MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: Pato la Mwananchi Lapanda Tabora
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > Pato la Mwananchi Lapanda Tabora
Habari

Pato la Mwananchi Lapanda Tabora

Lucy Ngowi
By Lucy Ngowi
Share
2 Min Read
– Uzalishaji wa Asali Wapaa, Uhifadhi Waongeza Mvuto wa Uwekezaji
Na Danson Kaijage
DODOMA: KATIKA kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, Mkoa wa Tabora umeonyesha mafanikio makubwa kiuchumi, kijamii na kimazingira, huku pato la mwananchi mmoja likipanda kutoka Sh. Milioni 1.77 mwaka 2020 hadi Sh. Milioni 1.85 mwaka 2024, sawa na ongezeko la asilimia 4.5.
Akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Jijini Dodoma, Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paulo Chacha amesema mafanikio hayo ni matokeo ya juhudi za kisekta zilizolenga kuimarisha uzalishaji, kuhifadhi mazingira, na kuvutia uwekezaji.
“Pato la mkoa limeongezeka kutoka Sh. Trilioni 5.4 mwaka 2020 hadi Trilioni 6.3 mwaka 2024. Tabora sasa ni kinara wa maendeleo yanayomgusa mwananchi wa kawaida,” amesema.
Kwa mujibu wa Chacha, uchumi wa mkoa huo umejengwa juu ya kilimo na ufugaji ambavyo huchangia asilimia 70 ya pato la mkoa.
Amesema mazao ya chakula yanayolimwa kwa wingi ni pamoja na mahindi, mpunga, mtama, muhogo, viazi vitamu, uwele na jamii ya mikunde; huku tumbaku, pamba, alizeti, karanga na mchikichi yakiwa ndiyo mazao ya biashara yanayoongoza.
Amesema serikali imetoa zaidi ya Sh. Bilioni 52.8 kwa ajili ya ruzuku ya mbolea, mbegu bora na miradi ya umwagiliaji.
Amesema skimu za umwagiliaji zimeongezeka kutoka 25 mwaka 2020 hadi 46 mwaka 2025, huku eneo la umwagiliaji likipanuka kutoka ekari 16,453.25 hadi ekari 37,560.25.
Kwa upande mwingine amesema mkoa huo ni maarufu kwa uzalishaji wa asali, umeweka historia mpya kwa kufanikisha ujenzi wa viwanda vinne vya kuchakata na kufungasha asali.
Uzalishaji umeongezeka kutoka tani 1,868.6 mwaka 2020 hadi tani 2,002.48 mwaka 2025.
“Mafanikio haya yanatokana na mikakati ya kuwajengea uwezo wafugaji wa nyuki na kuvutia wawekezaji katika sekta hii muhimu,” amesema.
Amesena katika jitihada za kulinda mazingira, misitu ya vijiji imeongezeka kutoka sita mwaka 2020 hadi misitu 37 mwaka 2025, zikiwa na jumla ya ekari 330,780.75 hali iliyochangia kudhibiti uharibifu wa mazingira na kuimarisha vyanzo vya maji, hali inayochochea tija katika kilimo na ufugaji wa nyuki.

You Might Also Like

VETA Yaleta Mapinduzi ya Kilimo na Biashara Kupitia Bunifu –  Profesa Nombo

PBPA Yaagizwa Kuharakisha Upokeaji Na Usambazaji Wa Mafuta Nchini

Naibu Waziri Katambi aagiza CMA kutoa mafunzo kwa njia ya mtandao

OUT Yawanoa Watumishi Wa Mamlaka Za Serikali Za Mitaa

Simbachawene Ashauri Suluhu ya Mafuriko Mpwapwa

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article FCC Yapongezwa Kukabili Bidhaa Bandia
Next Article OCPD Nguzo Kuu ya Utungaji Sheria – Dkt. Ndumbaro
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

TPHPA Yatumia Mbinu za Kibaiolojia Kudhibiti Gugu Ziwa Victoria
Habari May 24, 2026
Wizara Ya Viwanda Kutekeleza Vipaumbele Saba, Ipo  Miradi Ya Viwanda Ya  Kimkakati
Habari May 22, 2026
Biashara 15 Hazitakiwi Kufanywa Na Wageni Ndani Ya Nchi
Habari May 22, 2026
Wadau wataka mifumo jumuishi kupunguza mzigo wa malezi kwa wenye ulemavu
Habari May 21, 2026
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?