MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Jaji Mwambegele: Habari Sahihi ni Msingi wa Ushiriki Mpana wa Wananchi Kura 2025
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Jaji Mwambegele: Habari Sahihi ni Msingi wa Ushiriki Mpana wa Wananchi Kura 2025
Habari

Jaji Mwambegele: Habari Sahihi ni Msingi wa Ushiriki Mpana wa Wananchi Kura 2025

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Lucy Ngowi 
DAR ES SALAAM:  MWENYEKITI wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Mahakama ya Rufani Jacobs Mwambegele, amewataka waandishi wa habari nchini kutumia taaluma yao kuelimisha umma na kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura ifikapo zOktoba 29, mwaka huu 2025.
Mwambegele amesema hayo leo Agosti mbili. 2025 wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Kitaifa kati ya Tume na Waandishi wa Habari kuhusu Uchaguzi Mkuu.
Jaji Mwambegele amesisitiza kuwa vyombo vya habari ni nguzo muhimu ya kuhakikisha uelewa wa wananchi kuhusu mchakato wa uchaguzi unaimarika.
“Taarifa zenu zinaweza kuleta hamasa ya kitaifa au kuzua sintofahamu. Ni wajibu wa kila mwandishi kuhakikisha anawapa Watanzania habari sahihi, kwa wakati na kwa uwiano unaozingatia maadili ya taaluma,” amesema.
Naye Mkurugenzi wa Uchaguzi,  Kailima Ramadhani amekumbusha wanahabari kuwa na jukumu la kuhakikisha vyama vya siasa na wagombea wanapata fursa ya kusikika kwa haki katika kipindi cha kampeni.
Ametoa wito kwa vyombo vya habari kuzingatia uwiano wa uwasilishaji wa taarifa, bila upendeleo, ili kuimarisha misingi ya kidemokrasia nchini.
Pia amesisitiza umuhimu wa kuandika na kuripoti kwa uangalifu mkubwa ili kuepuka kueneza taarifa zisizo sahihi au zinazoweza kusababisha taharuki.
 Amesema katika kipindi chote cha uchaguzi, waandishi wanapaswa kutumia majukwaa yao kueneza ujumbe wa amani na mshikamano wa kitaifa.
“Uandishi una nguvu ya kuunganisha au kugawanya. Tunawasihi msitumie taaluma yenu kuwavunja moyo wananchi, bali kuwahamasisha kushiriki kikamilifu, kama wapiga kura au wagombea,” amesema.
Mkutano huu ni sehemu ya mfululizo wa mikutano ya wadau mbalimbali iliyoandaliwa na Tume katika maandalizi ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.
Tangu Julai 27, 2025 Tume imekutana na viongozi wa vyama vya siasa, asasi zisizo za kiserikali, wawakilishi wa wanawake, vijana, watu wenye ulemavu na wahariri wa vyombo vya habari.
Mikutano hiyo itahitimishwa Agosti nne, 2025 kwa kikao maalum na waandaji wa maudhui mtandaoni, pamoja na mafunzo kwa wahariri na waandishi wa habari.

You Might Also Like

Mvua, Upepo Yaharibu Shule Lindi, Serikali Yatoa Milioni 96

Ofisi Ya Taifa Ya Takwimu  Kufanya Tafiti Kwa Wakala Wa Huduma Za Fedha,Viwandani

Rais Wa Zanzibar Dkt. Mwinyi Mgeni Rasmi Mkutano Wa THRAPA

Serikali Yazindua Soko Kuu Jipya la Kariakoo Baada ya Moto wa 2021

BoT: Tumia Taasisi za Fedha Halali kwa Usalama wa Kifedha

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article TARURA Yatoa Elimu Nane Nane
Next Article VETA Yatahadharisha Changamoto ya Kuzidisha Uchanganyaji wa Chakula Cha Mifugo
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Tume Ya Ulinzi Wa Taarifa Binafsi Yatoa Siku Saba Kwa Taasisi Kujisajili
Habari June 12, 2026
Teknolojia Ya Juisi YA Ndizi Kali Yafungua Fursa Mpya Za Viwanda, Ajira
Makala Uncategorized June 12, 2026
Serikali Yaingia Makubaliano Ya Ushirikiano Na DIT Kuimarisha Usimamizi Wa Mataifa
Habari June 8, 2026
Wananchi Waelimishwa Masharti ya Kubadilisha Noti Zilizochakaa, Kuungua na Kuchanika
Habari June 7, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?