MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
Magazeti
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Habari Mpya
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Chagua hapa
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
  • Advertise
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Reading: VETA: Miaka 30 ya Kuinua Ujuzi na Kuunda Wataalamu wa Kesho
Share
Notification Show More
Font ResizerAa
Font ResizerAa
MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Search
  • Home
  • Habari
  • Mfanyakazi
  • Magazeti
  • Bookmarks
Follow US
© 2022 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
MFANYAKAZI TANZANIA > Tovuti > Habari > VETA: Miaka 30 ya Kuinua Ujuzi na Kuunda Wataalamu wa Kesho
Habari

VETA: Miaka 30 ya Kuinua Ujuzi na Kuunda Wataalamu wa Kesho

Author
By Author
Share
4 Min Read

Na Lucy Ngowi

DODOMA:MAMLAKA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imejidhihirisha kuwa chombo muhimu si tu cha kutoa elimu ya ufundi, bali pia cha kuchochea maendeleo ya kiuchumi kupitia uzalishaji wa bidhaa na huduma zinazokidhi mahitaji ya soko la ajira la sasa.

Hilo limeonekana katika kipindi cha miaka 30 tangu kuanzishwa kwake.

Mtaalamu wa ubunifu na ujenzi wa majengo kutoka VETA Makao Makuu, Joseph Mchanake, amesema hayo katika banda la mamlaka hiyo katika maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara yanayoendelea mkoani Dar es Salaam.

Amesema mafanikio ya taasisi hiyo ni ushahidi wa dira, dhamira na utekelezaji wa mipango inayozingatia mahitaji halisi ya taifa.

“Leo hii mafundi wanaohitimu kutoka VETA hawajiandai tu kwa soko la ajira, bali pia wanazalisha bidhaa halisi wakati wa mafunzo yao, jambo linalowaweka moja kwa moja kwenye mazingira ya kiuchumi,” amesema Mchanake.

Amesema kupitia tafiti za kila mwaka za soko la ajira, VETA imekuwa ikibaini kwa usahihi aina ya fani, bidhaa na teknolojia zinazohitajika sokoni, hali inayoifanya taasisi hiyo isalie kuwa hai na yenye kuakisi mahitaji ya wakati.

Amesema mwaka 2021, VETA ilikuwa na vyuo 47 nchini kote lakini hadi kufikia mwaka huu, 2025 idadi hiyo imeongezeka hadi vyuo 80, huku serikali ikiendelea na ujenzi wa vyuo vingine 65 — vyuo vya wilaya 64 na chuo kimoja cha mkoa.

“Lengo ni kuhakikisha karibu kila mkazi wa Tanzania anaweza kupata elimu ya ufundi stadi bila kulazimika kusafiri umbali mrefu,” amesema.

Kwa maelezo yake, kila eneo lina fani zinazolenga kuchakata maliasili na fursa za kipekee za kijiografia na kutolea mfano Kanda ya Ziwa kwamba wanatiloa mafunzo ya zana za uvuvi na uchakataji wa mazao ya samaki.

Mkoani Arusha ni Utalii na huduma za wageni, Mtwara ni Kilimo cha korosho na uzalishaji wa bidhaa zake.

Amesema ushirikiano kati ya VETA na viwanda umekuwa na matokeo makubwa kwa kuwa wafanyakazi wa viwanda hupatiwa mafunzo ya kuongeza ujuzi, huku wanafunzi wa VETA wakipewa nafasi za mafunzo kwa vitendo jambo linalowaandaa vizuri kwa ajira.

Kwenye upande wa sekta ya madini, amesema VETA haina machimbo yake, lakini kwa kushirikiana na sekta hiyo, vijana hupatiwa mafunzo ya kitaaluma ya uchimbaji na uchenjuaji, kisha hupelekwa machimboni kupata uzoefu wa moja kwa moja.

Vile vile amesema, VETA imekuwa mstari wa mbele kurasimisha ujuzi wa mafundi waliopata maarifa kwa njia zisizo rasmi.

“Tunawafuata walipo, tunawapima, tunawapa mafunzo ya ziada kama kunahitajika, kisha tunawapa vyeti vinavyotambulika kisheria,” amesema.

Amesema vyeti hivyo huwasaidia mafundi hao kuomba ajira kwenye taasisi rasmi na kuongeza wigo wa kipato chao.

Kuhusu makundi maalum, amesema kwa kushirikiana na serikali na wahisani, VETA hutoa mafunzo ya ujasiriamali kwa wajasiriamali wadogo na wa kati. Wanawake, wajasiriamali wa samia, mama lishe na makundi maalum kama watu wenye ulemavu pia wamekuwa wakifikiwa kupitia programu maalum.

“Hatuwaoni kama watu wa kusaidiwa bali kama mafundi halali wanaostahili nafasi sawa. Idadi ya wanafunzi wenye ulemavu imeongezeka kutoka nane hadi 362 kwa mwaka,” amesema.

Amesema falsafa ya VETA inaelekeza kuwa ujuzi ni silaha ya kiuchumi. Kila mwanafunzi hufundishwa kujiamini, kuanzisha biashara, kuajiri wengine, au kuwa tayari kwa soko la ajira rasmi.

“Kwa sasa, zaidi ya wanafunzi 83,000 wanadailiwa kila mwaka, ikilinganishwa na wanafunzi 1,940 wa mwanzo. Ongezeko hilo linaendana na ongezeko la vyuo na fani nchini,” amesema.

You Might Also Like

Watumishi wa Umma wafahamu haki ya rufaa Kwa mujibu wa sheria

UDOM yashauri matumizi ya green house kupata tija

TUGHE: Wafanyakazi wapewe haki ya kujiunga vyama vya wafanyakazi

Tutuba: Noti Mpya Kuanza Kutumika Februari Mosi mwaka huu

Waziri Ridhiwani Akutana Na Balozi Wa Japan Nchini,  Wazungumzia Vijana

Share This Article
Facebook Twitter Whatsapp Whatsapp Email Copy Link Print
Previous Article Vyombo vya Habari ni Kama Maji’ -Biteko 
Next Article PURA Yajivunia Agenda Ya Matumizi Ya Nishati Safi
Leave a comment Leave a comment

Leave a Reply Cancel reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Stay Connected

235.3kFollowersLike
69.1kFollowersFollow
11.6kFollowersPin
56.4kFollowersFollow
136kSubscribersSubscribe
4.4kFollowersFollow
- Advertisement -
Ad imageAd image

Latest News

Tanzania, Comoro Zaongeza Ushirikiano wa Lugha
Habari July 10, 2025
TSB Yasisitiza Umuhimu Kuwekeza Kwenye Uchakataji Wa Mkonge
Habari July 10, 2025
eGA Yatengeneza  Mifumo  Kurahisisha  Kazi
Habari July 10, 2025
July 10, 2025
Habari July 10, 2025
//

To be acknowledged as Africa’s premier and most reliable digital media network, delivering exceptional content across all our platforms by 2025.

Sign Up for Our Newsletter

Subscribe to our newsletter to get our newest articles instantly!

MFANYAKAZI TANZANIAMFANYAKAZI TANZANIA
Follow US
© 2024 Mfanyakazi Tanzania. All Rights Reserved.
Welcome Back!

Sign in to your account

Lost your password?