MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Tanzania Yaingia Saba Bora Duniani  Kwa Uzalishaji Wa Pamba Hai
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Tanzania Yaingia Saba Bora Duniani  Kwa Uzalishaji Wa Pamba Hai
Habari

Tanzania Yaingia Saba Bora Duniani  Kwa Uzalishaji Wa Pamba Hai

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
Simiyu Kinara Kitaifa
Na Danson Kaijage – Dodoma
DODOMA: TANZANIA inashika nafasi ya saba duniani kwa uzalishaji wa pamba hai, huku Mkoa wa Simiyu ukitajwa kuwa kinara wa kitaifa katika kilimo hicho chenye tija kwa wakulima.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Anamlingi Macha amesema hayo alipozungumza na waandishi wa Habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari (Maelezo) jijini Dodoma alipokuwa akielezea mafanikio ya serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan.
“Kwa sasa zaidi ya asilimia 60 ya pamba yote nchini huzalishwa Simiyu, na uzalishaji umeongezeka kutoka tani 64,594 mwaka 2020 hadi kufikia tani 140,000 mwaka 2024,” amesema.
Amesema Simiyu ndiyo mkoa pekee nchini unaolima pamba hai, ambapo uzalishaji wake umeongezeka kutoka tani 10,300 msimu wa 2021/2022 hadi tani 12,285 msimu wa 2022/2023, nyuma ya mataifa kama China, India, Uturuki na Pakistan.
Amesema hatua hiyo imeiwezesha Tanzania kushika nafasi ya saba duniani katika uzalishaji wa pamba hai.
Amepongeza serikali kwa kufanikisha uboreshaji wa miundombinu ya kilimo, usambazaji wa pembejeo kwa wakati, na uwepo wa wataalamu wa kutosha wa kilimo ambao wamewasaidia wakulima kuongeza tija.
Amesema Chama Kikuu cha Ushirika cha Mkoa wa Simiyu (SIMCU 2018 Ltd) kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB), kimefanikiwa kufufua kiwanda cha kuchakata pamba cha Sola Ginnery kilichopo Wilaya ya Maswa kwa gharama ya Sh. Bilioni 4.0.
“Kiwanda hiki kimeongeza thamani ya pamba kwa wakulima wetu, kimetoa ajira kwa vijana, na pia kimepunguza gharama za usafirishaji wa mazao,” amesema.
Vilevile, Mkoa wa Simiyu umeendelea kuboresha huduma za ugani kwa kuwapatia maofisa ugani vifaa vya kisasa, pamoja na kuwezesha wakulima kwa mikopo midogo ya kilimo kutoka taasisi za kifedha.
“Pamba siyo zao tu, bali ni uti wa mgongo wa uchumi wa wakazi wa Simiyu. Tunaishukuru Serikali kwa kuwezesha mapinduzi haya ya kilimo,” amesena.

You Might Also Like

Fursa za Uwekezaji Kanda ya Ziwa: Buzwagi na Maeneo Mengine ya Kimkakati

MAIPAC Yagawa Bure  Majiko Ya Gesi Monduli, Lowassa Apongeza.             

Tanzania Na Africa50 Wazidi Kuimarisha Ushirikiano

Mwalim: Niko Tayari Kushirikiana na Majaliwa Nikipewa Ridhaa ya Urais

Uzalishaji wa chuma kuanza nchini 

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Mara Yapaa: Miaka Minne Ya Mafanikio Chini Ya Rais Samia
Next Article Uvuvi Wa Kisasa Wainua Mwanza Kiuchumi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Twendeni Tukapige Kura Ya Ukombozi, CHAUMMA Yahitimisha Kampeni
Habari October 28, 2025
Elimu Ya Nishati Safi Ya Kupikia Yawafikia Maofisa Dawati Ngazi Ya Mikoa Na Halmashauri
Habari October 27, 2025
Wananchi wahamasishwa kuandika historia mpya kupitia kura
Habari October 25, 2025
Shibuda: WanaMaswa jitokezeni kupiga kura bila woga
Habari October 25, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?