itaendelea Kuboresha Mazingira Ya Uwekezaji

Tanzania Na Italy Wasaini Makubaliano Kuongeza Ubora Mafunzo Ya Ukarimu

Mpango Awaalika SADC Kutuma Timu ya Uangalizi wa Uchaguzi

CWT Yaiomba Serikali Kurekebisha Sheria za Vyama vya Wafanyakazi

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mramba Afungua Mafunzo Ya Teknolojia Ya Nishati Jua Kwa Watalaam
Next Article Balozi wa Tanzania Nchini Italy Afurahishwa  Ubunifu wa TPHPA Maonesho ya Nanenane
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mwandishi Lucy Ngowi Miongoni mwa Waliong’ara Mei Mosi
Habari May 2, 2026
Tanzania yaendelea kuwa Shule ya Utumishi Barani Afrika,
Habari April 29, 2026
Wizara Ya Kilimo Yaomba Bunge Kuidhinisha Trilioni 1.1,Yaweka Mikakati Kuimarisha Sekta Hiyo
Habari April 28, 2026
NSSF Yafikia Trilioni 11.2, Hifadhi Skimu Yatajwa Kubadili Maisha ya Watanzania
Habari April 27, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?