MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Wakazi Wa Ntyuka Wataka Kiongozi Mchapakazi
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Wakazi Wa Ntyuka Wataka Kiongozi Mchapakazi
Habari

Wakazi Wa Ntyuka Wataka Kiongozi Mchapakazi

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Na Danson Kaijage
DODOMA: BAADHI ya wakazi wa Kata ya Ntyuka, katika Halmashauri ya Jiji la Dodoma, wameeleza matarajio yao ya kupata kiongozi mchapa kazi atakayesaidia kusukuma mbele maendeleo ya eneo hilo.
Kauli hiyo ilitolewa wakati wa kikao cha Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Ntyuka, ambapo wagombea nane waliopitishwa na Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kwa ajili ya kuwania ubunge katika Jimbo la Dodoma Mjini walijitambulisha kwa wajumbe.
Wagombea waliopitishwa ni Samwel Malecela, Rashid Mashaka, Pascal Chinyele, Samwel Kisaro, Fatuma Yusufu Waziri, Robert Mwinje, Rosemeary  Jairo na Abdulhabib Mwanyemba.
Baadhi ya wajumbe walieleza kuwa wanatamani kumpata mbunge anayetoka katika maeneo yao na anayezifahamu changamoto za wananchi, wakibainisha kuwa uelewa wa mazingira ya eneo ni nyenzo muhimu katika utekelezaji wa majukumu ya uwakilishi.
Akizungumza mbele ya wajumbe, mmoja wa wagombea, Samwel Malecela, alieleza kuwa iwapo atapata ridhaa ya kupitishwa kwenye kura za maoni, ataweka kipaumbele kwenye kushughulikia changamoto mbalimbali, ikiwemo masuala ya ardhi.
“Jimbo la Dodoma Mjini lina jumla ya kata 21, na kila kata ina changamoto zake. Nia yangu ni kuhakikisha kuwa sauti za wananchi zinasikika bungeni na changamoto zao zinapatiwa majibu kupitia ushirikiano wa pamoja,” amesema Malecela.
Kura za maoni ndani ya chama hicho zinatarajiwa kufanyika hivi karibuni ili kumpata mgombea atakayepeperusha bendera ya CCM katika uchaguzi mkuu ujao kwa Jimbo la Dodoma Mjini.

You Might Also Like

July 10, 2025

MBUNGE wa Kasulu Mjini Ahoji Serikali Kuhusu Mradi wa Maji Mwanga B

Ajira kwa Vijana na Afya kwa Wazee: Ajenda Kuu za Wagombea Jimbo la Dodoma Mjini

UDSM  Kujenga Jengo La Kisasa La Bil 8.3

Hazina yaanza kuwalipa wanachama 465 wa TALGWU

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Kisaro Ahojiwa Kuhusu Migogoro ya Ardhi,  Mwinje Ajitosa na Suluhisho la Miundombinu na Umiliki wa Ardhi
Next Article TARURA Yatoa Elimu Nane Nane
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Serikali Yaingia Makubaliano Ya Ushirikiano Na DIT Kuimarisha Usimamizi Wa Mataifa
Habari June 8, 2026
Wananchi Waelimishwa Masharti ya Kubadilisha Noti Zilizochakaa, Kuungua na Kuchanika
Habari June 7, 2026
DMI Yawaalika Vijana Kujiunga Na Masomo Ya Ubaharia
Habari June 6, 2026
Taifa Gas Yaendelea Kuongoza Kampeni ya Nishati Safi kwa Taasisi na Sekta ya Utalii Tanzania
Habari June 6, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?