MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Tume ya Kurekebisha Sheria Yaelimisha Umma Kuhusu Haki za Wanyama
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Tume ya Kurekebisha Sheria Yaelimisha Umma Kuhusu Haki za Wanyama
Habari

Tume ya Kurekebisha Sheria Yaelimisha Umma Kuhusu Haki za Wanyama

Author
By Author
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi
DODOMA; WAFUGAJI wengi nchini hawana ufahamu wa kutosha kuhusu Sheria ya Ustawi wa Wanyama, Sura Na. 154, hali inayosababisha baadhi yao kuwanyima huduma muhimu wanyama wao bila kujua kuwa ni kosa kisheria.
Wakili wa Serikali kutoka Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT),
Vick Mbunde amesema hayo katika  Maonesho ya Wakulima ya Nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma.
Amesema lengo kuu la elimu hiyo ni kuwawezesha wafugaji kufahamu haki na ustawi wa wanyama wanaowafuga, pamoja na wajibu wao kisheria.
“Wafugaji wengi hawafahamu kuwa kuna sheria inayowataka l kuwahudumia vyema wanyama wao, ikiwa ni pamoja na kuwapatia chakula cha kutosha, maji safi, malazi bora na matibabu.
“Sheria hii inalinda wanyama dhidi ya mateso, manyanyaso na mazingira duni ya maisha,” amesema.
Amesema  Sheria ya Ustawi wa Wanyama inatoa adhabu kwa mtu yeyote atakayekiuka masharti hayo, ikiwa ni hatua ya kulinda maslahi ya wanyama wanaofugwa na binadamu.
Katika maonesho hayo, Tume hiyo pia imekuwa ikigawa vipeperushi vyenye maelezo ya msingi kuhusu sheria husika, sambamba na kutoa nafasi kwa wananchi kuuliza maswali na kupatiwa majibu ya kitaalamu kuhusu masuala ya kisheria yanayohusu mifugo na wanyama kwa ujumla.
Hosea Godwin, mmoja wa wafugaji waliotembelea banda la Tume hiyo, amepongeza jitihada hizo na kusema kuwa elimu waliyopata imewasaidia kufahamu masuala ambayo hapo awali walikuwa hawajayazingatia.
“Nilikuwa sifahamu kuwa ukimtesa mnyama, kama kumpiga au kumwacha bila chakula kwa siku kadhaa, ni kosa linaloweza kupelekea kuchukuliwa hatua za kisheria. Hii ni elimu muhimu sana kwetu wafugaji,” amesema Hosea.

You Might Also Like

Chalamila Akabidhi milioni 100, saruji Kukamilisha Zahanati

TPHPA Kuipokea Ndege Yake

TPHPA Tuna Mchango Mkubwa Katika Utoshelevu Wa Chakula – Ndunguru

Swahili International Tourism Expo Kufanyika Oktoba 11 hadi 13

TARI yapongezwa kwa kuwa na teknolojia bora za kilimo

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Bundi Wasaidia Kupambana na Panya: Teknolojia Asilia Inayobadili Maisha ya Wakulima
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Bundi Wasaidia Kupambana na Panya: Teknolojia Asilia Inayobadili Maisha ya Wakulima
Habari August 6, 2025
Ofisa wa TARI Kuwapo Kila Kituo cha Umwagiliaji – Naibu Katibu Mkuu
Habari August 6, 2025
Mbinu Mpya za Kilimo kwa Vijana Zapata Umaarufu Nanenane Banda La VETA
Habari August 6, 2025
VETA Yatahadharisha Changamoto ya Kuzidisha Uchanganyaji wa Chakula Cha Mifugo
Habari August 6, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?