MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Ikomba: Aliishi Na Watoto Wiki Sita Akiwafundisha Kabla Ya Mtihani WaTaifa
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Ikomba: Aliishi Na Watoto Wiki Sita Akiwafundisha Kabla Ya Mtihani WaTaifa
Habari

Ikomba: Aliishi Na Watoto Wiki Sita Akiwafundisha Kabla Ya Mtihani WaTaifa

Author
By Author
Share
3 Min Read
Na Lucy Ngowi
DAR ES SALAAM: RAIS mpya wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Mwalimu Suleiman Ikomba, amekuwa kiongozi wa mfano kutokana na historia yake ya kujitoa na kujituma kwa miaka mingi katika kuwahudumia watoto wanaotoka kwenye mazingira magumu.
Ikomba akizungumza na Mfanyakazi Tanzania, ameeleza namna alivyowalea watoto kutoka familia maskini kwa miaka mingi akiwa mwalimu na Mkuu wa Shule katika maeneo mbalimbali, ikiwemo Wilaya ya Temeke Dar es Salaam.
“Nilikaa na watoto ambao wazazi wao hawakuwa na uwezo nyumbani kwangu kwa wiki sita kabla ya kufanyika Mtihani wa Taifa wa darasa la saba ili niwaandae.
“Wengi wao hawakuwa na mazingira mazuri ya kusoma. Niliwaleta nyumbani, nikatafuta chakula, na nikawasimamia masomo mpaka wakati wa mtihani” amesema Mwalimu Ikomba.
Amesema alianza kazi ya ualimu mwaka 1991, kipindi ambacho ada za shule zilikuwa kikwazo kikubwa kwa watoto wengi kutoka familia za kipato cha chini.
“Nikiwa Mkuu wa Shule, nilikusanya watoto wote waliokuwa hawawezi kulipia ada au mahitaji mengine.
“Nikiwa na mke wangu ambaye pia alikuwa mwalimu, tuliwalea hawa watoto  walikula, walisoma na kulala kwetu mpaka tukahakikisha wamefikia malengo yao,” amesema.
Amesema mmoja wa watoto aliowalea kipindi hicho ambaye kwa sasa ameajiriwa, aliungana naye katika kampeni za kuwania urais wa CWT, akionyesha mshikamano na shukrani kwa kile alichofanyiwa na mwalimu huyo huko nyuma.
Amesema katika Shule za Msingi Minazini na Mtoni kwa Mama Mary, Wilaya ya Temeke, Mwalimu Ikomba alianzisha utaratibu wa kup1rishi na wanafunzi wanaotoka katika familia masikini kwa muda wa siku 40 kabla ya mitihani ya kitaifa, kwa lengo la kuwapa fursa ya kujifunza kwa ukaribu zaidi.
“Niliamini kuwa njia ya kweli ya kumkomboa mtoto wa maskini ni kumwezesha kielimu. Hata kama hakuwa na sare, viatu au chakula, nilihakikisha anapata elimu,” amesema.
Amesema katika shule zote alizopita mtu akiulizia kipindi chake kilikuaje, watamuelezea moyo wa kusaidia watoto aliokuwa nao.
Licha ya kujitoa kwake, Mwalimu Ikomba amesema kuna wakati aliumizwa na wazazi kushindwa kuwapeleka watoto shule kutokana na hali ngumu ya maisha.
Amesema hali hiyo ilimvunja moyo kwani hakuweza kuwasaidia watoto ambao hawakufika shuleni.
“Nilikuwa nasubiri watoto wafike, halafu nipambane kuhakikisha wanasoma. Lakini kama hawafiki, nilijisikia kushindwa,” amesema.
Kwa mujibu wa walimu na wazazi waliowahi kushirikiana naye, jina la Mwalimu Ikomba linaenziwa katika maeneo aliyofanyia kazi.
Kwa kuwa Wengi wanamtaja kama kiongozi asiyechoka, aliyewahi hata kushirikiana na taasisi mbalimbali za misaada ili kuhakikisha watoto wa mazingira duni wanapata elimu bora.

You Might Also Like

Udongo wa kupandia mboga mboga unapatikana VETA

Nishati Safi Ya Samia Yawafikia Wanawake chalinze

TPHPA Yanunua Ndege Kudhibiti Visumbufu Vya Mazao

Maboresho sheria, kanuni za madini yameongeza mapato

Wanazuoni Kujadili   Dira  Itakayojenga  Uchumi Unaofikia   Dola Trilioni Moja

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Samia Aleta Mapinduzi Arusha
Next Article Vijana Ni Chachu Ya Maendeleo Endelevu Wakiwezeshwa-Kikwete
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Mapinduzi ya Elimu Geita: Wasichana Wamerudi Shule kwa Kasi
Habari July 21, 2025
Vijana Ni Chachu Ya Maendeleo Endelevu Wakiwezeshwa-Kikwete
Habari July 21, 2025
Samia Aleta Mapinduzi Arusha
Habari July 21, 2025
Rais CWT Asikitishwa Na Uzembe, Maofisa Wa Halmashauri
Habari July 20, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?